Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 5,122
- 17,406
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, John Heche amezungumzia kurejea kwa Halima Mdee ndani ya chama hicho wakati wa mahojiano kupitia Wasafi FM;
"Kwanza niseme Halima ni rafiki yangu, na mimi nampenda na anajua. Tumekuwa naye kwenye chama... ni mtu nampenda, anajua na chama chetu kinampenda."
"Halima ni mtu mwerevu, ni mtu ambaye kwa kweli ana mchango mkubwa kwa chama chetu, huwezi kupuuza hilo, huwezi kulikataa."
Kuhusu utaratibu wa kurejea kwenye chama amesema; "Anajua taratibu za chama chetu. Kama alivyofuata Anatropia [Theonest], Anatropia aliandika barua, akafuata 'process' zote, ikaja kwenye kikao..."
"Hivyo hivyo Anthony Komu... alikuwa Mbunge, akafukuzwa na yeye alifuata 'procedure', wote wamerudi ndani ya chama."
"Mirango iko wazi, hiki ni chama cha siasa... Kama anataka kurudi kwenye chama, 'procedure' zipo, 'process' zipo, arudi kwa kupitia utaratibu, atapokelewa kwenye chama."
Kuhusu Wanachama wengine wa CHADEMA walioondoka, Heche amesema; "Na hata wale wengine waliokimbia kule kwenda kwenye kile chama kile kingine... wengi umewasikia wanarudi wenyewe wanasema 'kumbe tulikengeuka'."
"Kwanza niseme Halima ni rafiki yangu, na mimi nampenda na anajua. Tumekuwa naye kwenye chama... ni mtu nampenda, anajua na chama chetu kinampenda."
"Halima ni mtu mwerevu, ni mtu ambaye kwa kweli ana mchango mkubwa kwa chama chetu, huwezi kupuuza hilo, huwezi kulikataa."
Kuhusu utaratibu wa kurejea kwenye chama amesema; "Anajua taratibu za chama chetu. Kama alivyofuata Anatropia [Theonest], Anatropia aliandika barua, akafuata 'process' zote, ikaja kwenye kikao..."
"Hivyo hivyo Anthony Komu... alikuwa Mbunge, akafukuzwa na yeye alifuata 'procedure', wote wamerudi ndani ya chama."
"Mirango iko wazi, hiki ni chama cha siasa... Kama anataka kurudi kwenye chama, 'procedure' zipo, 'process' zipo, arudi kwa kupitia utaratibu, atapokelewa kwenye chama."
Kuhusu Wanachama wengine wa CHADEMA walioondoka, Heche amesema; "Na hata wale wengine waliokimbia kule kwenda kwenye kile chama kile kingine... wengi umewasikia wanarudi wenyewe wanasema 'kumbe tulikengeuka'."