Jinsi tunavyoibiwa petrol station

Mnondwe

JF-Expert Member
Apr 10, 2015
4,013
3,678
Salamu wanajukwaa, leo asubuhi nimebaini jinsi wahudumu wa vituo vya kuuzia mafuta wanavyotuibia wateja.

Nilikuwa kwenye kituo cha mafuta Sinza nimepaki tayari kuwekewa mafuta baada ya kulakiwa kwa bashasha na kuelekezwa pump na wahudumu, kwa mara ya kwanza nilihisi wananiita kimashindano labda kuna bonus kwa mwenye mauzo makubwa.

Nilipaki kwenye pump ya kati katika tatu zilizopo, lakini nikaambiwa niende ya mwanzoni au mwishoni, mimi bado nikawa katika ileile pump ila muhudumu hakutaka kunihudumia pamoja na bashasha za kunilaki mwanzoni.

Akaja mtu ana dumu la lita tano akapewa petrol akaondoka, akaja na mwingine pia akapewa, kwakuwa nilikuwa nawahi nikasogea pump ya mwishoni nikapata huduma nikaondoka huku nikitafakari sana kwanini imekuwa vile.

Baadaya ya kuwaza sana, nimegundua pump zile mbili yaani ya mwanzo na mwisho huwa zitatoa mafuta machache, kwa mfano ukinunua lita tano, basi unapata pungufu na ndiyo maana wanasakizia wenye magari tuende huko kwakuwa hatutayaona.

Pump ya kati itakuwa inatoa ujazo sahihi ndiyo maana huwa wanawauzia wenye vidumu tu. Hili nimeliona pia Kinondoni katika kituo kikongwe sana.

Nawaomba wenye magari tukatae kuhamishwa pump jamani, inaonyesha watu wa vipimo hawajalibaini hili.

Karibuni tupeane uzoefu.
 
Kiukweli imenikuta pale mwenge mpakani niliweka mafuta ya elfu 20 kwakawaida huwa najua wapi gauge huwa inafikia. Siku hiyo mshale haukupanda nilipouliza nikaambiwa utapanda badae, nimeenda mpaka home haupandi.

Sasa nikaja kujua sababu huwa nikijaza mafuta 20 kwa routes zangu huwa natumia siku mbili ila siku ile nikaishiwa mafuta siku ya pili kabla sijafikia ata robo ya trip. Nikaamua kuwafuata na bahati nzuri nikamkuta jamaa aliyeniuzia kumpiga mkwara akasema eti pump nilikuwa mbovu, nikwambia nitawaripoti kwa euwra, wakasema labda ilitokea shida.

Watu wa shell ni wapuuzi sana, ni wezi sana.
 
Kiukweli imenikuta pale mwenge mpakani niliweka mafuta ya elfu 20 kwakawaida huwa najua wapi gauge huwa inafikia. Siku hiyo mshale haukupanda nilipouliza nikaambiwa utapanda badae, nimeenda mpaka home haupandi.

Sasa nikaja kujua sababu huwa nikijaza mafuta 20 kwa routes zangu huwa natumia siku mbili ila siku ile nikaishiwa mafuta siku ya pili kabla sijafikia ata robo ya trip. Nikaamua kuwafuata na bahati nzuri nikamkuta jamaa aliyeniuzia kumpiga mkwara akasema eti pump nilikuwa mbovu, nikwambia nitawaripoti kwa euwra, wakasema labda ilitokea shida.

Watu wa shell ni wapuuzi sana, ni wezi sana.
Mtindo huu nimeona sehemu nyingi,ila pale baada ya vidumu kupata mafuta,nikaona ipo namna tu.
 
Salamu wanajukwaa,leo asubuhi nimebaini jinsi wahudumu wa vituo vya kuuzia mafuta wanavyotuibia wateja.
Nilikuwa kwenye kituo cha mafuta siza nimepaki tayari kuwekewa mafuta baada ya kulakiwa kwa bashasha na kuelekezwa pump na wahudumu,kwa mara ya kwanza nilihisi wananiita kimashindano labda kuna bonus kwa mwenye mauzo makubwa.
Nilipaki kwenye pump ya kati katika tatu zilizopo,lakini nikaambiwa niende ya mwanzoni au mwishoni,mimi bado nikawa katika ileile pump ila muhudumu hakutaka kunihudumia pamoja na bashasaha za kunilaki mwanzoni.
Akaja mtu ana dumu la lita tano akapewa petrol akaondoka,akaja na mwingine pia akapewa,kwakuwa nilikuwa nawahi nikasogea pump ya mwishoni nikapata huduma nikaondoka huku nikitafakari sana kwanini imekuwa vile.
Baadaya ya kuwaza sana,nimegundua pump zile mbili yaani ya mwanzo na mwisho huwa zitatoa mafuta machache,kwa mfano ukinunua lita tano,basi unapata pungufu,na ndiyo maana wanasakizia wenye magari tuende huko kwakuwa hatutayaona.
Pump ya kati itakuwa inatoa ujazo sahihi ndiyo maana huwa wanawauzia wenye vidumu tu.
Hili nimeliona pia kinondoni katika kituo kikongwe sana.
Nawaomba wenye magari tukatae kuhamishwa pump jamani,inaonyesha watu wa VIPIMO hawajalibaini hili.
Karibuni tupeane uzoefu.
Wewe ndiyo umejua leo. Wenzio kila gari lina kidumu unanunua kisha unaenda kuwekea mbele mwenyewe. Siyo huko Sinza tu ni karibu vituo vyote
 
Hii nimeiona mara nyingi sana: Pump unayoshinikiziwa kupark gari huwa mara nyingi inakuwa imetoka kujaza volume ndogo ya mafuta kwenye chombo kingine cha moto, so ukipark hapo wanaanza kufuel kwako bila kuanzia ZERO reading ya meter yao (Mostly utakotakuta either imetoka bajaji or bodaboda) unaishia kulipa 20,000/= kumbe umewekewa mafuta ya 14,000/= hiyo 6000 ni faida kwake.

Pia huwa wanakuchangamkia mwingine anakuongelesha mwingine anaweka pump kwenye gari na kujifanya wamesahau kukuuliza waweke mafuta ya sh. ngapi na wanakwambia wameshaanza kuweka. Tabia hii ipo sana sheli za fulani hapa maeneo ya ubungo.

Huwa nikifika hapo nazima gari nashuka kabisa ndio naanza kuonea nao
 
Kuna vituo wako vizuri saana. Kuna Total Mlimani City na PUMA mandela road. Vingine huwa siwaelewi.
 
Kuna vituo wako vizuri saana. Kuna Total Mlimani City na PUMA mandela road. Vingine huwa siwaelewi.
Dawa yake kidumu. Mimi huwa ninachumba ya maji ya lita moja kwenye gari. Nikifika nawatisha kuwa nataka kwanza lita moja ya kwenye hiyo chupa, wakichomoa nasepa. wakikubali nanunua lita moja kwanza alafu ndio naweka kwenye tank ya gari.

HIZI SIO NYAKATI ZA KUONEANA AIBU
 
Dawa yao ni kujenga ka shell kadogo nyumbani kwako! Angalau ukichimbia katenk ka Lita 10000 Lt unatumia hadi unasahau!
Ni suala la bajeti tu!
Tenga eneo la nyumba yako iwe mfano Wa yard! Chimbia tank chini, nunua pump zile ndogo funga Kwa matumizi yako! Yakiisha unajaza tu!
Yanini kujipa stress na mafuta ambayo hujui ubora wake?
FAIDA ZA KUJAZA GARI FULL TANK
1. Mafuta hayatumiki sana, kinachotumika sana hapo ni gas inayokuwa generated ndani ya tank..tofauti ni kwamba mtu anayeweka mafuta ya kibaba yanapofika ndani ya tank yanasambaa na kuisha mapema tofauti na aliyejaza full tank.
2. Uhakika Wa safari ni mkubwa
3. Unaepuka uwezekano Wa pump kufuta uchafu uliochini unaweza leta madhala kwenye injini.n.k
MADHALA YA MAFUTA MACHAFU KWENYE GARI
1. Injini kufa mapema.
2. Petrol filters kuziba au kutoa uchafu.
3. Gari kuanza kumisi na kupoteza nguvu.
4. Gari kutoa moshi mwingi
5. Gari kuzima au kutetemeka.
6. Service za Mara Kwa mara
Kwa maelezo zaidi Jinsi ya kufanya mafuta yako yasiishe haraka hata Mara mbili zaidi ni PM nikupe dawa ya kudilute
 
Dawa yao ni kujenga ka shell kadogo nyumbani kwako! Angalau ukichimbia katenk ka Lita 10000 Lt unatumia hadi unasahau!
Ni suala la bajeti tu!
Tenga eneo la nyumba yako iwe mfano Wa yard! Chimbia tank chini, nunua pumb zile ndogo funga Kwa matumizi yako! Yakiisha unajaza tu!
Yanini kujipa stress na mafuta ambayo hujui ubora wake?
FAIDA ZA KUJAZA GARI FULL TANK
1. Mafuta hayatumiki sana, kinachotumika sana hapo ni gas inayokuwa generated ndani ya tank..tofauti ni kwamba mtu anayeweka mafuta ya kibaba yanapofika ndani ya tank yanasambaa na kuisha mapema tofauti na aliyejaza full tank.
2. Uhakika Wa safari ni mkubwa
3. Unaepuka uwezekano Wa pump kufuta uchafu uliochini unaweza leta madhala kwenye injini.n.k
MADHALA YA MAFUTA MACHAFU KWENYE GARI
1. Injini kufa mapema.
2. Petrol filters kuziba au kutoa uchafu.
3. Gari kuanza kumisi na kupoteza nguvu.
4. Gari kutoa moshi mwingi
5. Gari kuzima au kutetemeka.
6. Service za Mara Kwa mara
mmmh aiswee hivi una kavitz kako hiyo jeuri unapata wapi ya kutengeneza hicho kisima chako!
 
EWURA atumbuliwe na wakala wa vipimo haswa ndo wenyewe
anawaza nini, watumbuliwe kwa sababu gani ? Kama unaibiwa to a taarifa Polisi sasa ewura na wakala wa Vipimo waje kukaa hapo shell au ndio wanaopima? Cha msingi kama unatilia shaka kituo toa taarifa kwa mamlaka hizo wachukuwe hatua wao sio malaika wa kuota kuwa kituo Fulani kinaiba, vinginevyo ukigundua tabia kama hizo hama kituo watakosa Wateja watajirekebisha
napita tu
 
Wewe ndiyo umejua leo. Wenzio kila gari lina kidumu unanunua kisha unaenda kuwekea mbele mwenyewe. Siyo huko Sinza tu ni karibu vituo vyote
Nakushukuru kwa msaada wa njia mbadala,umenipa somo.
 
Back
Top Bottom