JF Exclusive: Hotuba ya Nyerere 1995

JF Exclusive: Hotuba ya Nyerere 1995

"Off the cuff" umejuaje? Umejuaje kwamba hotuba ya Nyerere aliitoa "off the cuff"? Ndo maana nakwambia unajivisha mamlaka ya usemaji wa ofisi ya Marehemu Mwalimu Nyerere. Umejuaje Nyerere alibwabwaja tu "off the cuff"?

Aidha, wanaotoa hati ya hotuba rasmi sio walioisikia uwanjani au kwenye radio kama wewe na mimi. Bali ofisi ya mtoa hotuba, tena mara nyingi kabla ya tukio. Wewe unajivika kilemba ukoka kama mamlaka ya nyaraka za rais mstaafu.

Kizazi kipya unachosema unakiandikia historia watakaposoma hayo yako na wakute rekodi za wengine zikionyesha kuwa Mwanakijiji hakuwa mamlaka ya alichoandika na kukisema Julius Nyerere kwa sababu anaongeza chumvi zake.

Hakuna sababu ya kulaumiana. Huyo aliyetoa hii hotuba ni bora zaidi kuliko kutokuwa nayo. Hii iliyohaliliwa bado ina nguvu ya kuamsha hamasa ya ukombozi mpya wa Tanzania yetu. Kama wewe unayo isiyohaliliwa weka hapa tusome. Kama kuna neno limeongezwa hapo ambalo limepotosha mawazo ya Nyerere liseme tukusikie na sisi tutakuunga mkono ili lirekebishwe.

Mawazo ya Mwalimu bado yana nguvu inayogusa moyo na akili ya kila mtu mwenye moyo wa ufahamu. Wasomi, Wachungaji na Mashe, Wanajeshi na Wafanya biashara, wakulima na wafugaji...wote wameendelea kuguswa na hotuba za Nyerere. Nyerere alikuwa amejitoa mhanga kuongoza nchi hii, alijitoa kutafuta majibu ya matatizo ya nchi yetu. Aliipenda nchi na watu wake wote. Ndio maana tunaomfahamu bado tunamkubali na kumheshimu kama binadamu aliyejitahidi kutumikia watu wake kwa nguvu zake zote.

Sasa ninaomba tuwe tunatoa hitimisho la mambo tunayojadili ili kama siku ingine yakirudi kujadiliwa, yaanzie kwenye hitimisho. Kwa mfano Je tunapokuwa na raisi aliyenunuliwa na anatumia ikulu kulipa fadhira au madeni ya wafadhiri wake je tufanyeje? Je tukubali kutembea naye kama mkristo anavyotembea na msalaba shingoni? Mfano mwingine ni mashirika ya umma yanayofanya vizuri kisha yakauzwa au yakaandaliwa mazingira ya kuuzwa, je tunawezaje kurekebisha tatizo hio? Nk.
 

"Off the cuff" umejuaje? Umejuaje kwamba hotuba ya Nyerere aliitoa "off the cuff"? Ndo maana nakwambia unajivisha mamlaka ya usemaji wa ofisi ya Marehemu Mwalimu Nyerere. Umejuaje Nyerere alibwabwaja tu "off the cuff"?

Aidha, wanaotoa hati ya hotuba rasmi sio walioisikia uwanjani au kwenye radio kama wewe na mimi. Bali ofisi ya mtoa hotuba, tena mara nyingi kabla ya tukio. Wewe unajivika kilemba ukoka kama mamlaka ya nyaraka za rais mstaafu.

Kizazi kipya unachosema unakiandikia historia watakaposoma hayo yako na wakute rekodi za wengine zikionyesha kuwa Mwanakijiji hakuwa mamlaka ya alichoandika na kukisema Julius Nyerere kwa sababu anaongeza chumvi zake.


Tindikali, What is this all about? Waliokuwa wanamfahamu Mwalimu na kufuatilia kwa makini utendaji wake kazi wanaelewa na watakueleza wazi kwamba Mwalimu alikuwa na akili kama mchwa zilizokuwa zikimuwezesha kuhutubia bila kutumia maandishi na message ikafika with a bang! Kama ulikuwa mfuatiliaji mmojawapo basi bila shaka ungekuwa umegundua kwamba Mwalimu alikuwa akitoa hotuba zake nyingi za Kiswahili "off the cuff" zilikuwa hazitayarishwi kwenye makaratasi prior to the event, alikuwa akizitayarisha mwenyewe kwenye kichwa chake, alijua anataka kusema nini na ndio maana wakati mwingine haziendi kwa mtiririko unaoweza kuwepo kwenye makaratasi ambayo yeye mwenyewe ama wasaidizi wake wangeliweza kuyapitia na kuwa editted kabla ya kutolewa. Hotuba zilizokuwa zikitayarishwa kwenye makaratasi ni zile ambazo zilikuwa zikitolewa kwenye mikutano maalum ya Chama na Serikali. Halikadhalika, hotuba alizokuwa akizitoa kwa lugha ya Kiingereza ndizo ambazo ziko pia kwenye makaratasi.

Kwa taarifa yako, hotuba aliyobandika hapa Mwanakijiji iliweza kuwekwa kwenye makaratasi kutoka kwenye audio tapes zilizochukuliwa siku ile ya Mei Mosi. Kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa hotuba za Mwalimu Nyerere bila shaka utajua kwamba Taasisi ya Mwalimu Nyerere iliwahi kutoa hotuba hiyo kwenye kijitabu cha "Tunatoka Wapi, Tuko Wapi na Tunakwenda Wapi" kama alivyodokeza Mwanakijiji at one point. Kwa mtindo huo huo, Taasisi iliwahi pia kutoa kijitabu kinachoitwa "Nyufa" chenye maelezo ya Mazungumzo ya Mwalimu Nyerere kwenye Klabu ya Waandishi wa Habari nchini kwenye Hoteli ya Kilimanjaro (Kempiski) Machi 13, 1995. Sioni mantiki yoyote ya mtu yeyote kukatazwa kujadili kuhusu maneno yenye manufaa kwa Taifa letu aliyowahi kutoa Baba wa Taifa katika uhai wake. Hivi yale tunayoyasikia kwenye vipindi vya "wOSIA WA BABA" ina maana tukishayasikia basi tuyaache jinsi yalivyo tusiyajadili? Kuna maana gani basi ya kuwekewa vipindi kama hivyo?

Mimi sidnani, ila naamini kabisa kwamba Mwalimu angelikuwa hai leo angelifurahi sana kuona watu wanabandika hapa machapisho yake ili yasomwe na yajadiliwe ipasavyo with or without his consent, mradi tu hayatumiki kumvunjia heshima au kupotosha ukweli.
 
Nyerere wa sbright thsn normal tz leaderz. Wanamuenzi kwa stail ya kishenzi sana
 
Hotuba hii inahitaji kusomwa na watu wengi ili waweze kujua CCJ inaelekea wapi...
 
Mwanakijiji yasikukatishe tamaa haya..natamani sana kupata hotuba zaidi za Mwalimu...najua nyingi zinawakera wana CCM wa sasa zinawakosoa na kuwaumbua mno. Mwalimu Tutakukumbuka Daima.

AK-47 kama uko Tanzania, sikiliza TBC Taifa kila siku saa mbili na Robo usiku na saa 11 kamili alfajiri.
 
Wakati kampeni za Agustine Mrema za mwaka 1995 zikiwa zimepamba moto na akiwa mikoa ya kusini, raia wenye furaha walimbeba kuonyesha kufurahishwa na somo alilowapa.

Hiki kilikuwa ni kipindi kigumu kwa CCM na uwezekano wa NCCR-MAGEUZI kuchukua nchi ulikuwa ni mkubwa lakini Baba wa Taifa aliwanusuru CCM pale alipowaambia.........."Ushauri wangu kwa serikali ya CCM waacheni na msiwabughudhi wapinzani."

Ushauri huu uliwafanya CCM kuacha kutumia nguvu ya dola kuzima kasi ya nguvu ya raia wenye shauku ya mabadiliko.

Leo Nyerere hatuko naye na CCM imesahau wosia huu mzito na huko Mwanza raia wasio na hatia wamebughudhiwa na mabomu ya machozi kwa kisa cha kutaka kuhudhuria mkutano wa Raisi Mtarajiwa Dr. Slaa.

Hili ni kosa kubwa CCM wamelitenda kwa sababu mbali ya ukweli kuwa kila rafu CCM wanacheza hivi sasa inaendelea kumjenga Dr. Slaa na Chadema lakini JK inabidi aende Mkoani Mwanza na kuwaomba msamaha wakaazi wa mji huo kwa kudhalilishwa na jeshi la polisi. Na JK anapaswa kuliagiza jeshi la polisi liache mara moja kubughudhi wananchi kwa nguvu za ziada na ambazo siyo za lazima hata kidogo.

