JK apanda chati DRC!!!

JK apanda chati DRC!!!

viongozi wachache sana wenye uvumilivu kama jk hana haraka lakini kazi inafanyika.

Kweli kabisa kaka/dada. Embu fikiria kama rais wetu angekuwa ameshachoka sasa na kuamua liwalo na liwe kama alivyochoka waziri mkuu. Watu wangekuwa wanapigwa tuu.
 
Hata mimi napenda alichofanya JK lakini asisahau kuchukuwa madini na mbao huko kulipia gharama tunazoingia wakati wa kutekeleza jukumu letu la kuwafanya Wakongo nao waishi na kuifurahia nchi yao kama binadamu wengine.

Mapato hayo yataingia vipi TRA?
Au ndio kuneemesha Ufalme wake kwa mgogo wa Wanajeshi wakiTanzania.
 
Dhambi kubwa sana inayowakabili wacongoman ni uoga!

I can't image nchi kubwa na yenye nguvu kazi kubwa ya kutosha kabisa kama DCR kunyanyaswa (tena kijinsia) na ka nchi kama rwanda!

Enzi za kabila chini ya mwamvuli wa SADC tuliwasaidia ku recruit wanajeshi vijana wa kicongo wa kutosha kabisa kuilinda nchi yao, cha ajabu kwa uoga wao wakawa wa kwanza kuikimbia vita au kujiunga na upande wa maadui, huku nchi yao ikitegemea utetezi wa majeshi ya SADC kutoka Angola, Zimbabwe, Botswana na sasa Tanzania kwa mwamvuli wa UN

Hapana mkuu. Jaribu kufikiri kwa kina kidogo. Tatizo la wacongo siyo woga. Congo ni nchi kubwa sana kieneo kiasi kwamba Congo ya mashariki na ya kule magharibi haziunganishwi na barabara, lugha wala utamaduni. Kama ambavyo muhaya na mngoni wanaunganishwa na vitu nilivyovitaja hapo juu, Congo jambo hilo halipo. (Hiyo ni moja tuu ya madhara ya mipaka yetu kuchorwa Berlin). Kwa mfano, mtu kama Dr. Remmy (RIP). Ingawa yeye alikuwa m-Congo, lakini alijiona anafanana zaidi kitamaduni na Tanzania kuliko Congo. Na hiyo ndiyo hali halisi ya Congo ya mashariki, kuanzia Uvira/Goma juu kule mpaka Lubumbashi na Kisangani huku chini. Na ndiyo maana ni vigumu sana kuwa-organise wa-Congo kuwa na jeshi imara. Sasa watu wenye tamaa kama Kagame wanalijua hilo na wanajinufaisha kwa kuangamiza wengine.
 
Jk lazima asifiwe coz ni mnafiki,siku zote mataifa ya nje husifia mnafiki
 
Jk lazima asifiwe coz ni mnafiki,siku zote mataifa ya nje husifia mnafiki
. Wewe una lako na J.K. Muache Rais wetu, anachofanya ni jambo jema sana na Mungu anaendelea kmbariki!
 
*Wananchi wamuona mkombozi,shujaa wao!

*Wabunge wa DRC kufunga safari hadi ikulu ya Magogoni kumshukuru!

*Kumuomba kichapo cha Nduli Amini kirejewe kwa Kagame!

*M23 waishi kama Ngedere kwa matunda porini!

*Ni baada ya kichapo cha masaa2 tu toka JWTZ!

*Wakimbia waacha silaha,vyakula!

*Saa 48 walizopewa kuweka silaha chini zazidi kuyoyoma!

nasubiria hii seies kuiona aisee..
 
DRC waende mbali zaidi waruhusu JK awe Rais wao kama hawajajuutaa kuzaliwa.
 
[h=5]*Wananchi wamuona mkombozi,shujaa wao!

*Wabunge wa DRC kufunga safari hadi ikulu ya Magogoni kumshukuru!

*Kumuomba kichapo cha Nduli Amini kirejewe kwa Kagame!

*M23 waishi kama Ngedere kwa matunda porini!

*Ni baada ya kichapo cha masaa2 tu toka JWTZ!

*Wakimbia waacha silaha,vyakula!

*Saa 48 walizopewa kuweka silaha chini zazidi kuyoyoma![/h]

Usimpe mtu sifa kabla ya mission kukamilika maana adui anaweza akajipanga upya na kusababisha madhala makubwa kwa unayempa sifa. Cha msingi ni kusubili huo muda aliopewa adui kuisha n if an enemy [M 23] is not going to accept altimatum kitakachofuata hatujui. Tumelianzisha TPDF na tusubili matokeo. I will be proud of my country if TPDF is going to accomplish the mission. Na hili litakuwa somo kwa P. Kagame & J. Banda
 
. Wewe una lako na J.K. Muache Rais wetu, anachofanya ni jambo jema sana na Mungu anaendelea kmbariki!

Yakuza unanipotezea attention kwenye mada kwa Avatar yako jamani.
Hata hivyo, Raisi wetu yupo sahihi kabisa katika hili.
 
Kuna mtu alileta mada jamvini akasema Congo D.R imesaini mkataba na Kenya kutumia Bandari ya Mombasa na mizigo itakuwa inapitia bandari ya nchi kavu itakayokuwa RWANDA!Yaani mpaka leo siamini kama kuna ukweli katika hili, yaani Joseph Kabila uhusiano wake ulivyo na KAGAME kwasasa aruhusu hilo??

Turudi kwenye mada, nawapongeza sana MONUSCO na Jeshi la Congo D.R kwa ushindi wanaoelekea kuupata dhidi ya madhalimu wa M23.
 
Back
Top Bottom