JK apanda chati DRC!!!

JK apanda chati DRC!!!

Maumivu ya kichwa huanza pooole pole,kisha......................
still loading
 
Haya Chadema Makamanda wenzenu wa M 23 aka M 4c wanachezea za uso huko ..
kawasaidieni sio kupiga porojo tu hapa...
 
Da
Hawaja
jamaa
Walikua
Wanawaita
JWTs
Skaut
Yaan
nimefulai
Sana
 
Acha Ufala wewe, Usichomekee utumbo kwenye mambo ya uzalendo. Ungetafuta maala pake lakini sio kwenye mtililiko huu. Usiwakatishe tamaa JWTZ, kiazi wewe.

Tumia akili Mbulula wewe uzalendo uko wapi hapo kwani wanaipigania Tz? hao askari wetu wapo huko kwa maslahi ya nani? Tulitumia nguvu kubwa sana kuzikomboa nchi za kusini mwa sahara wakati wa ukoloni lakini tulipovamiwa na Nduli mwalimu aliwaomba walau wamkemee tu Amini lakini hamna hata mmoja aliyemkemea wala kutusaidia it's time now tuelekeze nguvu kujenga taifa letu na sio kujijengea maadua huu ni mradi wa watu huu
 
DRC ina watu millioni 70, ina madini, ina misitu... lakini inasumbuliwa na Rwanda yenye watu milioni 12? Hata ukijumlisha na milioni 34 wa Uganda, kweli ndio wa kuinyanyasa ncho kubwa namna hiyo?!!!
Kweli waafrica tumelaaniwa... si bure...

I think you have so litle or no knowledge at all on War and National Defense Principles.Do some homework please
 
Ndugu, hapa tunaongelea mambo ya nchi dhidi ya nchi za nje. Mambo ya magamba yanakujaje ndugu? Inapokuja kutetea taifa dhidi ya udhalim wa kutoka nje twahitaji kusimama pamoja. Mambo ya ndani si mahali pake kwenye hii thread ndugu. Samahan km ntakua nimekosea. Ni mtazamo wangu. Nampenda Rais wangu Mh Jakaya Kikwete, naipenda nchi yangu Tanzania

Nimekusoma mkuu
 
Hata mimi napenda alichofanya JK lakini asisahau kuchukuwa madini na mbao huko kulipia gharama tunazoingia wakati wa kutekeleza jukumu letu la kuwafanya Wakongo nao waishi na kuifurahia nchi yao kama binadamu wengine.

nimeipenda hii
 
bila shaka wewe upo ulimwengu wa shetani. hivi ni kweli hujui kuwa majeshi yetu yapo DRC? au unajitia ukipofu tu? kama uliagizwa umpinge jk si kwa kila kitu. huo ni utumwa wa mawazo

Hayo majeshi huko yapo kwa manufaa ya nani? Kwanini hamtaki kujiuliza hili swali na mnakimbilia kushabikia tu
 
hiyo ngoma ni moja kwa moja hadi Kigali. UN ilitoa saa 48 kwa m23 kujisalimisha la sivyo watapokonywa silaha. muda umemalizika na msako umeanza. baada ya goma safari kigali
Hawa jamaa wana mbinu nyingi za kutaka kuvuruga mipango ya UN, yaani wanafanya mambo ya kitoto kuhadaa DUNIA kwamba suala la DRC si rahisi kupatiwa ufumbuzi!! Kwa nini nalisema hili - leo Museveni kaja na mpya, anasema waasi wa Al Shabaab wamevamia mji mdogo wa Kongo uliopo mpakani na Uganda eti waliuteka kwa muda na kuwafanya RAIA wa Kongo kukimbilia nchini Uganda. Hivi Al Shaabab wana interest gani ndani ya DRC, kwa nini wajitokeze wakati M23 wamepewa masaa 48 kusalimisha silaha zao - kwa mawazo yangu naona huu ni mchezo wa kuhigiza uliochongwa na M7 na PK wakiwa na lengo la kushtua nchi za magharibi specifically Merikani ambayo imewakalia kooni, wala siwezi kushangaa kama wanaohitwa ni Al Shabaab ni kikosi kidogo cha majeshi ya M7 au PK kilifanya operation hii kutaka ku-draw attention za International Community oh yes publicity STUNT. Ukiangalia kwa makini utagundua siku hiyo hiyo au kesho yake Balozi wa Rwanda ndani ya UN alipokuwa anaulizwa maswali/ufafanuzi na wandishi wa habari alikuwa anajibu kimkato mkato kwa jeuri na kiburi kabisa mtu unashangaa hawa watu wamelelewa VIPI - jamaa hawa wako mahili sana katika harakati zao za kudanganya DUNIA, wanacho tafuta hapa ni kutaka kuonyesha kwamba saula la DRC ni gumu kutatuliwa, madai ya kusema kwamba kundi la AL Shabaab wamekwisha jipenyeza ndani ya DRC(uongo mtupu) lina lengo la kuvuruga mipango ya UN, yaani UN ipunguze kasi ya kuwashughulikia M23 na kuanza kufikilia Al Shaabab wa kuchongwa na jamaa hawa. Nataka niwakumbushe kwamba dunia imekwisha washtukai mbinu zao, wasipo jirudi watasjilahumu sana siku za usoni.
 
Tumia akili Mbulula wewe uzalendo uko wapi hapo kwani wanaipigania Tz? hao askari wetu wapo huko kwa maslahi ya nani? Tulitumia nguvu kubwa sana kuzikomboa nchi za kusini mwa sahara wakati wa ukoloni lakini tulipovamiwa na Nduli mwalimu aliwaomba walau wamkemee tu Amini lakini hamna hata mmoja aliyemkemea wala kutusaidia it's time now tuelekeze nguvu kujenga taifa letu na sio kujijengea maadua huu ni mradi wa watu huu
Ukiwa bavicha ni tatizo kubwa.
 
