Job Ndugai ni Shujaa wa Historia-Anatuonesha Matobo na Udhaifu wa Samia Suluhu

ubongokid

JF-Expert Member
Apr 30, 2017
2,030
3,908
Ndugu zangu;

Kila nchi inakopa,na kila mkopo lazima utumike kikamilifu.Hata hivyo hii mikopo ambayo tunaaminishwa kwamba imetumika vizuri ni changa la macho.

IKO hivi.Idadi ya watu Tanzania ni Chini ya Milioni 60.Idadi ya shule ni chini ya elfu 20.Trilioni moja ni sawa na Bilioni 1000.Kamata Trilioni 1.3 ya covid imepelekwa kujenga madarasa,na TOZO ya uzalendo nayo imeenda kujenga madarasa basi inamaana yamejengwa madarasa ya thamani ya milioni 100 kwa kila moja ambayo ni sawa na madarasa 10,000.Kama kila darasa linakaa wanafunzi 40 inamaana wanafunzi laki nne na zaidi wamejengewa madarasa mapya.

Katika hali ya kawaida unaweza fikiri kwamba JOB NDUGAI aliteleza ulimi aliposema kwamba TULIPITISHA TOZO ili TUPUNGUZE KUKOPA lakini MBONA bado TUNAKOPA?Ni swali la msingi sana.Kama serikali imeweka TOZO zenye majina tofauti na kila siku wanabuni majina mapya ya TOZO na kodi .JE inaleta PICHA gani iwapo tunaendelea kupewa mikopo yenye majina TOFAUTI?

Je, serikali inafuja PESA zetu? TRA wanasema wamekusanya trilioni 11 kwenye miezi kama 6 iliyopita na wakati huo huo tumechukua mikopo ambayo ni sawa na kiasi hicho cha makusanyo ingawa miradi iliyofanywa bado haijafikia kiwango hicho cha cha makusanyo.JE nani muongo?

Binafsi naamini kabisa NDUGAI alisema ukweli wake na alichagua kuondoka kishujaa pamoja na kwamba alikuwa sehemu ya ufedhuli na unyonyaji.Huyu Ndugai alikaa India kwa Muda mrefu akitumia pesa za walipakodi kula RAHA ukiona mpaka amefikia hatua ya kufunguka UJUE kuna JAMBO

ANYHOW.Nfasi ya kazi ipo WAZI niwakumbushe tu wale vijana ambao wanao mpango wa kuwa SUPIKA kwamba nafasi iko wazi na mtu yeyote anaweza kugombea mradi tu kuwe na chama cha siasa kinachokudhamini..So muanze kazi mapema.
 
Ndugai hoja yake ni nzuri sn tatizo la Ndugai ni ukatili wake na maovu
upo sahihi maisha yake ya uspika ya miaka mitano iliyopita ya unable,vitisho nk...kwahiyo sio wa kuonewa huruma kabisa huyu
 
Hoja yake nzuri baada ya mgongano wa kimaslahi na Samia?

Majani yanaweza yakawa yamestawi vizuri lakini kumbe chini mizizi imeoza

Baada ya muda mchache na hayo majani pia yatanyauka.

Ndugai anaangalia tumbo lake sio tumbo lako wewe.

Haumizwi chochote na hyo mikopo Bali kuna kuna kitu nje ya hyo mikopo hapo alikuwa anatafuta sababu.

Hauwezi kumwambia amir jeshi mkuu kuwa atauzwa hyo NI dharau
Ndugai hoja yake ni nzuri sn tatizo la Ndugai ni ukatili wake na maovu
 
Jamaa alikuwa na kiburi hata pale kijijini kwao alijiona Mfalme , mnapoambiwa mkipata uongozi kuweni waadilifu basi mjue Quran sio maneno ya kubangaiza ,jitahidi uwezavyo kufanya wema na uadilifu ili upate mwisho mwema ,japo kuna changamoto za hapa na pale lakini mtu akiwa mwadilifu basi ataonekana tu.

Ndigai hakuwa mwadilifu alikuwa mtu wa kujipitisha kivitendo na kutaka misifa ,tumeona aliyoropoka kwa pro Assad,tumeona alivyokandia upingwaji wa wabunge wa chadema kwa jeuri kabisa ,aliwasimanga sana Chadema na hata kuwatoa walio kuwa kifungozi na kuwaapisha kuwa wabunge,na hata baada ya covid kufukuzwa ndani ya Chadema ,Ndugai alionyesha hakuna kama yeye,leo hana wa kumtetea ispokuwa wale wa aina yake.
 
Kumbuka pia huku vijijini watu tunatozwa michango ya maendeleo ya kufa mtu nchi hii ni hatari
 
Hoja yake nzuri baada ya mgongano wa kimaslahi na Samia?
Majani yanaweza yakawa yamestawi vizuri lakini kumbe chini mizizi imeoza
Baada ya muda mchache na hayo majani pia yatanyauka.
Ndugai anaangalia tumbo lake sio tumbo lako wewe.
Haumizwi chochote na hyo mikopo Bali kuna kuna kitu nje ya hyo mikopo hapo alikuwa anatafuta sababu.
Hauwezi kumwambia amir jeshi mkuu kuwa atauzwa hyo NI dharau
Huyu bibi ako naye ana hati miliki na Magogoni hataki mtu mwingine aguse maanake hayupo hapo kutumikia wananchi mbali maslahi yake binafsi
 
Ni kweli Ila ndugai Ana mabaya yake.mengi tu.
Mwanzo aliona nini leo kaona nini?
ebu tukumbuke miaka 5 nyuma ndugai alikuwaje kwanini iwe Leo ndo kaja kuyaona hayo aliyoyaona?
Anamchukia Samia?
Kwanini huu mnaouita utetezi wa raia aje kuufanya kipindi Cha Samia?
Unajua watu wangapi wameteseka kipindi Cha magufuli na yeye akiwa spika wa bunge?
Aliongea nini?
yaani mateso ya watu na vifo vya watu havikuwa na umuhimu Ila mikopo ya Samia ndo Ina umuhimu?
TUACHE UNAFIKI SIMUONEI HURUMA NDUGAI HUYO ATAPANDA ALICHOVUNA
Huyu bibi ako naye ana hati miliki na Magogoni hataki mtu mwingine aguse maanake hayupo hapo kutumikia wananchi mbali maslahi yake binafsi
 
Samia ana roho mbaya sana kafunga vituo vya mafuta vya Ndugai mpwapwa na kongwa.
 
Hoja yake Ni nzuri shida tabia zake Ni mbaya. Ametuumiza Sana CHADEMA.
 
Ni kweli Ila ndugai Ana mabaya yake.mengi tu.
Mwanzo aliona nini leo kaona nini?
ebu tukumbuke miaka 5 nyuma ndugai alikuwaje kwanini iwe Leo ndo kaja kuyaona hayo aliyoyaona?
Anamchukia Samia?
Kwanini huu mnaouita utetezi wa raia aje kuufanya kipindi Cha Samia?
Unajua watu wangapi wameteseka kipindi Cha magufuli na yeye akiwa spika wa bunge?
Aliongea nini?
yaani mateso ya watu na vifo vya watu havikuwa na umuhimu Ila mikopo ya Samia ndo Ina umuhimu?
TUACHE UNAFIKI SIMUONEI HURUMA NDUGAI HUYO ATAPANDA ALICHOVUNA
Nakubalina na wewe Ndugai ni mtu muovu sn lakini huyu bibi ni zaidi ya tatizo kwenye kiti chake utaniambia anawaza 2025 na sikingine
 
Tatizo sio mkopo. Tatizo sio Jobu. Tatizo ni uchaguzi 2025. Mama amenusa wanaotaka kumzibia riziki. Hofu ya uchaguzi imetanda maoema sana.
 
Jamaa alikuwa na kiburi hata pale kijijini kwao alijiona Mfalme , mnapoambiwa mkipata uongozi kuweni waadilifu basi mjue Quran sio maneno ya kubangaiza ,jitahidi uwezavyo kufanya wema na uadilifu ili upate mwisho mwema ,japo kuna changamoto za hapa na pale lakini mtu akiwa mwadilifu basi ataonekana tu,
Ndigai hakuwa mwadilifu alikuwa mtu wa kujipitisha kivitendo na kutaka misifa ,tumeona aliyoropoka kwa pro Assad,tumeona alivyokandia upingwaji wa wabunge wa chadema kwa jeuri kabisa ,aliwasimanga sana Chadema na hata kuwatoa walio kuwa kifungozi na kuwaapisha kuwa wabunge,na hata baada ya covid kufukuzwa ndani ya Chadema ,Ndugai alionyesha hakuna kama yeye,leo hana wa kumtetea ispokuwa wale wa aina yake.
Upo sawa mkuu,hakuna kupepesa waambie ukweli.
 
Hoja yake ya mikopo aliipunguza makali pale alipoomba msamaha, yeye mwenyewe anasema hakukusudia kueleweka hivyo. Hapo ndipo alipoiua hoja ya mikopo
 
Back
Top Bottom