Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, Mh. Mwankenja ameuawa kwa kupigwa risasi usiku wa leo majira ya Nne na dk 10 nyumbani kwake Kiwira. Taarifa za awali zinaonyesha kuwa marehemu Mwankenja alipigwa risasi akiwa ndani ya gari lake mara baada ya kuwasili nyumbani kwake.
Wauaji walitoweka mara baada ya kukamilisha mauaji yao na kabla ya watu kukusanyika. Hadi sasa sababu za mauaji hayo hazijafahamika. Hata hivyo baadhi ya viongozi waliofika nyumbani kwa marehemu usiku huu wanahofu mauaji hayo kuhusiana na masuala ya kisiasa.
Marehemu John Mwankenja
Viongozi na Wanasiasa wengine waliowahi kupigwa risasi
- Utata kifo cha hayati Abeid Karume
- DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali
- Simulizi: Kisa na Mkasa wa Mauaji ya Jenerali Imran Kombe (Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa-TISS)
- Kifo chenye utata cha Waziri Nicas Mahinda
- Wakili mtetezi wa ICTR Prof. Jwani Mwaikusa auawa Tanzania
- TANZIA - Waziri Salome Mbatia afariki dunia, maswali yaibuka!
- Iringa: Mwandishi Mwangosi auawa katika vurugu kati ya Polisi na CHADEMA
- Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka ashambuliwa kwa risasi na Watu wasiojulikana
- Askari polisi aliyepigwa risasi na majambazi Tanga afariki