K Basil sasa ni askofu chini ya kanisa la Gwajima

K Basil sasa ni askofu chini ya kanisa la Gwajima

PAULO kabla hajaokoka alikuwa anaitwa Sauli na alikuwa anawauwa wafuasi wa Yesu waliokuwa wanahuburi habari za Yesu kama stephano.
Lakini baada ya SAULI kuokoka akaitwa Paulo ,akaanza kuhuburi injili
,sasa kama tungemuhukumu kwa matendo yake ya nyuma ,Mungu alimuita kutumika kutoka muuaji wa wahubiri wa Yesu/mpinga kristo hadi kuwa muhubiri wa Yesu aliyekuwa anampinga mwanzo.
Ndivyo pia hata leo watu waliokuwa wanatumika matendo ya kale ya kidunia wanabadilishwa kumtumikia Mungu ,Ya kale yanapita yanakuwa mapya.
Kumtumikia Mungu hakuhitaji elimu ya Physics na Chemistry na Biology au mathematics au rocket science ,ni kujazwa nguvu ya rohoni ambayo inatoka kwa Mungu mwenyewe.Na huyo roho wa Mungu atawaongoza na kuwafundishaa jinsi ya kuwalisha na kuwachunga kondoo wake.
 
Aiseeeeeee... kweli ndio maana sitokaa nihame kanisa Takatifu Katoliki... ili uwe walau padre tu unahitaji degree mbili... haya makanisa ya kikanjanja yanaokota watu mtaani kesho wamekuwa maaskofu... dah...
La degree si kweli, ila navojua Catholic huwa inawaendeleza makasisi kielimu tu wanakuwa na professions zao
 

Attachments

  • Screenshot_20250623-083841_Chrome.jpg
    Screenshot_20250623-083841_Chrome.jpg
    278.9 KB · Views: 20
Aiseeeeeee... kweli ndio maana sitokaa nihame kanisa Takatifu Katoliki... ili uwe walau padre tu unahitaji degree mbili... haya makanisa ya kikanjanja yanaokota watu mtaani kesho wamekuwa maaskofu... dah...
Kwani ndo yalikua maagizo ya mtoto wa mungu Yesu mpk uwe degree ndo uwe kiongozi wa kanisani..?
Halafu isitoshe hao ni walokole Yesu kwao ni mungu nyie wakatoliki ni mtoto wa mungu so try to stay on your line
 
Aiseeeeeee... kweli ndio maana sitokaa nihame kanisa Takatifu Katoliki... ili uwe walau padre tu unahitaji degree mbili... haya makanisa ya kikanjanja yanaokota watu mtaani kesho wamekuwa maaskofu... dah...
Mapadre kibao wana degree 1 kibao na wengine form 6 wapo nisichoona tu wa form 4
 
Mm sijui sana mambo ya dini ila baada ya kusoma comments zote naomba nitoe hukumu juu ya hili.

Baada ya kusikiliza pande zote za walokole (kwenye kesi hii washitakuwa )na kusikiliza hoja za wakatoliki na madhehebu kongwe ya kikristo ikiwemo wasio WAKRISTO mfano waislamu(washitaki )

Mahakama yangu ili kufikia maamuzi imepitia hoja zifuatazo na kuzidadavua kabla ya kuhukumu.
1.shaka juu ya historia ya mwenendo wa Askofu Basil
TAFAKURI
Mahakama ilitupilia mbali hili kwani ukuaji kiroho hauhusiani na historia wala kuzuiwa na ,msambazaji mkuu wa ukristo mtume paulo aliwahi kuwa muuaji wa wakristo ,papa fransis aliwahi kuwa baunsa wa club za kujiuza .watu washenzi kabisa ndio walioslimu na kueneza vyema uislamu
2.Shaka juu ya elimu ya kidini na kidunia ya Askofu Basil
TAFAKURI
Mahakama ilijiridhisha bila shaka kuwa mshukiwa ni msomi wa kiasi cha degree na muumini wa muda mrefu muaminifu wa Kanisa la ufufuo na uzima .
Aidha pamoja na ukweli kuwa viongozi wa kwanza wa kiroho kama yesu nq mitume wake walikuwa wengi wahuni na watu wasiofaa kwenye jamii mfano petro alikuwa mvuvi mshirikina ,muhamadi alikuwa mtoto wa mjini na marioo wa hadija .
Mahakama imechagua kuheshimu taratibu za kila dini .Tuhuma za ulawiti ,ulevi na uzinzi za viongozi wa kanisa katoliki mahakama ilizikuta pia kwa mashehe huko madrasa kwa kiwango kilekile .aidha tuhuma za kuzaa na frola mbasha za Askofu gwajima ,tuhuma za ulevi za mzee wa upako ,tuhuma za askofu efata kuzaa na mke wa mtu zilikutwa kwa usawa kila aina ya dini.

