huyo ni mswahili tu mwenye tamaa na mmbea. Nimeshakutana nao. Nilipomaliza chuo nilikaa nyumba ya peke yangu uswahilini kidogo nikawa naishi kivyangu vyangu sina habari na mtu zaidi ya salamu, ila baadae nikasema nisijitenge sana niwaungishe hata kusuka tu. loh! nilijuta. Mpaka umalize kusukwa ushahadithiwa stori ya kila mwanamke hapo mtaani na wala huwajui unaishia tu enhe..inhi..mmh. Ameshakwambia siri zake zote (we ndo unaona ni siri). Halafu wanawake wa kiswahili karibia wote wanajua wenzao vitu tunanunuliwa na wanaume, kwa hiyo akikuona na kitu kizuri anajua una "bonge la bwana"! Wale watu wanaishi maisha ya raha sana, hawana stress. Ambition kubwa ni kumiliki dera kama la flani, acheze upatu anunue "desin tebo" kama ya fulani .. baas.