JK apanda chati DRC!!!

JK apanda chati DRC!!!

Magamba kwa kuanzisha majiviwanda ya uongo tu hamjambo mbona JWTZ wapo busy kupiga na kubaka watu huko Mtwara? au M23 ndo wapo mtwara siku hizi?

Acha Ufala wewe, Usichomekee utumbo kwenye mambo ya uzalendo. Ungetafuta maala pake lakini sio kwenye mtililiko huu. Usiwakatishe tamaa JWTZ, kiazi wewe.
 
*Wananchi wamuona mkombozi,shujaa wao!

*Wabunge wa DRC kufunga safari hadi ikulu ya Magogoni kumshukuru!

*Kumuomba kichapo cha Nduli Amini kirejewe kwa Kagame!

*M23 waishi kama Ngedere kwa matunda porini!

*Ni baada ya kichapo cha masaa2 tu toka JWTZ!

*Wakimbia waacha silaha,vyakula!

*Saa 48 walizopewa kuweka silaha chini zazidi kuyoyoma!

*Kumuomba kichapo cha Nduli Amini kirejewe kwa Kagame! - Wapi? Mkuu wake wa Majeshi ametokea JKT ni lini na wapi atakaa na mikakati ya KIVITA?

VITA SIO MCHEZO; Tulichoma MOTO ile HISTORIA yote tuliyokuwa nayo ya waliopitia JKT; Sasa hatujui ni JESHI gani tunalo, lipi IMARA na lililofundishwa...

Wanajeshi wetu wengi Wako URAIANI...
 
DRC ina watu millioni 70, ina madini, ina misitu... lakini inasumbuliwa na Rwanda yenye watu milioni 12? Hata ukijumlisha na milioni 34 wa Uganda, kweli ndio wa kuinyanyasa ncho kubwa namna hiyo?!!!
Kweli waafrica tumelaaniwa... si bure...

Miafrika Ndivyo Tulivyo - Nyani Ngabu
 
Last edited by a moderator:
Mkuu huyo ni CHADEMA at work achana naye, hata hivyo lazima liwaumize sana wanaposikia JK anasifiwa na mataifa ya nje kwa vile walitegemea wakapige propaganda huko nje kuwa Serikali ya JK sasa wanaona mipango yao inagonga mwamba.

Acha Umbwege wewe, aliye kwambia Chadema wote wanapinga kila kitu ni Kinana au Nape?.
MIMI MBONA SIWAPENDI CCM, LAKINI NAWAPENDA JWTZ.
 
habari ziwafikie dr slaa, kagame, mnyika, lema, mama banda wa malawi na jamaa wote wanaohusika popote pale walipo.

Usiwagawe watanzania, tunaitaji kuungana kwa hili. Si haki hata kidogo Kagame kumfananisha hata na panya wa Tanzania SEMBUSE Viongozi wazalendo wa CDM. wewe itakuwa ni mtusi, unajipenyeza kutugawa. MSHINDWE !.
 
Mkuu fuatilia vizuri vyombo vya habari utaona Wakongo wanavyo support kupigwa na kuuwawa kwa M23, hata kupitia ITV karibu kila siku wanaripoti issue za kongo na wamepeleka mwakilishi wao huko kwenye mapigano. Kwa logic ndogo kabisa Furaha hiyo ya Wakongo ni lazima waishukuru serikali ya Tanzania.
RAI wamepata wapi hizo habari za kupanda chati wakati vyombo vya habari DRC havijawahi kuandika au kusema?
 
Ni kweli...tuna issue zetu nyumbani...hizi ni zetu wenyewe na tutamalizana sisi wenyewe kwa njia zetu salama kabisa pamoja na malumbano makali mijadala mizito lakini Mungu ni mwaminifu tutafika tuu... Sasa inapokuja issue za PK huyu ni hatari hafai katika eneo hili la maziwa makuu, kwanza anapandikiza watu wake katika kila taifa kwa mujibu wa askari wake waliolazimishwa kwenda kujiunga na M23 halafu wakatoroka....kwahiyo hata sasa upo uwezekano mkubwa tuu kuwa ndani ya vyombo vyetu vya usalama wapo watu wake.....ni lazima kama Taifa kuwa naye makini sana huyu..na ndio maana anakiburi na jeuri..na kujiamini kwingi sana...lakini sasa imetosha tuangalie asijetuletea balaa la vita visivyokuwa na miguu wala kichwa....Vita ni Gharama...sio gharama ya mali tu hata maisha....kumbuka toka 1979 shilingi 5 yetu ikiwa sawa na dola moja ya Marekani (1$) ...Amini amesababisha mpaka leo no recovery miezi 18 imekuwa miaka 34 vita sio mchezo...Sasa huyu sio wakutumia nguvu...akili, hekima na maarifa yatumike
 
Kama namuona Kagame anavyotrot kuzunguka ofisi nzima akitukana! anatamani amkabe JK! ha ha ha ha Kagame kwishneyyyyyyyy
 
Kwani jk wenu kaenda kupigana au mnalopoka lopoka????
Wakusifiwa ni wanajeshi wanaopigana siyo jk+mama salme magogoni sliping'
 
*wananchi wamuona mkombozi,shujaa wao!

*wabunge wa drc kufunga safari hadi ikulu ya magogoni kumshukuru!

*kumuomba kichapo cha nduli amini kirejewe kwa kagame!

*m23 waishi kama ngedere kwa matunda porini!

*ni baada ya kichapo cha masaa2 tu toka jwtz!

*wakimbia waacha silaha,vyakula!

