Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Ifuatayo ni hotuba muhimu ambayo kila Mtanzania anapaswa kuisoma kwani ni mojawapo ya lulu za fikra zinazotudokeza taifa letu tumefikaje hapa na ni miongoni mwa hotuba ambazo Nyerere hakusita kukubali kuwa kuna mahali chini ya uongozi wake walikosea (kinyume na imani ya watu kwamba Nyerere hajawahi kukubali makosa).
Hotuba hii vile vile ni muhimu sana wakati huu ambapo Wafanyakazi nchini wanajiandaa kugoma na inaweza kutumika kabisa kama kichocheo cha mgomo huo. Ikumbukwe kuwa ilikuwa ni mara ya kwanza vyama vya wafanyakazi vilimkaribisha mtu ambaye si Rais kuwa mgeni rasmi mzungumzaji katika sherehe hizo.
Sehemu ya sauti imenisumbua kidogo kwani original file yangu nilishadelete inabidi nihamishe kutoka kwenye CD niliyotengeneza 2007!! so for now enjoy hii ya maandishi.
Nimegawa katika sehemu sita kutokana na maudhui yake.
Sura ya 1 - Inahusu wafanyakazi zaidi na haja ya kushikimana kudai haki zao. Ikumbukwe kuwa 1994 wafanyakazi waligoma na wakati ule walimuomba Mwalimu awe mgeni rasmi akawakatalia lakini 1995 alikubali.
Sura ya 2 - Anazungumzia hali tulipotoka, hasa katika masuala ya kiuchumi ili kuweza kuelewa tulipofika wakati ule. Kauli mbiu yake ni "Tumetoka wapi, tupo wapi, na tunakwenda wapi"? Ndio mbiu anayoirudia katika hotuba nzima.
Sura ya 3 - Baadhi ya Matunda ya Azimio la Arusha. Hapa anajaribu kuelezea baadhi ya matunda ya Azimio la Arusha hasa akijaribu kuonesha kuwa maamuzi ya Zanzibar yaliyobadili Azimio la Arusha yalibadili kitu cha msingi sana.
Sura ya 4 - Makosa ya Ubinafsishaji. Nyerere anajenga hoja ya msingi kuwa ubinafsishaji uliokuwa umeanza kufanywa ulikuwa kinyume na sera ya CCM.
Sura ya 5 - Tunakwenda wapi na sifa za viongozi tunaowataka. Anapofika hapa Nyerere anaendelea mbele kidogo kutokana na kile alichokisema Kilimanjaro alipotoa orodha ya sifa za viongozi tunaowataka. Kwa mwaka huu wa uchaguzi, sehemu hii ni muhimu kuisoma kabla hatujaamua kumuunga mkono mgombea yoyote wa nafasi yoyote.
Sura ya 6 - Sehemu hii ya mwisho Mwalimu anafanya utetezi wake wa kifalsafa wa wagombea binafsi na anaelezea kwanini serikali ilifanya makosa kufuta haki ya mwananchi kuchaguliwa kwa sababu inakera. Ni muhimu tunapoelekea kusikia uamuzi wa mahakama ya Rufaa kuhusu suala la mgombea binafsi.
HOTUBA KAMILI - Mwishoni hapo nimeweka hotuba kamili. Kwa hiyo una uchaguzi wa kuchukua sehemu sehemu au kudownload hotuba kamili ilivyo.
Attachments
-
Sura2TUMETOKA WAPI.doc36.5 KB · Views: 717
-
Sura4MakosayaUbinafsishaji.doc53.5 KB · Views: 562
-
Sura5TUNAKWENDA WAPI.doc43 KB · Views: 447
-
Sura1MWANZO.doc41.5 KB · Views: 429
-
sura3BAADHI YA MATUNDA YA AZIMIO LA ARUSHA.doc29.5 KB · Views: 447
-
Sura6HOJA YA WAGOMBEA BINAFSI.doc38.5 KB · Views: 469
-
nyerere1.jpg10.1 KB · Views: 767
-
Hotuba ya Mwalimu Mei Mosi 1995 TUMETOKA WAPI.doc115 KB · Views: 719