JK ana BIFU na Mwalimu Nyerere Foundation?

Phillemon Mikael

Platinum Member
Nov 5, 2006
10,518
8,583
Majuzi tumeazimisha miaka kumi bila mwalimu..yalikuwa ni maazimisho makubwa kwa kila hali,kikubwa si sherehe zinazoambatana na protokali bali kikubwa na hisia zilizojaa mioyoni mwa wananchi walio wengi juu ya Baba wa TAIFA.

Taasisi ya mwalimu nyerere ..iliasisiwa na mwalimu ikiiwa pamoja na mambo mengine ni kuendeleza yale aliyokuwa akiyaamini ...mwenyekiti wa kwanza wa taasisi ni mwalimu nyerere mwenyewe,kabla ya kumuachia Dr salim..,wajumbe wa bodi wapo wafuasi wa mwalimu kama kina butiku,warioba,mongela na wengine...Pamoja na kukabiliwa na ukata taasisi hii inayo heshima afrika labda nyuma ya taasisi nyingine kama MANDELA FOUNDATIONS na MO IBRAHIM foundation..,angalau inalo la kujivunia ,imekamilisha amani ya burundi kupitia upatanishi wake.

Taasisi kama ya mandela moja ya vyanzo vikuu vya mapato ni michango ya wahisani na kuungwa mkono na serikali husika.mfano sherehe za kuzaliwa mandela ni kati ya chanzo kikuu cha mapato....nadhani hata hapa Nyerere day ingetosha kuwa siku ya kuichangia taasisis kwa hali na mali....lakini nahisi imekuwa wahanga wa siasa za visasi.

Wenye macho na akili[hata za kawaida] wameona juzi ..namna kwenye maandalizi ya miaka kumi ya mwalimu ..taasisi ya mwalimu ilivyotengwa na serikali.Wakati taasisi ilijikakamua kuandaa hafla dar na mihadhara kumkumbuka mwalimu,ambapo katika cakula cha jioni ...serikali ilimtuma waziri mkuu,....hali ilikuwa tofauti butiama kwani viongozi wa taasisi ya mwalimu nyerere hawakualikwa au awakupewa umuhimu kwenye shughuli ile ya kitaifa,ile ilikuwa kasoro kubwa kwa waandaaji!

Wakati wa uwekaji wa mashada ..pale butiama mwenyekiti wa taasisi dr salim na katibu wake butiku hawakuwepo pale kwenye mwalimu maoseleum...,hata warioba na mongela waliokuwa pale waliweka mashada kuwakilisha waliofanya kazi na mwalimu....,Je hatuna sababu ya kuamini kuwa hali ile ilipangwa ?? je kikwete hawapendi viongozi wa mwalimu nyerere foundation...?...haiwezekani taasisi iliyo na jukumu la kuweka hai mawazo na imani a mwalimu isiwepo au isialikwe na watu tushindwe kuona hilo kwa jicho la tatu!!

Hata pale uwanjani ...hakuoneka kiongozi wa mwalimu foundation yeyote kutambulishwa...,na hataa safari hii tena warioba alisahauliwa hadi baadaye ndio akatambuliswa safari hii kama waziri mkuu mstaafu..wakati wanatambulishwa mwakilishi wa watoto wa mwalimu na wajukuu.

sitaki kuamini kama visasi vya uchaguzi wa mwaka 2005..ndio mwendelezo wa haya......
 
Naomba kuanza kuuliza kwani Mwalimu Foundation is a governamental institute????????
Haya ndio maisha!Ukifa hudhaminiwi ila Mwalimu amedhaminiwa vya kutosha kwa kumuenzi!
Sioni haja ya kuwatumikia hao Wazalendo wa hiyo Foundatoin simply because wanafanya kazi katika taasisi iliyoanzishwa na Mwalimu Nyerere.
Cha muhimu tunayaenzi mambo ya Mwalimu na kuendeleza historia yake.Nyerere Foundation ifanye kazi na siyo kujiingiza kwenye mambo ya Kiserikali!
 
mwalimu nyerere foundation is not an gov institue ...but ipo kuratibu ....yale aliyokuwa akiamini na kusimamia mwalimu..ili yaridhishwe kwa vizazi....nadhani si sawa kusema ukifa ,umekufa...kwani kila nchi inayo namna ya kuezi mambo yake....ndio maana mawazo ya watu kama mahatma gandi ,che guevara..etc yapo kwa ajili kuna taasisi zinazoratibu....

huwezi tofautisha ..na kusema unamuezi mwalimu bila kuenzi kazi zake..potelea mbali hata kama viwanda na majumba tumeuza.....tusiangalie nani anaongoza foundation .....tuiangalie kama ya mwalimu!!
 
