Jirani yangu simwelewi

Jirani yangu simwelewi

Nashindwa kumuelewa jirani yangu na ananifanya nisiwe comfortable.... Nyumba ninayoishi tupo watano kila mtu na kwake anaijtegemea wote ni vijana na hakuna mwenye familia. Tupo wadada wawili tu. Huyu dada jirani yangu alinikuta wakati akihamia hapo na mwanzoni alipata matatizo nikamsaidia kama kama ambavyo ningemsaidia binadamu yoyote. Aliumwa na hakuwa na ndugu karibu (kwao Shinyanga) hivyo nilimhudumia kwa ukarimu wote nilimpikia, na kumsaidia kufanya usafi hadi alipopata nafuu.

Baada ya kupona maisha yaliendelea japo hatukua na ukaribu zaidi ya salamu na mambo basic kama kushare bills. Kumbuka sisi ni vijana na pretty much ndio tumeanza kujitegema so hatujajiestablish kihiivyo...ila nimegundua huyu jirani yangu ni kama anawivu ama sijui ni kitu gani. Alipokuja kwangu kila alichokiona alitaka kujua ni menunua bei gani na vingine alidiriki kuniuliza umenunuliwa na mpenzi wako? Sikumbuki nilipotezeaje coz sionagi kama ni sawa ku disclose mambo yangu binafsi kwa mtu ambae sio wa karibu.

Ila naona ni kama tabia kila tukionana akiona nimebadilisha style atauliza umesuka bei gani, juzi kaniona na simu kaniuliza mbona hujanionyesha kitu kipya. yani hata nikinunua maybe kiblouse kipya lazima atauliza. Kinachonimaliza ni kwamba hata kama niko ndani napika ataongea from her room eeeeh jirani leo unapika samaki au leo unapika kitu flani? Hua namjibu kwa maneno machache tu.

Bottom line ni kwamba she makes me uncomfortable!!!!!!! Yani very uncomfortable!!!!! Akiona mpenzi wangu wangu yupo ndani atakuja kunigongea either aombe kitunguu au kibiriti.

Nisaidieni jirani wa hivi naishije nae?????


Kama katoka shinyanga na hana ndugu mjini
usikute ni mshamba tu wa jiji
sasa nywele zinauzwa hadi vichochooni yeye anakushangaa wewe
iusikute wewe ndo 'Jlo wake wa kwanza kuishi nae mjini hapa'

mfundishe tu taratibu ataelewa.....na vile ulivyo vichoka choka mpe tu...
ila pia tabia ya kukugongea akiona 'kidume' usikute ana tabia za umbea na majungu na kuchimbachimba watu
so very soon utasikia aliyoyatunga if anazo....
 
Jirani jirani yanguuu nimekukosea niniii??? Aaah Wapi Twanga Pepetaaa
 
Nikionaga Avatar Ya kabanga Yule Mtu Alivyonuna Basi Aisee Na Sawa... Za Kabanga Nazisomaga Kwa Bass Nadhan Ile Avatar Ndo Inaongea Kwa Bass
Hahahaha!jaman,hivi nilijua ni mimi tu,bwana kabanga ananichekeshaga sana majibu yake mafupi tu nikirudi kwenye Avatar yake ndo nazidi kucheka,kwakweli natamani sana kumuona anafananaje mtu huyu.
 
Wanawake ktk ubora wao kuna kauli inasema wanawake hawapendani sijui ni kweli badilika kutokana na mazingira dada yangu kila mmoja amekulia ktk malezi tofauti mfano binafsi siwezi kukaa maskani na wala spendi kujichanganya na watu yaani niko kiupekee pekee na mda mwingi napenda niwe peke yangu just ni malezi tu ila fika mda unapaswa ubadilike kutokana na mazingira hebu mkaribishe awe rafiki yako usimzuie asiwe karibu na ww mkaribishe na ajue ww ni mtu wa aina gani yataondoka hayo maudhi km huwezi just ondoka hapo.
 
Pole sana,cha kufanya mchane tu,kama unashndwa kumwambia direct kuwa hupendezwi na tabia yake basi muonyeshe ishara kuwa hupendi akifanyacho,kama ni muelewa basi atafaha
 
Siku moja usiku mwite chumbani kwako, akiingia zima taa sekunde tatu washa akukute umeshika bisu kubwa, atastuka, mwonye kwa ishara asisubutu kupiga ukelele, kisha mwambie, "USINIZOEE KUANZIA LEO VINGINEVYO UTAIJUA KAZI YANGU" zima taa mwambie "POTEA" hatorudia na nyumba atahama.
nimekubali aisee
 
Nikionaga Avatar Ya kabanga Yule Mtu Alivyonuna Basi Aisee Na Sawa... Za Kabanga Nazisomaga Kwa Bass Nadhan Ile Avatar Ndo Inaongea Kwa Bass
nimechka kwa nguvu.....kumbe na ninyi huwa mnamuona na zile aiseeeee zake! avatar yake inasadifu yaliyomo ndani yake
 
huyo ni nyakunyaku siyo bure hata yaaan usimzoeee ana tamaa pitilizi
Roho mbaya haijengi. Mwenzio ndio kwanza kaingia jijini akishalijua jiji hayo yote yataisha. Kwani wewe ulijitawazisha mwenyewe udogoni?
 
Watu wa aina hii wapo sana. Wazoee tu. Ukute hakuna zaidi ya admiring tu.

Kuna kina dada flani hivi tunafanya kazi eneo moja. Kila mara wananiuliza nani ananisafishia viatu, nanunua wapi nguo, yadda yadda yadda. Mwingine aliomba shati nililovaa nikajua utani, bwana we.... niliishia kumpa tu.
yewoooo...ukampa shati lako?? hilo lishafika kwa babu tanga. tusubiri tu ndoa sasa. alililiiiiiiii....
 
Watu wa aina hii wapo sana. Wazoee tu. Ukute hakuna zaidi ya admiring tu.

Kuna kina dada flani hivi tunafanya kazi eneo moja. Kila mara wananiuliza nani ananisafishia viatu, nanunua wapi nguo, yadda yadda yadda. Mwingine aliomba shati nililovaa nikajua utani, bwana we.... niliishia kumpa tu.
Duh usirudie kugawa nguo aisee kuna watu wa ajabu acha.
 
Well maybe its mere admiration and I'm over reacting or maybe ni uswahili wa kufatiliana sijui but either way It makes me uncomfortable. Like you said watu wa hivyo wapo ila if you're smart enough to read peoples minds you'll know who is genuine and who is not. In my case my neighbor isn't...that's what irritates me the most!
huyo ni mswahili tu mwenye tamaa na mmbea. Nimeshakutana nao. Nilipomaliza chuo nilikaa nyumba ya peke yangu uswahilini kidogo nikawa naishi kivyangu vyangu sina habari na mtu zaidi ya salamu, ila baadae nikasema nisijitenge sana niwaungishe hata kusuka tu. loh! nilijuta. Mpaka umalize kusukwa ushahadithiwa stori ya kila mwanamke hapo mtaani na wala huwajui unaishia tu enhe..inhi..mmh. Ameshakwambia siri zake zote (we ndo unaona ni siri). Halafu wanawake wa kiswahili karibia wote wanajua wenzao vitu tunanunuliwa na wanaume, kwa hiyo akikuona na kitu kizuri anajua una "bonge la bwana"! Wale watu wanaishi maisha ya raha sana, hawana stress. Ambition kubwa ni kumiliki dera kama la flani, acheze upatu anunue "desin tebo" kama ya fulani .. baas.
 
Ukiendelea kumchekea atakojozwa na boyfriend wako. Hapa ni mjini.
 
Back
Top Bottom