Mahakama yangu kwa karipio kali inazitaka pande zote kutopuuza elimu ya dini na dunia kwa viongozi wao hususan katika changamoto za majukumu ya dunia ya leo elimu kama psychological cancelling,philosophy,sociology,medicine ,interprenuar ship ni muhimu katika kujenga na kuongoza taasisi zetu zote za kidini hasa katika enzi hizi za mporomoko mkuu wa kimaadili wa ushoga,usagaji,ulaji rushwa wa wanasiasa,uvunjaji haki za binadamu etc unaotokana na ujinga,umaskini kwa kukosa ajira ba mitaji .
3.uchaguzi wa Askofu basil kuwa askofu mkuu wa ghafla
TAFAKURI
Mahakama yangu ilijiridhisha hali ovu ya hatua isiyo ya kikatiba wala kiungwana ya serikali ya awamu ya sita kujibu hoja kwa mabavu dhidi ya askofu gwajima juu ya mwenendo mchafu na doa la utekaji wa watanzania na hofu ya maisha yao kuwa kanisa lilipaswa na limefaa kumkaimisha Askofu mwingine kwa ustawi wake.
Aidha mahakama haikupata nyaraka za mchakato ila ilitafakuri pia kuwa kabisa Katoliki limesha sema na hata kusoma makanisani yote aliyotuhumu gwajima hata kuyasoma madhabahuni mwao kila jumapili ila mahakama yangu na wazee wake tulikubaliana serikali haizitendei kwa usawa dini kwani waislamu (wengi wasunni) wamekuwa na kauli za kinafiki kwa kuwa bakwata ni baraza chawa na waislamu huru kama sheikh ponda kupitia magumu kwa kuunga mkono hoja kinzani na serikali.


HATI YA HUKUMU
Mahakama kwa sauti moja imetupilia mbali tuhuma na mashitaka yote .Aidha inatoa onyo ikiambatana na karipio kali kwa wote wasio toa heshima kwa viongozi wa dini na kuhoji hoji mifumo yao ya ndani wakati mahakama imejiridhisha watuhumu na watuhumiwa wote wanamakasoro mazito na inatoa rai wote kukazana kujikosoa na kujiboresha .
Kwa maelezo haya hukumu ni kuwa BABA ASKOFU MKUU BASIL (Kama mahakama inavyomtambulisha na kumtambua rasmi) aheshimiwe na kuungwa mkono na jamii nzima kulisimamia na kulikuza kanisa lao.
NAKALA: WASHITAKI ,WASHITAKIWA NA MAKUNDI YOTE YA KIJAMII.
24/06/2025

HAKIMU: THE ONLY JF SENIOR MEMBER

(MUHURI RASIMI NA SAHIHI)
 
Aiseeeeeee... kweli ndio maana sitokaa nihame kanisa Takatifu Katoliki... ili uwe walau padre tu unahitaji degree mbili... haya makanisa ya kikanjanja yanaokota watu mtaani kesho wamekuwa maaskofu... dah...
Acha kulopoka kabla hujafanya utafiti au kuwahoji wanasomea hao sio wanakurupuka kama mawazo yako yanavyokupeleka wewe
 
Aiseeeeeee... kweli ndio maana sitokaa nihame kanisa Takatifu Katoliki... ili uwe walau padre tu unahitaji degree mbili... haya makanisa ya kikanjanja yanaokota watu mtaani kesho wamekuwa maaskofu...
Hivi yesu alikua na degree ngapi vile? na zehebu lako la kikoloni, unaweza ukawa darasa la saba na ukawa mtumishi wa Mungu mkubwa sana. Haya endelea ku support hao mapapa wenu wanaounga mkono ushoga.
 
Kiingereza ingekuwa intelligence huko ulaya na marekani kusingekuwa na homeless people kwa wingi.
Linganisha maisha ya kijijini kwenu.Ukijilinganisha na ulaya au USA ni ujingaujinga.Kama kiingereza ni upuuzi,hebu fanya ulinganisho kiswahili kimekusaidia nini!?
 
Aiseeeeeee... kweli ndio maana sitokaa nihame kanisa Takatifu Katoliki... ili uwe walau padre tu unahitaji degree mbili... haya makanisa ya kikanjanja yanaokota watu mtaani kesho wamekuwa maaskofu... dah...
Mwamba anakitabu mkuu.
Lakin kama kisa ni mziki vip kuhusu Musa, mtume Paulo, Petro na Rahabu wa yeriko, je wao walkuwa na status zip mtaani?
 
H
Gwajima alijirekodi akiwa anafanya mapenzi. Mbona husemi kuhusu hili?.. halafu anafufua watu kwa uwongo... na bado mnamuamini???? Mnasema ni mambo ya Rohoni?????
SIsemi kuwa wakatoliki wako perfect, but atleast wana taasisi imara, mashule, mahospitali, vyuo e.t.c... na hili pia linawezeshwa na kuwa na wasomi imara ndani ya taasisi. Makanisa ya kikanjanja wanamiliki vijikanisa vyao tu.. hata nursery school ni changamoto
Hatuwez unga mkono dhambi za mtu, lakin lile suala gwajima sio standard ya kujaji kanisa la ufufuo.

Hivi unadhani mapadree kuwa na skendo za ngono na watoto wadogo ndo standard ya kujaji RC?

Skendo ya Daudi kumbaka mke wa Uria mhiti je ndo ilkuwa standard ya kujaji uaminifu wake kwa Mungu?

Kama imani ya ufufuo na uzima ni ya kishetani basi ni kutokana na misingi yao, na sio tukio la gwajima.
 
Mapadre kibao wana degree 1 kibao na wengine form 6 wapo nisichoona tu wa form 4
Kuna jamaa tumesoma naye Olevel alipata div 4,lakin miaka miwili baadae alinipigia simu akanambia yuko kusomea upadree.
 
Back
Top Bottom