JF Exclusive: Hotuba ya Nyerere 1995

Kuna vimaneno huwa vinasemwa semwa kuwa mzee was removed ili watu wamalize mambo yao!!
 
Nimeisikiliza hotuba ya mwl Jk kwa makini sana na kulinganisha hali na mwelekeo wa nchi yetu tanzania inakoelekea kwa sasa imenigusa sana kwani inamajibu ya matokeo ya kinachoendelea hasa kwenye swala la katiba, uongozi, na ubaguzi katika nyanja zote za ukabila, dini, na asili ya mtu Hii dhambi Itatutafuna..inamaana viongozi, wantanzania hatulioni hili, tafafhali msikilize mwl pia toa maoni juu ya mstakabali na mwelekeo wa taifa la Tanzania kwa manufaa ya wote..Watch "Nyerere Speech 1995" on YouTube - Nyerere Speech 1995:

http://youtu.be/jE7oTPXtpas
 
Tazama clip kwa umakini sana, kinachosikitisha ni miaka 20 sasa na hali inazidi kuwa mbaya.

Je ni kweli waTanzania hususani vijana tumekuwa wapumbavu kiasi cha kushindwa kujua mambo muhimu ya msingi ya nchi hii mbadala na majina ya watu waliotangaza nia ya uraisi wa awamu ya tano?

Tunashindwaje kuwauliza maswali magumu au kuwachuja kutokana na vitendo vyao walivyofanya kwenye historia za uongozi wao?

Ushabiki wa nyama tuweke pembeni tutachangie kama waTanzania wenye uzalendo wa kweli na taifa hili


 
Last edited by a moderator:
Huko mbele tutajieleza kwa nini tunasikiliza ujumbe mzuri kama huu halafu tunaacha upite tu masikioni bila ya kuutendea haki.
Hakika tutalipa tena ghali sana!
 
Huko mbele tutajieleza kwa nini tunasikiliza ujumbe mzuri kama huu halafu tunaacha upite tu masikioni bila ya kuutendea haki.
Hakika tutalipa tena ghali sana!

Siyo ujumbe mzuri tu,ni msingi mzima wa kupata maendeleo kwa taifa lolote lile lenye kujitambua.

Kikuu, ni idadi kubwa ya kuleta maendeleo inalenga vijana kwa taifa hili lakini ndiyo wamekuwa wakwanza kushabikia mambo ya kipumbavu yasiyo na manufaa kwao au kwa taifa hili. Inasikitisha sana
 
Kwa nini hotuba ya mwaka 1985 ya kuwaaga wazee wa Dar es Salaam pale Diamond Jubilee inafichwa. Hiyo ndiyo hotuba bora ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
 
Kwa nini hotuba ya mwaka 1985 ya kuwaaga wazee wa Dar es Salaam pale Diamond Jubilee inafichwa. Hiyo ndiyo hotuba bora ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Ndio ile ya IKULU kuna biashara gani tuwekee mkuu
 
Siyo hiyo mkuu, ya mwaka 1985 anawaaga Watanzania anang'atuka anamuachia nchi Mwinyi.
Hatari ya kufarakana baada ya Nyerere
Misingi ya umoja iliwekwa na wazee
Waliepuka chuki za kidini, kikabila
Walikuwa wakarimu, wastaarabu

"NAWAELEZENI haya wazee kwa sababu huko tulikotoka, tulikotoka pamoja na wazee, wazee wa nchi tulishikamana sana".
Hiyo ni sehemu ya hotuba ya Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyoitoa jioni ya Jumamosi Novemba 2, 1985 katika ukumbi wa Diamond Jubilee wakati akiwaaga wazee wa Dar es Salaam baada ya kung'atuka wadhifa wa Urais.
Tangu kufariki dunia Mwalimu Julius Nyerere baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiirudia mara kwa mara hotuba hiyo kama wasia wa mwasisi huyo kwa Watanzania.
Kwa upande mwingine watu kadhaa waliopata fursa ya kusikiliza hotuba hiyo wamekuwa wakitoa maelezo yanayolenga kuonesha hekima na busara aliyokunayo Hayati Mwalimu Nyerere.
"Mwalimu alikuwa na hekima kubwa ndiyo maana aliweza kuishi na watu wa aina zote", amedai Afisa mmoja Mwandamizi wa chombo kikongwe cha habari nchini.
Aidha, Mwanadiplomasia mmoja alidai kuwa hotuba hiyo ni mojawapo ya hotuba nzito alizowahi kutoa Mwalimu Nyerere.
Uchunguzi wa gazeti hili umeonesha wananchi wengi wamekuwa na hisia tofauti kinyume na vile ambavyo mkondo wa historia unavyotaka kuelekezwa.
Uchunguzi huo pia umegundua wasiwasi walionao wananchi juu ya unakoelekezwa mkondo wa historia hasa mara baada ya kifo cha Mwalimu Nyerere.
Makundi ya watu yamekuwa yakiujadili ukarimu na bashasha za wazee wa Dar es Salaam kumpokea kijana mdogo wanayetofautiana naye kidini ambao historia hiyo inajaribu kuufunika.
"Nani angestahili kupongezwa zaidi hivi sasa yule mkaribishaji au aliyekaribishwa?" Amehoji Mzee Rashid Mohammed mkazi wa Ubungo katika maongezi ya moja ya vikao vya mitaani vinavyojaribu kutafakari hali ya baadaye ya Tanzania.
Aidha, Bwana Sadiki wa Mwanyamala amehadharisha kuwa vyombo husika kujaribu kupotosha ukweli huku vikiimiza amani na mshikamano wa kitaifa ni kuitumbukiza nchi kusikofaa.
AN-NUUR pia ilibahatika kuongea na baadhi ya wananchi katika soko la Kariakoo ambao nao kama wananchi wengine walikuwa na maoni yao ambapo wengi wameshauri kujengwa kwa mahusiano ya kijamii kwa njia ya haki, ukweli na uadilifu badala ya propaganda na vitisho.
Muafaka huo umeelezwa kuwa ndio utakaodumisha amani na utulivu nchini.
"Watu wa dini zote watazamwe kwa muono sawia, malalamiko yapokelewe kwa uzito unaostahiki na yashughulikiwe", amesisitiza Amiri wa Maimamu Sheikh Juma Mbukuzi wakati akiongea na Waislamu Msikiti wa Kibo jijini Dar es Salaam.
Naye Katibu wa Kamati ya Kutetea Haki za Waislamu Sheikh Issa Ponda aliliambia AN-NUUR kwa njia ya simu kuwa Hayati Mwalimu Nyerere aenziwe sambamba na wale alioshirikiana nao katika harakati za kudai uhuru.
"Alichokisema Mwalimu katika hotuba yake ni kile ambacho Waislamu wamekuwa wakikikumbushia mara zote wanapolalamikia kunyongeshwa kwao kulinganisha na mchango mkubwa walioutoa katika kudai uhuru wa nchi yetu". amesema Sheikh Ponda.
Mwalimu Julius Nyerere ambaye kesho anazikwa kijijini kwake Butiama alizaliwa miaka 77 iliyopita ambapo baada ya masomo yake ndani na nje ya nchi alijiunga na harakati za kudai uhuru wa Tanganyika mnamo mwaka 1952.
Chama kilichokuwepo wakati huo ni Tanganyika African Association (TAA) kilichokuwa kikiongozwa na marehemu Abdulwahid Sykes.
Pamoja naye walikuwepo wazee kadhaa wa maeneo ya Gerezani, Kariakoo na Kisutu.
Miongoni mwa wazee hao ni pamoja na Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Suleiman Takadir, Sheikh Haidar Mwinyimvua na Mzee Jumbe Mohammed Tambaza.
Wengine ni Mzee Mshume Kiyate, Mwinyijuma Mwinyikambi, Mzee Idd Faiz Mafongo, Idd Tosir, Sheikh Mohamed Ramia na wengineo.
Hayati Nyerere alichaguliwa kuwa Rais wa TAA mnamo mwaka 1953.
Mnamo mwaka 1954 TAA iligeuzwa kuwa TANU chama ambacho kilikuja kunyakuwa uhuru wa Tanganyika mwaka 1961.
Kwa mujibu hotuba ya Mwalimu kwa wazee wa Dar es Salaam mwaka 1985, jina la TANU lilipendekezwa na marehemu Abdulwahid Sykes.
 
Kama anakubali yeye alivurunda basi anapoteza haki ya kuwa mkufunzi, lecturer, mkosoaji wa mambo ambayo yeye yalimshinda, anafundisha ambayo hakuweza kuya practice. Siasa hizo ni unafik.

Sasa anamkosoa nani kama yeye yalimshinda haya ya kujitegemea? Hakuwa mkweli hata kidogo.

Kama unaelewa Uprofesa unapatikana vipi?
Basi hupati shida kumwelewa Nyerere.

 
Kwa nini hotuba ya mwaka 1985 ya kuwaaga wazee wa Dar es Salaam pale Diamond Jubilee inafichwa. Hiyo ndiyo hotuba bora ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Nadhani Mzee Mwanakijiji kwa uzoefu wake au Invisible wanaweza kusaidia.Tunapoelekea Uchaguzi Oct.2015 kujikumbua hotuba za JK Nyerere ni jambo njema hasa kwa mpiga kura. Vyama vyetu wanafaa kuliona hilo kwa afya ya Nchi yetu.


Ni jambo liliowazi CCM kwa sasa hotuba kama hiyo kusikilizwa na Wajumbe wa Mkuutano Mkuu ni sawa kumuomba Padre ahubiri Msikitini au Sheihk kuhubiri Kanisani.

 
Last edited by a moderator:
Shukrani sana kwa mtoa mada. Kama unazo na nyingine hata za miaka ya nyuma sana sio vibaya ukatuwekea hapa pia.
 
Tazama clip kwa umakini sana, kinachosikitisha ni miaka 20 sasa na hali inazidi kuwa mbaya.

Je ni kweli waTanzania hususani vijana tumekuwa wapumbavu kiasi cha kushindwa kujua mambo muhimu ya msingi ya nchi hii mbadala na majina ya watu waliotangaza nia ya uraisi wa awamu ya tano?

Tunashindwaje kuwauliza maswali magumu au kuwachuja kutokana na vitendo vyao walivyofanya kwenye historia za uongozi wao?

Ushabiki wa nyama tuweke pembeni tutachangie kama waTanzania wenye uzalendo wa kweli na taifa hili




Jamani kama kuna watu wanafahamiana vizuri na wakuu wa vyombo vya habari (-TBCcm) washawisheni hii clip ichezwe kila siku kila baada ya taarifa ya habari (kama ile zamani MAZUNGUMZO BAADA YA HABARI). Huu ni mhadhara kamailifu wa elimu ya uraia kwa Watanzania. Redio za mikoani, eneza uzalendo (simaanishi yale maigizo ya ACT) katika maana halisi ya dhana 'uzalendo'.
 
Last edited by a moderator:
Nilikuwa najiuliza sana kwanini hotuba nyingi za baba wa taifa ni ngumu kuzipata ni kama zimefichwa na RTD?

Nikaja gundua ni amri ya serikali kwa kuwa maadili yao yanakinzana na hayaendani na msimamo wa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Kuna hotuba hata maktaba ya Mwalimu Nyerere kule kijijini hawana naishangaa sana hii nchi.

Kwanini hakuna hata kiongozi mmoja au taasisi zikashinikiza hotuba hizi ziwe hadharani?
 
Back
Top Bottom