Hayo majeshi huko yapo kwa manufaa ya nani? Kwanini hamtaki kujiuliza hili swali na mnakimbilia kushabikia tu
Upeo wa mawazo yako ni mdogo hivyo huwezi kuona mbali we baki hapo bavicha tu.
 
hizo movie za freemason chagawood ltd haziishi na leo,wametulia kidogo maana mkanda wa bomu la Arusha haujakamilika nasikia wamepeleka Germany kufanyiwa marekebisho
Hiyo movie ya MTWARA
mnaweza kuendelea nayo, ila haiwezi kulikatisha tamaa jeshi letu
kuhakikisha amani inapatikana kwa majirani zetu.
 
*Wananchi wamuona mkombozi,shujaa wao!
*Wabunge wa DRC kufunga safari hadi ikulu ya Magogoni kumshukuru!
*Kumuomba kichapo cha Nduli Amini kirejewe kwa Kagame!
*M23 waishi kama Ngedere kwa matunda porini!
*Ni baada ya kichapo cha masaa2 tu toka JWTZ!
*Wakimbia waacha silaha,vyakula!
*Saa 48 walizopewa kuweka silaha chini zazidi kuyoyoma!

Ni post kama hizi zinaishushia hadhi JF halafu wapuuzi wanaoleta posti kama hizi ndio wa kwanza kueneza upuuzi wao kwingineko kwamba JF kumejaa uzushi na umbea. Zamani kidogo mtu akileta mada kama hii wadau kabla ya kuchangia walijitahidi angalau kupata ukweli wa mambo kabla ya kuanza kuchombeza huku wakichakachua kama ilivyo kawaida ya wapuuzi wenzao popote pale walipo.

Ni vizuri kwanza kujiuliza; ni kitu gani kinatokea Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo au République Démocratique du Congo na kwa nini wapiganaji wetu wako huko. Je mleta mada anaijua MONUSCO, The United Nations Organization Stabilization Mission in the Democratic Republic of the Congo or MONUSCO? Utafiti kidogo tu ungemsaidia mleta mada kuelewa kwa nin wapiganaji wetu wako Congo na wanatimiza wajibu kwa maelekezo ya nani.

Sitapoteza muda wangu kujibishana na mleta mada (nakataa katakata kukimbizana na kichaa!) ila nitamwambia tu kwamba Tanzania ni mojawapo kati ya nchi nyingi tu karibia sitini (60) zilizoitikia wito wa UN zenye askari wake nchini Congo kulinda amani. Mpaka mwishoni mwa mwezi wa Juni MONUSCO ilikuwa na askari zaidi ya 20,438 na nchi zinazoongoza kwa kuwa na askari wengi ni pamoja na;

  • India..............3,731
  • Pakistan.........3,714
  • Bangladeshi....2,540
  • .
  • .
  • .
  • Tanzania.........1,247
Kwa ufupi ni kwamba idadi ya askari wa Tanzania walioko Congo ni kama asilimia 5% tu ya wapiganaji kutoka nchi mbali mbali. Sasa swali langu kwa mleta mada ni hili; je huo ukombozi kama upo utakuwa umeletwa na Kikwete au Umoja wa Mataifa. Ushauri wangu kwa wote walichangia hii mada; kuna mbinu ya kuichafua JF kwa mada za kipuuzi na kijinga zimeshika kasi, tuchukue tahadhari tunapozichangia.

Toka mwaka 2010 kuna virusi vinaishambulia JF kwa lengo la kulidhoofisha nguvu na siku zinavyosogea ndio virusi vinaongezeka...tusije tukashangaa kwa hii ari na kasi mpya kuelekea 2015. Kuwatambua ni rahisi sana wanapovamia mada, hawatoi nafasi hata ya kujibiwa...unaweza kuta kurasa moja imejaa majibu kutoka kwa kirusi hicho hicho kimoja, vina mission maalum lakini dawa za kinga pia zipo, kazi kwenu.
 
Kwa hili JK nampongeza sana, na msimamo wake kuwa wakimbizi warudi kwao sasa Kagame hataleta kuchungia ng'ombe wake kule Ngara
 
Magamba kwa kuanzisha majiviwanda ya uongo tu hamjambo mbona JWTZ wapo busy kupiga na kubaka watu huko Mtwara? au M23 ndo wapo mtwara siku hizi?

Licha ya kejeli zote ila itabaki palepale kwamba JK ni miongoni mwa maraisi bora ktk taifa letu,hata huo uhuru wakuandika utakavyo ktk mtandao wakijamii ni miongoni mwa ubora wake,ila haishangazi kwani kwakawaida nabii hasifiwi kwao.Hongera JK hongera JWTZ
 
hivi JK mtamsifia hadi lini, harafu mnatumia nguvu sana. Sifa huja zenyewe, angalia sifa alizonazo filikunjombe kwani alitafuta mpiga debe??? Juzi wakazi wa songea walikuwa wakimshangilia kila neno moja analosema tofauti kabisa na waziri mkuu. Aliposimama filikunjombe wananchi walisimama na kuanza kushangilia kama mkombozi kasimama.

Sasa nyie mnafanya kazi on empty.
Khaa!! Kumbe kuna wanaM23 humu:bored:
 
Mmshauri JK akamalizie muda wake wa urais DRC maana ya Tanzania yamemshinda, nina hakika Kabila atamuachia urais na yeye atakuwa makamu wake.
 
Back
Top Bottom