You can clutch the past so tightly to your chest that it leaves your arms too full to embrace the present!
 
Katika viongozi hawa wa sasa walimpenda na kumuenzi mwalimu kwa kuwa aliwapatia fursa ya kutawala na kuchuma bila ukomo huku wakijijengea himaya za kifalme yaani kurithishana uongozi kwa familia na rafikiz
 
Labda tujiulize 'kumuenzi Mwalimu Nyerere' maana yake ni nini. Pamoja na kuwa labda wengine nyuma ya kompyuta zetu hatufahamu ukweli wa mambo kuhusu hili swala, lakini nilifikiri kumuenzi Mwalimu Nyerere ni pamoja na kuhakikisha MNF inaratibu ipasavyo mambo aliyoyafanya mwalimu na kuipa heshima inayostahili. Ukweli ni kwamba huwezi kuzungumzia ushiriki wa Tanzania katika usulihishi wa migogoro katika nchi za maziwa makuu-Ambayo Tanzania inasifika kwa hilo bila kuitaja MNF. Ninafikiri serikali itakapoiwezesha MNF kufanya kazi ipasavyo na kuithamini itakuwa ni njia mojawapo ya kumuenzi Mwalimu zaidi ya kuhitimisha mbio za mwenge Butiama, kusikiliza hotuba zake, na kuzipa shule, barabara na vitu vingine jina la 'Nyerere'
 
Ameanziwa sana mpaka na wasiwasi si muda mrefu wajinga watamfanya mungu (mungu aepushe)
1. Uwanja wa ndege unaitwa kwa jina lake
2. Maonyesho ya sabasaba kwa jina lake
3. Shule, barabara, etc
need more...mbio za mwenge kila mwaka...duuu
need more..foundation ipewe ..priority na serikali duu...
need more...mchakato wa wa kuwa st. uko ukingoni..duu..
By the way what good he did for a country:
a) Blah blah za umoja, kama vile alikuwa mwenyewe Akh!
Failure is always hero for our people poleni sana...nashukuru kama JK ataachana na hili Libabu nuksi...
 
Ameanziwa sana mpaka na wasiwasi si muda mrefu wajinga watamfanya mungu (mungu aepushe)
1. Uwanja wa ndege unaitwa kwa jina lake
2. Maonyesho ya sabasaba kwa jina lake
3. Shule, barabara, etc
need more...mbio za mwenge kila mwaka...duuu
need more..foundation ipewe ..priority na serikali duu...
need more...mchakato wa wa kuwa st. uko ukingoni..duu..
By the way what good he did for a country:
a) Blah blah za umoja, kama vile alikuwa mwenyewe Akh!
Failure is always hero for our people poleni sana...nashukuru kama JK ataachana na hili Libabu nuksi...

Near to nothing BUT much harm to the country!!!
 
Hakuna sababu yeyote ya msingi kwanini Mwalimu Nyerere foundation iwe na ukata; nahisi kuna tatizo katika utendaji wa taasisi hii kwani inaendeshwa kama vile ya kifamiliana ndio maana haishamiri kama vile watu wengi walivyotegemea. Mandela foundation inaendeshwa na professionals walioajiriwa kwa uwezo wao na wale waliofanya kazi na mzee Madiba wao sio watendaji bali wako kwenye board ya foundation; hivyo basi kila kitu kinatekelezwa kiutaalam unlike the Mwalimu foundation where Butiku by virtue of being a relative wa Mwalimu amejiweka kuwa mtendaji mkuu. Pia swala la fedha kutotumika vyema wakati foundation inasimamia mgogoro wa Burundi ilileta credibility problem kwa foundation!
 
Ameanziwa sana mpaka na wasiwasi si muda mrefu wajinga watamfanya mungu (mungu aepushe)
1. Uwanja wa ndege unaitwa kwa jina lake
2. Maonyesho ya sabasaba kwa jina lake
3. Shule, barabara, etc
need more...mbio za mwenge kila mwaka...duuu
need more..foundation ipewe ..priority na serikali duu...
need more...mchakato wa wa kuwa st. uko ukingoni..duu..
By the way what good he did for a country:
a) Blah blah za umoja, kama vile alikuwa mwenyewe Akh!
Failure is always hero for our people poleni sana...nashukuru kama JK ataachana na hili Libabu nuksi...

Huna lolote...Tuondolee PUMBA zako hapa
 
tatizo ni kuwa watu wanaiongoza taasisi hiyo siyo mashabiki wakubwa wa JK.. so.. kwanini JK awawezeshe?
 
hurt.pork2000.jpeg
Akh! Niondolee upumbavu wako?
 
Ameanziwa sana mpaka na wasiwasi si muda mrefu wajinga watamfanya mungu (mungu aepushe)
1. Uwanja wa ndege unaitwa kwa jina lake
2. Maonyesho ya sabasaba kwa jina lake
3. Shule, barabara, etc
need more...mbio za mwenge kila mwaka...duuu
need more..foundation ipewe ..priority na serikali duu...
need more...mchakato wa wa kuwa st. uko ukingoni..duu..
By the way what good he did for a country:
a) Blah blah za umoja, kama vile alikuwa mwenyewe Akh!
Failure is always hero for our people poleni sana...nashukuru kama JK ataachana na hili Libabu nuksi...


akili ni nywele; kila mtu anazake!

Sasa George Washington ana majengo mangapi ambayo yanaitwa kwa jina lake? Martin Luther King ana barabara ngapi, na maeneo mangapi yanayotajwa kwa ukumbusho wa jina lake? Hivi Mandela anakumbukwa vipi katika miundo mbinu mbalimbali huko SA?
 
akili ni nywele; kila mtu anazake!

Sasa George Washington ana majengo mangapi ambayo yanaitwa kwa jina lake? Martin Luther King ana barabara ngapi, na maeneo mangapi yanayotajwa kwa ukumbusho wa jina lake? Hivi Mandela anakumbukwa vipi katika miundo mbinu mbalimbali huko SA?

Well said mkuu..Tumain anahitaji maombi.He needs the Holy Spirit
 
You all have a programmed mind..endelee kuimba na kuimbishwa...to the great failure...

Teh teh..Wewe ndo mind yako imeganda na imejaa chuki(maneno yako yaeleza kila kitu),kama vp soma Darasa fupi la Mwanakijiji hapo juu kwenye post yake ya mwisho).Na wewe ndo a GREAT FAILURE aisee.Jiulize ni kwa nini US na SA wanawaenzi viongozi wao wa zamani George Washington na Nelson Mandela,ama kwa nini nchi kama Indi kila kitu kipya utakuta chapewa majina kama Mohandas(Mahatma) Karamchand Gandhi,Jawaharlal Nehru,Indira Gandhi ama Rajiv Gandhi...Acha chuki zako zisizo kuwa na maana wewe,ebo!!!
 
Teh teh..Wewe ndo mind yako imeganda na imejaa chuki(maneno yako yaeleza kila kitu),kama vp soma Darasa fupi la Mwanakijiji hapo juu kwenye post yake ya mwisho).Na wewe ndo a GREAT FAILURE aisee.Jiulize ni kwa nini US na SA wanawaenzi viongozi wao wa zamani George Washington na Nelson Mandela,ama kwa nini nchi kama Indi kila kitu kipya utakuta chapewa majina kama Mohandas(Mahatma) Karamchand Gandhi,Jawaharlal Nehru,Indira Gandhi ama Rajiv Gandhi...Acha chuki zako zisizo kuwa na maana wewe,ebo!!!
So what? kwakuwa wamefanya india na Tanzania ...tufanye (Programmed) mind ..after all huwezi kulinganisha Washington na nyerere...
Chuki blah blah hizo ...nimeshasikia mara nyingi sana kwa watu walioshindwa hoja kwahiyo ...endelea kuimba na kuimbishwa kwa kuwa akili yako na ya wenzako kama wewe mwkjj inclusive tunawaita wale waleeeeeee "Programmed mind"
 
So what? kwakuwa wamefanya india na Tanzania ...tufanye (Programmed) mind ..after all huwezi kulinganisha Washington na nyerere...
Chuki blah blah hizo ...nimeshasikia mara nyingi sana kwa watu walioshindwa hoja kwahiyo ...endelea kuimba na kuimbishwa kwa kuwa akili yako na ya wenzako kama wewe mwkjj inclusive tunawaita wale waleeeeeee "Programmed mind"

Asinus asinum fricat
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom