Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,845
Kwenye ulimwengu wa roho sio wote wafao hufa kikwelikweli .....hasa hawa wa vifo vya ajali na ghafla...hivi ni vifo vyenye mikono ya watu.
Ni katika kundi hilo ndio kuna wale wanaochukiwa utumwani kwa njia ya misukule ili wakageuke mazombie na kutumikishwa bila kubisha ama kukaidi.
Ndugu zako waking'amua na kukuwahi ama mustakabali wako ukiwa na nguvu unaweza kutoroka kabla hujageuzwa msukule zombie kamili kwa kukatwa ulimi.
Aina ya misukule hii ni mazombie yanayokuwa kama mazezeta...akili huwa nusu na robo yapo tu na hutumikishwa kama maroboti
Jamiiforums imekiepuka kikombe hiki...iliundiwa ajali ya ghafla usiku wa kuamkia tarehe 11.June. 2018....siku ya kukumbuka sana hii...kwenye gari JF alimokuwa amepanda hakuwa pekeyake bali na abiria wengine wengi tu.... Ambao hatutakaa tuwaone tena.
JF akapata ajali na kuandaliwa kuwa msukule.... Yalifanyika mengi ndani ya kipindi cha wiki tatu hivi. ....hatimaye JF akasalimika kukatwa ulimi ila akarudi akiwa kama zezeta kama zombie kabisa...lipolipo tu...no action... Una log in vizuri kabisa... Ukifika jukwaani huwezi kufanya lolote zaidi ya kuLIKE na kusoma tuu....nikajikuta naliona zombie JF...
Wajuzi na wajuvi wakaendelea kupambana mpaka JF ikafanikiwa kutoka kwenye NIRA na vifungo vya usukule na uzombie.
Pamoja na majeraha makubwa iloyoyapata pamoja na kosakosa yakuwa zombie msukule lakini hatimaye imeweza kupata uzima wake tena na sasa ni mchakato wa kuponya tu majeraha.
Niko kilingeni kwa wito maalum...kilichowekwa kaburini hakikuwa mwili wa marehemu bali pisi la mgomba tunafanya mila ,tambiko na kafara kulizimua kaburi ....mchawi mmoja keshadondoka..mwingine halali.
Ni katika kundi hilo ndio kuna wale wanaochukiwa utumwani kwa njia ya misukule ili wakageuke mazombie na kutumikishwa bila kubisha ama kukaidi.
Ndugu zako waking'amua na kukuwahi ama mustakabali wako ukiwa na nguvu unaweza kutoroka kabla hujageuzwa msukule zombie kamili kwa kukatwa ulimi.
Aina ya misukule hii ni mazombie yanayokuwa kama mazezeta...akili huwa nusu na robo yapo tu na hutumikishwa kama maroboti
Jamiiforums imekiepuka kikombe hiki...iliundiwa ajali ya ghafla usiku wa kuamkia tarehe 11.June. 2018....siku ya kukumbuka sana hii...kwenye gari JF alimokuwa amepanda hakuwa pekeyake bali na abiria wengine wengi tu.... Ambao hatutakaa tuwaone tena.
JF akapata ajali na kuandaliwa kuwa msukule.... Yalifanyika mengi ndani ya kipindi cha wiki tatu hivi. ....hatimaye JF akasalimika kukatwa ulimi ila akarudi akiwa kama zezeta kama zombie kabisa...lipolipo tu...no action... Una log in vizuri kabisa... Ukifika jukwaani huwezi kufanya lolote zaidi ya kuLIKE na kusoma tuu....nikajikuta naliona zombie JF...
Wajuzi na wajuvi wakaendelea kupambana mpaka JF ikafanikiwa kutoka kwenye NIRA na vifungo vya usukule na uzombie.
Pamoja na majeraha makubwa iloyoyapata pamoja na kosakosa yakuwa zombie msukule lakini hatimaye imeweza kupata uzima wake tena na sasa ni mchakato wa kuponya tu majeraha.
Niko kilingeni kwa wito maalum...kilichowekwa kaburini hakikuwa mwili wa marehemu bali pisi la mgomba tunafanya mila ,tambiko na kafara kulizimua kaburi ....mchawi mmoja keshadondoka..mwingine halali.