CCM wakumbuke kuwa siyo wote wanaoenda kwenye mikutano ya upinzani watawapigia kura hao wapinzani. Wako wengine humo ni CCM damu pia. Sasa unapowapiga mabomu ujue vile vile unapoteza hata zile kura za wanachama na mashabiki wako. Hii hasara ya nini? Kheri ushindwe uchaguzi kwa heshima badala ya kujidhalilisha ya kuja kujulikana na raia sote kuwa kumbe ulikuwa mtu mwenye uchu wa madaraka.....

Swali jingine JK angelijiuliza hivi ingelikuwa mimi nina mgongano wa viwanja vya kufanya kampeni hapo Mwanza wahudhuriaji kwenye mkutano wangu wangelipigwa mabomu hayo?

Jibu hapo acha nimsaidie JK kuwa ni HAPANA......Sasa JK wasubiri nini kuomba msamaha kwa makosa ya askari walio chini ya uangalizi wako...Au unatudharau?


 
Mkuu Mwalimu Julius Nyerere hakuwa kioo cha demokrasia ila atakumbukwa kama kinara wa ukombozi kuondoa wakoloni weupe na kuleta wakoloni weusi. Alidumaza Demokrasia baada ya kufuta mvumo wa vyama vingi,matatizo ya CCM leo chimbuko ni Mwalimu.Misingi ya demokrasia tulipopata uhuru ilikuwa wazi ya ushindani,mimi nilikuwa mdogo lakini nakumbuka ule wimbo wa Union Jack ipepee kwao kisiwani Uingereza wakiimba wananchi wa TANU na CONGRESS wote nia ilikuwa kujitawala kuwa uhuru.Bila ushindani hakuna Demokrasia.
 
Nimejaribu kuweka Video imeshindika lakini Nyere anasema katika Hotuba yake na waandishi wa habari 1995 kuwa tunahitaji viongozi wanaoongoka kwa utawala wa sheria na Katiba so hakuna sababu ya watu kutamba that they are unpredictable in 21st Century.
 
Nimejaribu kuweka Video imeshindika lakini Nyere anasema katika Hotuba yake na waandishi wa habari 1995 kuwa tunahitaji viongozi wanaoongoka kwa utawala wa sheria na Katiba so hakuna sababu ya watu kutamba that they are unpredictable in 21st Century.
Tuambie tukusaidie hiyo sehemu yenyewe unayotaka kuiweka iko kwenye part no. ngapi maana video ina part 1-10.
 
Part 1



Part 2



Part 3




Part 4




Part 5



Part 6




Part 7


 
Last edited by a moderator:
I remember that day,

Nilitoka home mpaka Airport kwa miguu nikienda kumpokea Mwalimu tena nilikua Kifua wazi enzi hizo nilikua mdogo sana.

Sintokaa na kuisahau hiyo siku.

Viva Julius
 
Kweli tutakukumbuka sana JK Nyerere
ulikuwa muwazi sana katika kila kitu

Leo tunaambiwa serikali yetu haiwezi kuongelea mambo ya Libya?
sio siri inaumma sana, Utaifa wetu na ujasiri tuliokuwa nao wakati wa nyerere wote umekwisha kabisa
 
Hiki kichwa kilikuwa balaa!

Ni kweli yani ukisikiliza kwa makini utaona jinsi aliovyo kuwa na
uwezo mkubwa wa kuelewa mambo.

Kuna baadhi ya watu wanaosema eti sababu ya kuonekana anaakili
sana ni kwasababu wengi wakati wa utawala wake walikuwa
hawajasoma. Lakini nikimsikiliza vizuri naona sikweli, huyu mzee
alikuwa anaakili sana. Hata sasa japo tunawasomi wengi bado
uwezo wake ulikuwa mkubwa sana kulinganisha na wasomi wengi
tulionao sasa.
 
Hapa chini nimeweka vipande vya hotuba ya Mwl. Nyerere (The late, great) aliyo itoa siku ya wafanyakazi mwaka 1995. Naipenda hii hotuba kwa sababu alizungumzia karibia kila kitu kuhusu taifa letu na mengi aliyo yaonya tuna yaona leo. Kweli asie sikia la mkuu.....













 
Last edited by a moderator:
Alizungumizia haki za wafanyakazi, ufisadi, vyama vya siasa, wagombea binafsi nk. Yani hii ni moja ya hotuba zake zilizo gusa karibia kila nyanja.
 
Aligusia katika kila nyanja! Je katika soka na hati miliki za wanamuziki alisema nini?
 
Back
Top Bottom