*saa 48 walizopewa kuweka silaha chini zazidi kuyoyoma!



source please!
 
hivi JK mtamsifia hadi lini, harafu mnatumia nguvu sana. Sifa huja zenyewe, angalia sifa alizonazo filikunjombe kwani alitafuta mpiga debe??? Juzi wakazi wa songea walikuwa wakimshangilia kila neno moja analosema tofauti kabisa na waziri mkuu. Aliposimama filikunjombe wananchi walisimama na kuanza kushangilia kama mkombozi kasimama.

Sasa nyie mnafanya kazi on empty.

:bored: Wacha wivu wewe! Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Kuna siku utakuja kumbuka Rais wako kafanya nini. Huko misri kuna wanaokumbuka sasa Hussein Mbarak alifanya nini na hata huko Libya kuna wanaokumbuka Gaddaf aliwafanyia nini. Kuna ule msemo wa Nabii hasujudiwi nyumbani. Ndio maana wewe humuoni JK wamaana lakini wananchi wa DRC wanaona mtu muhimu kwao. JK ana miaka saba tu katika kuiongoza nchi na si kweli hali ya Tanzania kama ni mbaya imetokea katika muda huo pekee. Kila Rais amefanya mazuri na mabaya yake. Kama ni mabadiliko lia na mabadiliko lakini ujue wazi katika hayo mabadiliko kutakuja mazuri na mabaya yake. Usidanganyike kuna hata siku moja katika ulimwengu huu utaishi kwa maziwa na asali kama inavyohubiriwa. Matatizo yatakuwepo hadi siku ya kuchimbiwa kaburini. Hata hao wasiokua na mengi na wanakula kuku na bata wana machache yao matatizo. Si umewasikia wa EPA? Wengine wanayo mabilioni hadi leo lakini wapo kila kukicha mahakamani. Unadhani kweli wana raha?
 
ni kweli...tuna issue zetu nyumbani...hizi ni zetu wenyewe na tutamalizana sisi wenyewe kwa njia zetu salama kabisa pamoja na malumbano makali mijadala mizito lakini mungu ni mwaminifu tutafika tuu... Sasa inapokuja issue za pk huyu ni hatari hafai katika eneo hili la maziwa makuu, kwanza anapandikiza watu wake katika kila taifa kwa mujibu wa askari wake waliolazimishwa kwenda kujiunga na m23 halafu wakatoroka....kwahiyo hata sasa upo uwezekano mkubwa tuu kuwa ndani ya vyombo vyetu vya usalama wapo watu wake.....ni lazima kama taifa kuwa naye makini sana huyu..na ndio maana anakiburi na jeuri..na kujiamini kwingi sana...lakini sasa imetosha tuangalie asijetuletea balaa la vita visivyokuwa na miguu wala kichwa....vita ni gharama...sio gharama ya mali tu hata maisha....kumbuka toka 1979 shilingi 5 yetu ikiwa sawa na dola moja ya marekani (1$) ...amini amesababisha mpaka leo no recovery miezi 18 imekuwa miaka 34 vita sio mchezo...sasa huyu sio wakutumia nguvu...akili, hekima na maarifa yatumike

heshima kwako.
 
Namuunga mkono J.M. Kikwete (Tanzania) kwa kuendeleza Amani ukanda huu wa maziwa makuu. Hii ndiyo sifa kuu ya nchi yetu iliyojengwa/pikwa na Mwl. J.K. Nyerere. Lakini kwa mfumo tulionao napata utata kidogo. Itakumbukwa kuwa Mwl. J.K. Nyerere (Tanzania) alizisaidia sana nchi nyingi za Africa (Namibia, Msumbiji, Angola, South Africa, n.k) kupata Uhuru kwa kutumia rasilimali zetu wenyewe (fedha, silaha, muda, ardhi n.k), bila sisi Tanzania kufaidi chochote kutoka kwa mataifa hayo zaidi ya Heshima tu iliyojengeka miongoni mwetu. Kwa kipindi hicho sipaswi kujiuliza wala kumlaumu Mwl Nyerere eti kwanini alitumia rasilimali nyingi tu bila ya kupata faida zaidi ya kujijengea heshima. Hii ni kwasababu ya msimamo itikadi ya Mwl. Nyerere (Tanzania) kuwa Africa ni moja na binadamu wote ni sawa, hakuona tofauti ya Mtanzania, Mkongo wala Msouth Africa kiuchumi, kisiasa, kijamii, na kiutamaduni kwakuwa wote ni ndugu. Lakini kwa kipindi hiki cha mfumo wa UBEPARI (Capitalism), sio rahisi kutumia mawazo ya Mwl Nyerere na katika kusisaidia DRC na kwingineko kuwa huru kijeshi, kiuchumi na kijamii. Sera za ubepari zinatambua wazi kabisa kwamba hata siku moja hakuna rafiki wa kudumu bali kuna maslahi ya kudumu. Kwamba nje ya mipaka hakuna Dada wala Kaka, wala Mjomba, kuna maslahi ya nchi. Sasa swali ninalojiuliza maslahi yetu DRC, Comoro n.k ni yepi? Nini sera yetu katika ukanda huu wa maziwa makuu? Najua sera yetu ya mambo ya nje ni Economic Diplomacy, Je inatekelezwa au inatekelezeka huko DRC, Comoro?. Kagame na Kaguta sera zao zilikuwa wazi kabisa DRC kwamba waifanye isitawalike ili wao (Kagame & Kaguta) wafaidi Madini na rasilimali nyinginezo (ambapo kimsingi wapo sawa kulingana na sera na mfumo wa ubepari), Je Tanzania kuifanya DRC, Comoro etc zitawalike nini tulifaidi/tunafaidi kwa mtizamo wa sera na mifumo ya kibepari Vs economic diplomacy ya kwetu?
 
Hongera zake...lakini bado Tanzania tunamdai meengi tu
 
Back
Top Bottom