M-bongotz
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 1,736
- 411
Ni wiki 2 zilizopita tu tulishuhudia hekaheka za maandalizi ya mkutano wa World Economic Forum pale Mlimani City, katika maandalizi yale kuna ile miti ilipandwa katikati ya barabara ile ya Sam Nujoma, nadhani lengo lilikuwa ni kuwahadaa wageni kuwa Bongo ni ever green, sasa mkutano umeisha ile miti inakauka pale na badala ya kuwa mapambo sasa inakuwa ni uchafu, nadhani kwa kuwa mkutano umekwisha jiji lingefanya mpango wa kutuondolea magogo yale tuendelee na hali yetu tuliyoizoea.