Fredrick Sanga.
Dogo Nassari anaropoka sana muwekeni chini mfahamisheni siasa za Tanzania zilivyo.
Kwa kweli naanza kupata wasiwasi kuhusu kijana mzalendo mwana Demokrasia kwa kuanza anavyofanya katika uwanja wa Siasa hapa Tanzania,... ''Kuhusu kwamba Sehemu ya Kaskazini Ijitenge, Iwe Jamuhuri yake''. Inawezekana ni wazo au ni mojawapo ya sera Lakini SI WAKATI HUU kwa sasa, Kwani Chama Tawala kinaweza kutumia kama njia ya Kukiharibu Chadema kwa Wananchi ambao tayari walishaanza kuweka matumaini na Kumshukuru MUNGU kuwa wamepata Chama cha kuwakomboa na cha Chama cha kupeleka Sauti zao Bungeni na kwenye Serikali.
NAJIULIZA,..
1. Inawezekana huyu kijana Alisha kuwa SETUP (Kuwekwa Pandikizi) toka yupo Chuoni kama wengine walivyofanywa?
2. Au Ameshaongwa hela Ili aje Aharibu chadema?
Sielewi lakini naamini MUNGU Atasimama kwa Raia zake,....!
Wewe ndio inaelekea unatumia makamasi katika kuchambua haya maswala, kwani wewe kwa upeo wako mfupi unafikiri siasa ya Tanzania ipo vipi yaani kwa mfano niki kuliza...?
Kweli huyu dogo anahitaji semina elekezi. Wewe tayari ni mbunge, maana yake wanachi wote katika jimbo lako wanawakilishwa na wewe. Ukisema wanaona Jimbo lako limesema. Sasa ukija na sababu za udogo wakati wewe ni mbunge naona kama hujui unachoongea. Nafikiri jifunze kujifunza kwanza, na kukaa kimya ni busara.Haya ni baadhi tu maneno machache ya Mbunge Joshua Nassary ktk mahojiano yake na polisi baada ya kujisalimisha.
Kasema hivi" Mimi sikuwa na nia mbaya juu ya kauli yangu bali ilikuwa ni kutoa hamasa ya mabadiliko kwa mikoa mingine iige Arusha,Mbeya,Musoma,Manyara, kwa mabadiliko walioonyesha pia Mimi ni mtu mdogo sana ktk nchi hii so sina mamlaka ya kumzuia Rais kuja Arusha wala sina uwezo wa kuigawanya nchi kwani kama ni kweli mm ninaweza kuigawanya nchi na kumzuia Rais basi HIYO ITAKUWA SIYO NCHI WALA HAIPASWI KUWEPO maana mi ni mtu mdogo sana"
Mdogo ki umri au ki akili,kama ni yote mawili,nawahurumia wananchi wa Arumeru.Leo baada ya mahojiano na polisi Arusha mjini zaidi ya masaa sita,Nassari akiongea na waandishi wa habari alisema "Mimi ni mdogo,kama ninauwezo wa kuigawa nchi hii basi nchi hii haikupaswa kuwepo"
Source;ITV News 2000hrs*
pandikizi ni mtu wa aina gani?
Wewe unayeshangaa hayo ndiye mchanga kwenye siasa kuwa uyaone, kuna nchi zimewahi kujitenga kwa sababu ya serikali kutojali matatizo ya sehemu moja. Halafu mkuu uko addicted sana na 'H'.Pro-Chadema JF wengi ni wachanga kwenye siasa hivi hunaweza kumpiga marufuku Rais wa Tanzania kwenda Arusha? Akili za kitoto kabisa hizi
I doubt the mental ability politically of Nassari on issues...
he talks cheaply & lightly ..... kuanzia sasa kumbe JJ Mnyika ni very matured, huyu kwa CDM wamchunge naona atachafua CDM kwa maneno....
Msemo wa mgema akisifiwa TEMBO hulitia maji, dalili zaonyesha CDM wamelewa misifa HIVYO wamefikia kuongea pasipo tafiti wala busara. Imefikia hatua viongozi kutoa matamko tofauti wakiwa majukwaani. Moja kwa moja UONGOZI WA KITIMU NDANI HIKI CHAMA HAUPO.
Imethibitika katika mkutano wa UNGA LTD, mbunge Nasari katoa tamko la UBAGUZI na kuthibitika hiki chama ni cha Kanda ya Kaskazini tu, wengine ni abiria.
Watanzania tutumie vichwa vyetu tufikiri kwa makini, CDM ni kwa ajili wa KANDA MOJA!!!!
Kuna matukio mengi yanayoonyesha CDM hawana utashi wa kuongoza TZ, kwani walianza kutoutaka muungano, na sasa wanataka kujitenga. tuwahurumie ndugu zetu toka kanda ya Ziwa, Kusini Nyanda za Juu waliovutwa na upepo wa msimu wa CDM pasipo kujua undani wa wamiliki wa CDM; ambao ni Mbowe & Mtei Co.
Najua wafuasi wa CDM toka kanda husika mtasema sana kwa vile nimewagundua ujanja unaotumia kutaka kutugawa watanzania kwa misingi ya ukanda.
Wewe unayeshangaa hayo ndiye mchanga kwenye siasa kuwa uyaone, kuna nchi zimewahi kujitenga kwa sababu ya serikali kutojali matatizo ya sehemu moja. Halafu mkuu uko addicted sana na 'H'.
Kumbe ni kweli Chadema mnataka kujitenga...
Pro-Chadema JF wengi ni wachanga kwenye siasa hivi hunaweza kumpiga marufuku Rais wa Tanzania kwenda Arusha? Akili za kitoto kabisa hizi
Ngoja niweke wazi kabisa; sina tatizo na kauli ya 'kujitenga'. Ni kauli ya kisiasa na imeshawahi kutolewa mara nyingi na watu wa Kigoma, watu wa Mtwara/Lindi, na hata watu wa Pemba.Binafsi hilo halinisumbui sana. Na mtu yeyote anajua aliitoa kauli hiyo kwa maana ya kuweka point ya utani ndio maana alisema "kama Sudan". Haina maana nzito ya kihivyo kwani na wengine wameshatoa kauli kama hizo.
Lakini huwezi kutoa kauli yenye kumtishia Rais na ukabakia hivihivi. Mtagundua kwamba kauli zenye kutishia maisha au usalama wa kiongozi yeyote wa umma huwa hatuzivumilii hapa kwa sababu moja kubwa - siyo watu wote wana akili zilizotulia na huwezi kujua nani akisikia anasukumwa vipi.
Nassari ni kiongozi maarufu sana sasa hivi na ameshinda kwa kishindo kikubwa sana. Kule Arusha ana mvuto mkubwa sana na ni mvuto wa watu kukesha na kumlinda hadi dakika ya mwisho. Chuki dhidi ya CCM ni chuki ya kweli (real hate) na siyo watu wote wanaweza kudumu kwenye chuki hiyo na wakiacha kwenye mambo ya kisiasa tu. Sasa, mbunge maarufu, tena kijana anaposimama na kusema anaweza kumpiga mkwara rais asikanyage Arusha siyo jambo dogo kwa sababu siyo wasikilizaji wake wote wanamuona 'mdogo hivyo'. Nassari ana ushawishi na anamvuto.
Labda watu wengi hawajui historia. Martin Luther King hakuwa na cheo chochote cha kisiasa zaidi ya kuwa mhamasishi mwanaharakati. Lakini mauaji yake yalisababisha miji ya Wamarekani kuingia katika machafuko makali sana. Ni kwa sababu watu walijua ameuawa na mikono ya watu wenye nguvu. Hata Nassari pamoja na "udogo" wake wote hakuna mtu Arusha atapenda anatendewa vibaya au kuonewa na wapo watu wanaoweza kufanya lolote kwa ajili ya utii wao. Nadhani watu wengi wameshasahu kuwa mauaji ya Arusha ya 2011 kwa kiasi kikubwa yalisababishwa na polisi kutumia nguvu dhidi ya watu ambao waliona wanaonewa.
