Nyambala, mikataba yote inatawaliwa na sheria ya mikataba, 'law of contract' hata ndoa ni mkataba. Ikishafungwa, hata kama ni illegal marriage, ni mahakama tuu ndio yenye mamlaka ya kutamka it is illegal, sio bunge, sio kamati ya bunge na sio mtu yoyote.
Baada ya kamati ya bunge kutambua kuwa richmond was illegal company, serikali ilipaswa kwenda mahakamani fasta na kuuvunja mkataba huku mahakama ikitangaza mkataba ule ni illegal. Kwa vile hakuna chochombo chochote kilichotangaza kuwa mkataba ule kuwa ni illegal,pamoja na illegality yake, umeendeleav kuwa legal mpaka leo tunapolipishwa!.
ICC pia imeponda hoja za usajili na legality ya richmond kwa sababu subject mater hapa sio nani ni nani, wala kampuni ipi imesajiliwa wapi, subject matter ni majereta ya kuzalisha umeme wa dharura, ni majereta ya ukweli na umeme wa ukweli. Msingi wa fidia ndipoo ulipolalia hapo!.
Suala hili limefanywa kisisas sana kulika kihalisia, serikali ilivunja mkataba wa kuilipa dowans capacity charge ya shilingi milioni 150 kwa siku, lakini tukakubali kuilipa IPTL shiling milioni 300 kwa siku na lita za mafuta laki 6 kwa siku!.