JF Exclusive: Video/Audio ya Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine (1978)

JokaKuu,
Tunaweza kuyajadili yote haya:
1. "kuonea wananchi katika kampeni dhidi ya 'walioitwa wahujumu uchumi"' Sijui hapa umewalenga 'wananchi' au 'walioitwa wahujumu uchumi'. Natambua 'wahujumu uchumi' nao ni wananchi; lakini wanatambulishwa na sifa yao hiyo ya nyongeza.

2. "Mwalimu Nyerere na Sokoine walishindwa kuendesha uchumi wa nchi."

3." Badala yake wakaanza kulaumu na kusingizia kuwa hali mbaya ya uchumi imesababishwa na wahujumu uchumi na walanguzi" Hapa nitapata fursa ya kujifunza kutoka kwako juu ya ushahidi wa hawa wawili kuzitumia sababu hizi kuwa ndio zilizosababisha anguko la uchumi.

4. Itakuwa ni fursa ya nadra pia kupata nafasi ya kujua heshima anayopata Sokoine imejikita zaidi katika "kutambua mchango wake alipokuwa waziri mkuu wakati wa vita vya Kagera." Bila ya vita hivyo "usingewaelewa wanaomkubali Sokoine".

Yote haya manne tunaweza kuyajadili vizuri tu.
 
Kwa bahati mbaya sana rekodi kama hizi za video hazipatikani kirahisi kutokana na nchi kutokuwa na televisheni ya taifa kwa wakati huo!

Hata hotuba nyingi za Nyerere, mahojiano yake na vyombo vya habari vya ndani na nje, rekodi zake za video hatuna.

Ukitaka kuzipata labda YouTube huko. Na huko YouTube inabidi uwe mjanja jinsi ya kuzipata.

Naamini vyombo vya habari kama BBC, Reuters, AP, n.k, si ajabu vina footage nyingi sana za Nyerere na viongozi wetu wengine wa wakati kuliko hata vyombo vyetu vya habari vya ndani.

It’s a shame.
 
"Treasury reporting rates of exchange as of March 31, 1978"
US Dollar = Tsh. 8.311

Unaweza kuweka time scale ya Sokoine ya kuwa PM first time na second time. Kumbuka alijiuzulu na baadaye kuchaguliwa tena. Then ni kipindi kipi aliruhusu dala dala na tatu kama unakumbuka aliposhambuliwa na kwenda kutibiwa Europe etc.

NB Kama huwezi kuzipata chap chap nitazitafuta.
 
Unaweza kuweka time scale ya Sokoine ya kuwa PM first time na second time. Kumbuka alijiuzulu na baadaye kuchaguliwa tena. Then ni kipindi kipi aliruhusu dala dala na tatu kama unakumbuka aliposhambuliwa na kwenda kutibiwa Europe etc.

NB Kama huwezi kuzipata chap chap nitazitafuta.
Mkuu, mimi sijawahi kusikia habari ya Ndugu Sokoine "...kushambuliwa na kwenda kutibiwa Europe etc." Hii habari ndio naipata toka kwako kwa mara ya kwanza kabisa. Itapendeza kama utaweza kuielezea zaidi.

Ninachojua ni kwamba alikwenda masomoni, baada ya kujiuzuru.

Na kuhusu 'time frame' kama ushahidi wa daladala ya Tanzania kuwa na thamani ya dollar moja ya Kimarekani, hata ungekwenda hadi 1961, hutapata US $ 1 kuwa sawa na Tsh. 5.00
 
Kalamu1,

Hilo la kushambuliwa naweka kapuni siwezi kukwambia maana unatafuta umbeya sasa, na sina muda wa kuweka maelezo wewe fahamu hivyo. Upo wrong nitatafuta hizo info za time scale alipokuwa PM nitaweka humu lakini itachukua muda kidogo sio leo wala kesho. Vilevile nitaweka na viwango vya exchange rates.
 
Mkuu 'Ole' alisema anao uhakika wa anachokiandika kwa asili mia na kumi (110%). Aliposema vile tu, nikajua hajui lolote kuhusu hayo aliyokuwa akiyaandika. Kashindwa tu kuwa muungwana na kukubali kuwa taarifa aliyoiweka haikuwa ya kweli.

Kang'ang'ana atakwenda kutafuta ushahidi, sijui ataupata wapi, huku kuutengeneza hawezi!
 
Sijui kwanini TBC hawajaamua kudigitize collection yao ya videos za mambo mbalimbali ya enzi na enzi...
National Achives ya Video enzi hizo ilikuwa kwenye film rolls ikifanywa na Taasisi ya Vielelezo, Audio-Visual Institute pale ilipo TBC Kijitonyama.
By the time wanaziunganisha kuunda TVT, ile 1998, film rolls ilikuwa tayari fazed out. Hivyo zile digital zote tunazoziona za sherehe za uhuru, ni kwa hisani ya foreign achievers.

Shirika la Habari la China, Xinua linazo lots of our early events katika digital achievers zao na pia Cuba wanazo.

Issue ni TBC kuziomba tuu.
P
 
Hawa walikuwa Wazalendo hasa. Sio hawa wanajiita wazalendo kumbe wapigaji wakubwa.
 
MKJJ hivi inzi wako unawalisha mafuta gani kupata habari hizi tamu tamu? Jamaa huyu alikuwa ni kiongozi first class kupatikana Tanzania bila ya kuwa muasisi. Alipofariki nilikuwa Morogoro wakati huo na ile benzi yake aliyopata nayo ajali ilkaa pale Polisi kwa karibu miezi sita kabla ya kuondolewa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom