JWTZ: Baada ya siku 7 atakayepatikana amevaa, anatumia au anauza mavazi ya Jeshi atapatiwa adhabu kali

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,462

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limebainisha hatua hiyo inatokana na ongezeko la raia wanaotumia mavazo hayo wakikinzana na Sheria ya Ulinzi wa Taifa, Sheria ya Taifa na Sheria ya Kanuni ya Adhabu zinazokataza raia kuvaa au kutumia mavazi ya Kijeshi au yanyoendana na Jeshi.

Angalizo hilo pia limewagusa baadhi ya Taasisi ambazo zimekuwa zikiwashonea Wafanyakazi wake mavazi ya Kijeshi na wengine Wafanyabiashara wanauza mavazi hayo.

Amesema “Kwa unyenyekevu tunawaomba Wananchi wanaokiuka Sheria hizo kuacha kuvaa, kuyatumia au kuyauza mavazi hayo kuanzia leo (Agosti 24, 2023), baada ya siku 7 atakayepatikana atapatiwa adhabu kali, tumetoa muda huo kwa kuwa kuna raia ambao hawana uelewa hivyo tunawaelewesha kwa kuzingatia Utawala wa Sheria.”
 
Nasikia wengine wakikuona umevaa wanakuadabisha kisawasawa !
Wanakurusha kichurachura,wanakupiga mitama,wanakuvulisha hilo vazi unabaki uchi wa mnyama unaanza kutunyama Sasa..
Nitakufahamisha maana ya kutunyama!,kutunyama ni Ile uvulishwe nguo ya chini halafu malighafi zako zinabaki wazi!,hapo ukute Kuna hadhira inaona malighafi zako zinavyochezacheza mara uambiwe binuka,rukaruka,tambaa kama mnyoo... Huko ndio kutunyama..😅

Lkn mbona hawajatoa tamko juu ya dp world au wanasubiri tushindwane ndo waingie kati...??
 
Wanakurusha kichurachura,wanakupiga mitama,wanakuvulisha hilo vazi unabaki uchi wa mnyama unaanza kutunyama Sasa..
Nitakufahamisha maana ya kutunyama!,kutunyama ni Ile uvulishwe nguo ya chini halafu malighafi zako zinabaki wazi!,hapo ukute Kuna hadhira inaona malighafi zako zinavyochezacheza mara uambiwe binuka,rukaruka,tambaa kama mnyoo... Huko ndio kutunyama..😅

Lkn mbona hawajatoa tamko juu ya dp world au wanasubiri tushindwane ndo waingie kati...??
Aiseeehhh!! Hatari sana!
 
Aisee Kuna jamaa namhurumia sana, ana duka kubwa sana la nguo amejaza nguo zenye mabakabaka sijui ndo za jeshi au migambo ya china, yaani nyingi kama zote karibia duka zima
Wapi hapo mkuu niende nikajichukulie mali safi
 
Kama wanaongelea kufuata sheria, na wanasisitiza hivyo, basi Jeshi linapaswa kuwa mfano wa kufuata hizo sheria. Kwa kuanzia waanze kwa kupeleka malalamiko yao Polisi.

Polisi ndiyo wenye mamlaka ya kufuatilia hilo, waachane na jungle minds, zama zimebadilika hizi wanapaswa kujua majukumu yao yanapoishia. Tunalipenda na kuliheshimu Jeshi letu, so linapaswa kutambua misingi, sheria kanuni na mipaka ya majukumu yao.

Kwa Jeshi kupeleka malalamiko yao Polisi, siyo unyonge, bali itadhihirisha kuwa ni Jeshi linalojitambua, na linalotambua majukumu yake na ya wengine, na mipaka yake, zaidi itaibua hali ya Wananchi kufuata sheria na kwamba kumbe kufuata sheria siyo unyonge au utumwa bali ni ustaarabu na kujitambua.

Nguvu za hizi taasisi zinaundwa kutokana na sheria. Uhamiaji ilikua ni idara tu, sasa hivi baada ya muswada kupitishwa na kuwa sheria, Uhamiaji hivi sasa ni Jeshi kwa mujibu wa sheria iliyoliunda, na kuna sheria zinazoelekeza aina ya silaha wanazopaswa kutumia wawapo kazini, pia wanazoruhusiwa kuwa nazo popote hata majumbani.

Sheria ndiyo inaelekeza aina ya mafunzo gani yatolewe kwa Jeshi lipi, siyo kwa sababu labda Jeshi fulani ni noma kuliko lingine.

Sheria ikibadilishwa inaweza kupelekea JW inakua Polisi na Polisi wakawa JW. Tuachane na jungle minds, those days are long gone.
 
Back
Top Bottom