Sasa mbunge anaposimama na kutoa kauli ambayo vyombo vya usalama vinaiona ni ya vitisho dhidi ya Rais ni kutokuwa makini kudhania tu ni jambo dogo. Alichotakiwa kusema Nassari ni hiyo kauli yake ya kwanza tu kuwa hakumaanisha ubaya wowote na kama mtu yeyote amekwazwa anaomba radhi. Lakini siyo kusema kuwa ati yeye ni mtu mdogo na asingeweza kugawa nchi; well hilil ni zaidi ya kugawa nchi. Hivi akisema kuwa Rais asikanyage na Kikwete akaamua kukanyaga na mwehu mmoja akaamua kufanya kitu kibaya kwa msafara wa rais watu watamlaumu mwehu kwa vile ni mwehu siyo? Lakini, yule mwehu ukimuuliza atasema "rais wetu" alitoa amri Kikwete asikanyage Arusha na akakanyaga!
Hii ni sababu moja ambayo inanifanya miye nisiwe shabiki sana ya hoja ya 'uongozi bora ni ujana' kwani tayari tumeshaona mengi yasiyo ya lazima ambayo vijana wameyafanya na kuthibitisha ukosefu mkubwa wa hekima na utulivu unaotokana na busara. Siyo lazima useme kila kinachoingia kichwani hata kama unaamini ni sahiihi. Kuna vingine unaweza kuvisema ila kwa namna tofauti. Hili huwezi kufundishwa shuleni au chuoni!
Ni matumaini yangu Polisi hawatoliendeleza hili na Nassari atakuwa amegundua (sidhani kwa sababu arrogance ya madaraka nayo nimbaya sana!) makosa yake. Sitaki ajisikie ameonewa bali ajue genuinely hakupaswa kutoa kauli hiyo na ni unfortunate. Kwa mfano Lema angekuwa makini na kauli zake wala asingevuliwa Ubunge! HEKIMA, HEKIMA, HEKIMA!!
Acha kujikomba kwa Mzee Mwanakiji amechemka sana. Sidhani kama ni yeye ama kaibiwa password.
Siungi na sikubaliani na kauli ya Dogo Janja, lakini pia sikubaliani na pumba alizoongea MMK. Suala la msingi ni kwamba ile kauli haikuwa kauli ya chama, ndiyo maana ilikanushwa pale pale uwanjani na Mbowe, na hili Mzee Mwanakijiji alijua mapema siku hiyo. Jambo alilotakiwa kulijadili Mzee Mwanakijiji kama nguli humu Jf ilitakiwa iwe ni nini kilisababisha Dogo Janja afikie hatua ya kutamka yale manen, nini kiliwaudhi au kilimuudhi. Hii ndiyo ilitakiwa iwe pakuanzia.
Tusiwe kama wapumbavu wanaopiga vita uvutaji wa sigara wakati huo huo wanasimamia uzalishaji wa sigara.
Hii kauli ya Kaskazini kujitenga mnaona kama kauli mbaya ya kibaguzi kuliko kauli ya uvccm mkoa wa pwani ambayo hadi leo hakuna kiongozi wa ccm aliyethubutu kanusha kwa kumwogopa Riz1! Shame on you guys!
Ni afadhali ya CHADEMA waliothubutu kukanusha kauli ya Dogo Janja pale pale.
Amesema jambo ambalo kwa haraka linaonekana lina mantiki lakini linapuuzia uzito wa alichokisema. Kama ni mtu mdogo hivyo aligombea ubunge wa nini? Kama anakosa hekima ya kupima madhara ya maneno yake - watu wanaweza kuumia kwa kauli moja tu ya mtu mwenye ushawishi - kwa sababu yeye ni 'mtu mdogo' ananitisha. Yeye anaweza kuwa na umri mdogo lakini nguvu ya ushawishi wake inashinda baruti na siyo watu wote wanaomsikiiliza wanamchukulia kuwa ni mtu 'mdogo'. grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr