Jinsi tunavyoibiwa petrol station

Jinsi tunavyoibiwa petrol station

Kuna vituo wako vizuri saana. Kuna Total Mlimani City na PUMA mandela road. Vingine huwa siwaelewi.
Vituo hivyo ulivyotaja hata kwa muonekano tu,unajua kuna biashara halali,hawa wengine nahisi mabosi wanajua,pengine wanagawana %
 
Dawa yake kidumu. Mimi huwa ninachumba ya maji ya lita moja kwenye gari. Nikifika nawatisha kuwa nataka kwanza lita moja ya kwenye hiyo chupa, wakichomoa nasepa. wakikubali nanunua lita moja kwanza alafu ndio naweka kwenye tank ya gari.

HIZI SIO NYAKATI ZA KUONEANA AIBU
Ha ha ha,umenena vema,aibu itatufanya tushindwe kufika malengo
 
Salamu wanajukwaa,leo asubuhi nimebaini jinsi wahudumu wa vituo vya kuuzia mafuta wanavyotuibia wateja.

Nilikuwa kwenye kituo cha mafuta siza nimepaki tayari kuwekewa mafuta baada ya kulakiwa kwa bashasha na kuelekezwa pump na wahudumu,kwa mara ya kwanza nilihisi wananiita kimashindano labda kuna bonus kwa mwenye mauzo makubwa.

Nilipaki kwenye pump ya kati katika tatu zilizopo,lakini nikaambiwa niende ya mwanzoni au mwishoni,mimi bado nikawa katika ileile pump ila muhudumu hakutaka kunihudumia pamoja na bashasaha za kunilaki mwanzoni.

Akaja mtu ana dumu la lita tano akapewa petrol akaondoka,akaja na mwingine pia akapewa,kwakuwa nilikuwa nawahi nikasogea pump ya mwishoni nikapata huduma nikaondoka huku nikitafakari sana kwanini imekuwa vile.

Baadaya ya kuwaza sana,nimegundua pump zile mbili yaani ya mwanzo na mwisho huwa zitatoa mafuta machache,kwa mfano ukinunua lita tano,basi unapata pungufu,na ndiyo maana wanasakizia wenye magari tuende huko kwakuwa hatutayaona.

Pump ya kati itakuwa inatoa ujazo sahihi ndiyo maana huwa wanawauzia wenye vidumu tu.

Hili nimeliona pia kinondoni katika kituo kikongwe sana.

Nawaomba wenye magari tukatae kuhamishwa pump jamani,inaonyesha watu wa VIPIMO hawajalibaini hili.

Karibuni tupeane uzoefu.
Hao ni big bon tuu kwa jinsi ulivyoelezea
 
Hii nimeiona mara nyingi sana: Pump unayoshinikiziwa kupark gari huwa mara nyingi inakuwa imetoka kujaza volume ndogo ya mafuta kwenye chombo kingine cha moto, so ukipark hapo wanaanza kufuel kwako bila kuanzia ZERO reading ya meter yao (Mostly utakotakuta either imetoka bajaji or bodaboda) unaishia kulipa 20,000/= kumbe umewekewa mafuta ya 14,000/= hiyo 6000 ni faida kwake.

Pia huwa wanakuchangamkia mwingine anakuongelesha mwingine anaweka pump kwenye gari na kujifanya wamesahau kukuuliza waweke mafuta ya sh. ngapi na wanakwambia wameshaanza kuweka. Tabia hii ipo sana sheli za fulani hapa maeneo ya ubungo.

Huwa nikifika hapo nazima gari nashuka kabisa ndio naanza kuonea nao

Uko sahihi kabisa mkuu tena kuna sheli pale mwanamboka ukiwaambia waanze na zero hawakubali kabisa tena ukifka wanakutolea pampu ile wanayoipenda madereva bodaboda
 
Dawa yao ni kujenga ka shell kadogo nyumbani kwako! Angalau ukichimbia katenk ka Lita 10000 Lt unatumia hadi unasahau!
Ni suala la bajeti tu!
Tenga eneo la nyumba yako iwe mfano Wa yard! Chimbia tank chini, nunua pump zile ndogo funga Kwa matumizi yako! Yakiisha unajaza tu!
Yanini kujipa stress na mafuta ambayo hujui ubora wake?
FAIDA ZA KUJAZA GARI FULL TANK
1. Mafuta hayatumiki sana, kinachotumika sana hapo ni gas inayokuwa generated ndani ya tank..tofauti ni kwamba mtu anayeweka mafuta ya kibaba yanapofika ndani ya tank yanasambaa na kuisha mapema tofauti na aliyejaza full tank.
2. Uhakika Wa safari ni mkubwa
3. Unaepuka uwezekano Wa pump kufuta uchafu uliochini unaweza leta madhala kwenye injini.n.k
MADHALA YA MAFUTA MACHAFU KWENYE GARI
1. Injini kufa mapema.
2. Petrol filters kuziba au kutoa uchafu.
3. Gari kuanza kumisi na kupoteza nguvu.
4. Gari kutoa moshi mwingi
5. Gari kuzima au kutetemeka.
6. Service za Mara Kwa mara
Kwa maelezo zaidi Jinsi ya kufanya mafuta yako yasiishe haraka hata Mara mbili zaidi ni PM nikupe dawa ya kudilute
Asante mkuu
 
Na wewe kwanini usishuke kuhakikisha zimesoma lita 5
Tatizo siyo meter reading,tatizo ni ujazo unaotoka kwenye kila mililitre au lita ndiyo inakuwa imepungua.
Anaejaza fulltank katika pump inayoiba basi anapoteza zaidi.
 
anawaza nini, watumbuliwe kwa sababu gani ? Kama unaibiwa to a taarifa Polisi sasa ewura na wakala wa Vipimo waje kukaa hapo shell au ndio wanaopima? Cha msingi kama unatilia shaka kituo toa taarifa kwa mamlaka hizo wachukuwe hatua wao sio malaika wa kuota kuwa kituo Fulani kinaiba, vinginevyo ukigundua tabia kama hizo hama kituo watakosa Wateja watajirekebisha
napita tu
Kwa wakala wa VIPIMO ni muhimu kuzikagua hizi pump kila kituo mara kwa mara.
 
  • Thanks
Reactions: cdc
Vitajeni vituo kwa majina tusaidiane madereva
Mimi kile cha Sinza Kijiweni kilishaga nitumbukia nyongo kuna Siku walinitenda
Mambo yote Siku hizi ni Gbp
Hapo nilienda,kuna mama mmoja bonge ana mkorogo hivi,huyo ukigeuka tu anaunganisha na ile hesabu isiyofutwa aliyotangulia kupewa mwenzio,hasa akiwa wa pikipiki.
 
Inatakiwa mipira ambayo ni transparent. Wese likipita tu unaona
 
Kumbe ndio maana huwa nahamishwa pump..., aisee nimeshtuka, kuanzia leo naenda pump ambayo hawataki.., wakinilazimisha nashuka natoa dumu la lita 5 tuone sasa
 
Kuibiwa tutaibiwa tuu cha msingi ni kuangalia Pump za kisasa hizi kidogo zipo ok na kitu cha pili angalia sehemu ambayo dala dala au gari za abiria kwa wingi zikijaza mafuta katika garage yeyote jua hapo mafuta kwa kiasi fulani wanatoa kwa usahihi maana hawa wa hiace wana hesabu sana mafuta yao kwa kila Route wanajua watatumia kiasi gani tofauti na private car..
 
Inatakiwa mipira ambayo ni transparent. Wese likipita tu unaona
Hiyo si suluhisho sana,vipimo wasimame katika ukaguzi wa mara kwa mara,katika mpira itayaona yanapita ila ujazo kwa lita ukipungua hautajua kama unaibiwa.
 
bado hujaeleza namna tunavyoibiwa. umeeleza hisia zako. nilidhani umegundua namna wanavyoiba.kumbe hamna kitu.
Acha ukilaza wewe, hayo mazingira yanaonyesha dhahiri kwamba kuna wizi, kugundua wizi kwa kuthibitisha ni kazi ya wakala wa vipimo, siyo kazi yake. Wewe utakuwa mfanya kazi wa filling station sio bure
 
Acha ukilaza wewe, hayo mazingira yanaonyesha dhahiri kwamba kuna wizi, kugundua wizi kwa kuthibitisha ni kazi ya wakala wa vipimo, siyo kazi yake. Wewe utakuwa mfanya kazi wa filling station sio bure
Uko sahihi sana mkuu
 
Nimejifunza kitu japo wa mkoa nitakua nanunua kwenye dumu naweka mwenyewe umbwa kabisa hao in manji's voice
 
Back
Top Bottom