K/koo: Kipande cha Sabuni badala ya simu

K/koo: Kipande cha Sabuni badala ya simu

kabla ya kutoa pesa chukua kagua kwanza kikiwa chenyewe husimrudishie ili akuwekee katika mfuko. mwambie mfuko utanunua mwenyewe, ukipugi ukampa akuwekee yeye umepigwa. Wakikuona unawakazia wanajifanya hawauzi tena. wale wa karata tatu husicheze kamwe utaliwa tu. wanaojifanya wanacheza nao ni wenzao. Ntakuja na uzi mwingine kuonesha namna wanvyotuibia
Mkuu mda huo wa kumwambia hivyo utaupata wapi?

Wakati huo akili si yako tena kaka!
 
Nakumbuka 2011,chupchup buguruni nipigwe,kwa bahat nzuri sehemu waliokuwa wanaisema mm ndio nikawa nimepita kama dakika tano,hiv so wakaferi kwa njia hiyo
 
Ha ha hA kuna ndugu yangu alitapeliwa, kapewa kijiti cha muhogo mwanzo aliona ni almasi mpk leo tangu 1999 jamaa jina lilibadilika anaitwa Almasi.

Mimi kariakoo nilishapigwa elfu 5 tu. Kama sikosei ilikuwa 2003. Jamaa aliniuzia jinzi kwa bei ya tsh 7000 dah nikatoa fasta, ile nampa akasema bro nimesema 17000/= nikamwambia nipe pesa yangu, akanirudishia fasta kumbe juu kanipa elfu 2 ndan kaifungia karatasi la box, ile elfu 5 kachukua, naenda mbele kufungua nakuta nna elf 2 na box basi, tangu siku iyo sijawai ibiwa wala tapeliwa.

Mkasa wa kuuziwa jinsi na mimi ulinikuta 2007 pale kariakoo mtaa wa kongo, jamaa kaja na jeans kali akasema anauza elfu sita tu! nikashangaa mzee nikatoa fasta elfu moja moja sita nikampa huku nikiishika jeans huku nikiikagua vizuri.

ile nataka niondoke jamaa akanigeuzia kibao eti jeans kama ile nitaipataje kwa buku 6! akasema chukua pesa yako! hah! akili ikachemka ile nachukua nakuta elfu 2 na kipande cha box! nikambadilikia sura akanipa pesa yangu yote nami nikampa jeans yake na alipotea ghafla.

Kilichonishangaza watu walikua pembeni wanaangalia tu jinsi nilivyokua naingizwa mjini! ila hiyo ya sabuni nilikua makini sana hasa pale ubungo mataa! wanawaonea sana wasafiri.
 
Mi nakumbuka baada ya kumaliza darasa la saba nikaenda Dar kufanya majaribio shule mbalimbali,siku moja nikakuta wale jamaa wanaokunja mkanda alafu ukichoma katikati unakula mara mbili ya fedha uliyoweka.
Wakaniambia kujaribu ni bure, nikajaribu ya kwanza, kuzungusha mkanda peni iko kati,nikajaribu ya pili peni iko kati,nikajua wajinga hawa nikakimbia home fasta, nikachukua elfu mbili( ya enzi izo) ndio nilikuwa nimebaki nayo tuu,nawahi eneo la tukio ili niwakute bado wapo.
Nikatoa 2000 alafu nikachoma peni,jamaa kuzungusha peni iko nje, nikaanza kuyahisi machozi kwa mbaali ila ndio basi tena.
 
Mimi ubungo niko narudi arusha, nikanunua magazeti nikiwa ndani ya basi, muuzaji yuko chini nikacheck headings nikanunua magazeti 3,basi limeondoka nakuja kuyacheki kumbe ya mwaka 2002 hapo ilikua mwaka 2004
Mimi ubungo niko narudi arusha, nikanunua magazeti nikiwa ndani ya basi, muuzaji yuko chini nikacheck headings nikanunua magazeti 3,basi limeondoka nakuja kuyacheki kumbe ya mwaka 2002 hapo ilikua mwaka 2004
Mimi ubungo niko narudi arusha, nikanunua magazeti nikiwa ndani ya basi, muuzaji yuko chini nikacheck headings nikanunua magazeti 3,basi limeondoka nakuja kuyacheki kumbe ya mwaka 2002 hapo ilikua mwaka 2004
Hii ndio kali kuliko zote..........!!
 
Mi nakumbuka baada ya kumaliza darasa la saba nikaenda Dar kufanya majaribio shule mbalimbali,siku moja nikakuta wale jamaa wanaokunja mkanda alafu ukichoma katikati unakula mara mbili ya fedha uliyoweka.
Wakaniambia kujaribu ni bure, nikajaribu ya kwanza, kuzungusha mkanda peni iko kati,nikajaribu ya pili peni iko kati,nikajua wajinga hawa nikakimbia home fasta, nikachukua elfu mbili( ya enzi izo) ndio nilikuwa nimebaki nayo tuu,nawahi eneo la tukio ili niwakute bado wapo.
Nikatoa 2000 alafu nikachoma peni,jamaa kuzungusha peni iko nje, nikaanza kuyahisi machozi kwa mbaali ila ndio basi tena.
Hiyo nakumbuka nilishuhudia ngumi,
 
Mimi ubungo niko narudi arusha, nikanunua magazeti nikiwa ndani ya basi, muuzaji yuko chini nikacheck headings nikanunua magazeti 3,basi limeondoka nakuja kuyacheki kumbe ya mwaka 2002 hapo ilikua mwaka 2004
Na marashi watu wamepigwa sana ubungo
 
Binafsi niliingizwa chaka kariakoo kwa kununua kipande cha sabuni badala ya simu mwaka 2006. Akaniambia ameiba mtaa wa pili hivyo nimpoze kidogo anipe, tena nifanye fasta atakutwa. nikamwambia sikuwa nimejiandaa kununua simu kwa siku hiyo. hivyo ntampa sh 20,000. akadai nimuongeze kidogo nikaona niokoe muda nikamuongezea sh 10000, zikawa sh 30,000. ile cmu dukani ilikuwa inauzwa 80,000. Sijuhi ilikuwaje nikageuka upande wa pili, ndo likawa kosa kubwa nikakuta jamaa ameshaniwekea katika box na mfuko akaniambia nikafungulie mbele. Nifanye fasta niondoke nikikutwa nitajijua. Kwa spidi ya 4G nikaingia ktk bus siti ya nyuma niliyokaa. Nikasubiri bus lianze kuondoka nikafungua kuona simu yangu. Looohooooo ni kipande cha sabuni(mbuni). Niliona giza........!
Nawe tuambie uliingizwaje chaka town?

Hili nadhani ni tukio la kweli na nimecheka kwa sababu umempa tapeli hela yako halafu unakimbia na kipande cha sabuni ulichouziwa kwa Tzs 30,000!!
 
Hii ndio kali kuliko zote..........!!
MI NILISHAWAHI KUINGIZWA CHAKA PALE KITUO KIDOGO CHA DALADALA NIKATAKA SIJUI KASHESHE VILE UKRASA WA JUU KASHESHE KWELI YA NDANI YOOOTE NI MCHANGANYIKO NA NI MIAKA TOFAUTI NILICHOKA SANA ASEE
 
Nakumbuka 2011,chupchup buguruni nipigwe,kwa bahat nzuri sehemu waliokuwa wanaisema mm ndio nikawa nimepita kama dakika tano,hiv so wakaferi kwa njia hiyo

Upigwe kwa sababu gani, fafanua kidogo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom