JF imenipatia binti.

JF imenipatia binti.

Hakuna lisilowezekana, ili mradi ulifanya hivyo kwa moyo wa dhati na kumtumainia Mungu mwenyezi. Hongera kwa kufanikisha mpango wako na kutoa mrejesho (feedback) katika jukwaa.

Yatendeni yampendezayo Mungu ili hatimaye siku moja yeye mwenyewe apate kuwaunganisha katika ndoa takatifu ili mpate kibali cha kuishi pamoja kama mume na mke katika kuutukuza uumbaji wake yeye muweza wa yote, huku mkipeana pasipo kunyimana na kusaidiana katika maisha yenu ya kila siku.

Asante kwa ushauri wako mkuu! Lyagwa.
 
Last edited by a moderator:
All the best, endeleeni kumuomba Mungu ili hatimaye ndoa ifungwe
 
We utakuwa mtunza fedha.. ofa nzuri mkuu.
Aaaaaaaaaaaa nooooooooh. Huko utanipeleka kwa Pilato, naomba Kiti cha hiyo kamati ya DATSE (Dawasco, TBL and Serengeti) aqua.
 
Kila la heri Mkuu katika mapenzi yenu.





Habari wanaJF,
Mda umepita tangu nijitojeze kutafuta rafiki wa kike kupitia hii forum. Bahati nzuri kwangu, naamini nimempata ambaye Mungu aliniandalia. Tumeanza taratibu sana na urafiki wetu unaendelea vizuri sana.

Naamini sana urafiki wetu utaishia kwenye ndoa takatifu. Wale wanaosema hapa hamna, jaribuni tena, ombeni na Mungu atawapa kwa kadri ya mapenzi yake. Asanteni kwa mlionitakia heri.
 
Last edited by a moderator:
sina budi kukupongeza na kukutakia kila la heri, sina shaka na wewe kumpata mke hapa
 
Hongera sana.
Ila kuna wadada waongo asikwambie mtu kuna mmoja nshawah kumpata humu akanambia yeye ni mwanafunz chuo kikuu Aridh mwaka wa tatu et anasoma education!!! Duh nilichoka make mi nipo Udsm na Ardh naijua vizur.
Wadada punguzen uongo!
 
Ungekua umefkia japo ile level ya kuweka pete ya uchumba kidolen kwake ningekuelewa kwa sasa sielewi unashukuria nini coz u still have a long long way to go
 
Ungekua umefkia japo ile level ya kuweka pete ya uchumba kidolen kwake ningekuelewa kwa sasa sielewi unashukuria nini coz u still have a long long way to go

Kila kitu kinaenda step by step, hii ni hatua ya mwanzo. Just stay tuned, I'll keep u posted here in jf
 
Hongera sana ila ushauri wangu kwako take care because life is simple by looking But tough in action.
 
Hongera saaaaaaaaaaaaaaana na naamini Mungu uliyemtegemea ndiye atakayekuwezesha kufikia malengo yako kimaisha. Muishi kwa upendo usio na unafiki na kamwe msiishi maisha ya kitamdhilia....Kuna waliokuambia ni mapema sana kutoa jibu ila naamini umerudi kwetu baada ya kuona kitu katika mwanzo wenu. Nitawakumbuka katika maombi ili mungu awaoteshee mapendo ya dhati daima.
 
Back
Top Bottom