Kwa hiyo TL Marandu hoja yako hapa ni kauli ya JPM ya ;
"...Nassari usoni ni CHADEMA lakini moyoni ni CCM....", siyo?
Aaah mzee wangu, hii mbona ni kauli ya kawaida ya kisiasa tu??
Sawa tu na upinzani unavyomrushia makombora yeye mwenyewe Pombe Magufuli kwamba, usoni ni CCM lakini moyoni ni MPINZANI halisi kwa sababu ndiyo maana anatekeleza hata yale yaliyolalamikiwa na upinzani miaka na miaka kwa mtindo wa kutumbua majipu!
Na kwa hakika sioni sababu ya Joshua Nassari kama alikuwa na nafasi hiyo kujumuika ktk ziara ya Rais na especially kama baadhi ya mambo aliyokuwa anashughulikia Rais yalikuwa yanahusu jimbo lake!
Jana nilimwona Waziri wa Ardhi Bwana William Lukuvi kupitia TV akiwa jimboni kwa Halima Mdee (jimbo la Kawe) kutatua mgogoro wa ardhi wa eneo la Chasimba dhidi ya mwekezaji mmoja
Ofcoz Mbunge mwenyewe wa jimbo lilipo eneo la mgogoro hakuwepo, lakini kwa sababu ya ishu yenyewe ilivyo nadhani chama au Halima mwenyewe alimuomba mbunge wa jimbo la Ubungo Bw Saed Kubenea kumwakilisha na mambo yalikwenda vizuri tu na tunaambiwa mgogoro umeisha.
I think hii ishu si kubwa kwa kiwango hiki na after all wote tunajua tatizo la Rais wetu Bw Pombe Magufuli kwamba, kupitia kauli zake anaweza kuzua tafrani wakati wowote mahali popote juu ya jambo lolote na kwa mtu yeyote hata kama kiuhalisia ndivyo sivyo!!
Wewe si unakumbuka kauli yake juu ya Crisis ya Zanzibar alipokuwa anaongea na wazee wa Dsm, kwamba hataongea chochote kuhusu mgogoro huo kwa sbb atakuwa anaingilia maamuzi ya tume - ZEC!? Ulimuamini?
Si kwamba wengi tulimpinga waziwazi humu kwa hoja, kwamba ana wajibu wa kuingilia na kuutatua mgogoro huo kwa sababu yy ndiye kinara wa JMT na Zenj ikiwa sehemu ya JMT?....Leo unamshangaa kweli huyu mheshimiwa Rais!!?
Mwelewe Magufuli na ukishamwelewa hutapata taabu. Zaidi sana naye anatakiwa atafutiwe kijembe cha kisiasa tu, apigwe nacho na mchezo unaishia hapo.
Binafsi, sioni tatizo la mbunge wa Arumeru Mashariki, ndg J. Nassari ktk hili jambo. So let it go, hakuna tatizo lolote!.