Watu wengi siyo waoga ila wanapenda uoga ndiyo maana wanatia hofu au kutia hofu wenzao...
Ukweli ni kwamba hakuna cha kuogopa Duniani labda maeneo mengine ambayo hatuna maelezo yake kwa usahihi.
Kuna aina ya kuzika kwa kula mzoga mbona hatuisemi wakati miili yetu ni makaburi ya kuku,ngombe,wadudu kama senene,mende na panzi?mbona hayo hatuyasemi.
Tunajifunza kula carcasses siyo kwa kwanza kula miili ya watu ila kwa kupenda sana kula miili ya wanyama ni kama kujifunza kuendesha gari kwa kuendesha upepo na kuunguruma mwenyewe kama gari ili kutunza matamanio na uwezo wa akili kuumba tukio halisi.
Jamii ya watu inatabia za hatari na zinazoibua taharuki na kuwaogofya wengine kuliko jamii za viumbe wengine huku ikijificha kwenye kigezo cha ustaarabu.
Woga ni zao la utamaduni tunaojifunza na siyo asili tuliyoumbiwa,waoga na wanowatia wenzao hofu ni zao la jamii kwa sababu wanayoyafundisha yametokana na utamaduni wa jamii.
Ukitakakuamini jifunze kwa mtoto mdogo ambaye hajachafuliwa akili yake na utamaduni wa jamii utastaajabu sana.