JF Exclusive: CAG Report on IPTL/Tegeta Escrow Account

JF Exclusive: CAG Report on IPTL/Tegeta Escrow Account

Miaka ya 90's EU na IMF waliupinga sana mkataba wa IPTL wakisema wazi ni mzigo usio wa lazima kwa uchumi wetu mdogo.
Canada ikajitolea gharama dola mil 200 za mradi wa Songas badala ya iptl,wakubwa bado wakang'ang'ana na iptl,yaani mtu anakataa hadi msaada na kulazimisha mkataba ghali kama iptl!
Walipobanwa sana,wakasema miradi yote miwili songas na iptl iende pamoja!
Washauri wa Tanesco wakati huo,Hunton and Williams wakaeleza wazi kuwa mkataba wa iptl haufai kwa kuwa;
-ni wa kipindi kirefu wakati tatizo lilikuwa la kipindi kifupi.
-ulikuwa na gharama kubwa zisizo na sababu.
-ulizidi mahitaji ya umeme na hivyo watumiaji na walipa kodi wangelipia gharama kubwa kuzalisha umeme wasioutumia.
-mkataba uliwapendelea mno iptl
-hakukuwa na ukomo wa muda wa kukamilisha ujenzi hivyo Tanesco kulipishwa gharama kubwa kutokana na ujenzi kuwa prolonged.Gharama zilipaswa kujadiliwa baada ya ujenzi kukamilika.

Nikipitia ushauri huu wa Hunton and Williams,na kwa kuzingatia mazingira ya kifisadi ya nchi yetu,naanza kupatwa na mashaka kama kweli matatizo ya umeme tuliyo nayo yalipaswa kuwa makubwa hivi.
Napata mashaka hata na data tunazopewa kama zina ukweli,hasa kwenye ukubwa wa tatizo,je,ni kweli mahitaji ya umeme au consuption ya umeme ya gridi nzima tunayoambiwa ni ya kweli au imezidishwa ili kuonyesha demand kubwa na hivyo kuhalalisha supply kubwa ambayo mafisadi ndimo wamewekeza?

Napata mashaka kuwa huenda tunao watu wenye ujasiri wa kufikiria kuhujumu mitambo na shirika la Tanesco ili lipate shida ambayo haikuwepo au ilikuwa ndogo na kulikuwa na alternative za kuitatua zenye gharama nafuu,lakini kwa kuwa hazikutoa maslahi kwa certain individuals,zikapigwa chini,tatizo likakuzwa na kuhakikisha linakuwa la muda mrefu ili watu wapige hela,na hivi ndivyo mashirika yetu mengi ya umma yalikufa,hata TTCL nakumbuka ilikuwa inajiendesha kwa faida kubwa,ghafla ikahujumiwa,tukaambiwa inajiendesha kwa hasara,ibinafsishwe.

Wakuu mnaukumbuka ule mgomo wa staff wa Tanesco wakipinga ubinafsishaji na kusema madai ya serikali kuwa Tanesco inajiendesha kwa hasara yalikuwa uongo mtupu?wakaishia kuzunguukwa na FFU!
Mnakumbuka net group solution ilivyokuja kuivuruga Tanesco zaidi?

1997 hazina ilikataa kutoa ushuru wa mafuta ya kuendesha mitambo ya Tanesco,lakini hazina hiyo hiyo ikatoa msamaha kwa wafanyabiashara waagizaji mafuta nje,matokeo yake mgao wa umeme ukafuatia baada ya Tanesco kushindwa gharama za ununuzi mafuta mazito kwa ajili ya mitambo ya iptl.

Hizi zote ni coicidence?
Inaogopesha sana kugundua tunao watz wenzetu wenye roho mbaya hivi,inatisha na kuondoa kuaminiana,na kutoaminiana kukikomaa,huzaa matabaka na makundi,mwishowe civil wars,kila mtu akitaka achukue chake.

Bunge hili litambue Tanzania kwanza,kabla ya vyama na maslahi binafsi.
Shughulikieni hao wezi bila huruma.

juve2012 Very good analysis. Jf ni hazina!
 
Last edited by a moderator:
Inasemekanika kuna kurasa zaidi ya hizo na ndizo zilizo na nani kamegewa kiasi gani kutoka kwa nani...

Sasa wewe unashangaa wakati kamati yote PAC wanayo hiyo ripoti, zipo, lakini hazina mshiko ndiyo maana huzioni humu.
 
Wakuu hivi katika taratibu za serikali ni spending authorization ya kuanzia sh. ngapi inahitaji waziri mkuu au raisi ahusishwe? Na je wana-authorize kwa signature ya mkono au digital. Au kwa mdomo? Ikumbukwe kuwa ni ktk makampuni utaratibu upo namna hiyo, kwamba kuna kiwango kikifika lazima CEO ahusishwe na asign. hili huwa halidhaniwi, halihisiwi ni utaratibu na lazima ufuatwe.

Ukisoma hii paragraph:

rj12qf.jpg


Ni kama vile wahusika wanarespond kwa hisia na si kanuni.

Nauliza haya maana naona tunarudi kule kule 2006 - 2008, JK ataibuka na kuonekana yeye ndiye mwenye busara and a big brother in the room.
 
Kinachotakiwa kwa sasa nikufungua hilo pandora box ili hili suala lijadiliwe kwa uwazi katika msingiambao wale wanaolijadili wanakuwa wako well informed.

Unaposema Ikulu ipo una maana gani?.

Kama maana yako ni Rais wa nchi basi hata maamuzi yanayofanywa na Mkuu wawilaya niya Ikulu, kwa maana kuwa, wakuu wa wilaya wanafanya kazi kwa niaba yaRais wa nchi.

Kuvulunda kwa Mkuu wa Wilaya katika utendaji kazi wake huambatana nakuwajibishwa huyo Mkuu wa Wilaya na siyo Rais wa nchi pamoja na kwamba Mkuu waWilaya alikuwa anafanya kazi zake kwa niaba ya Rais!.

Suala la msingi hapa, Rais yupo moja kwa moja katika context ipi kulingana nadocuments zenye viambatanisho ambavyo vilivyowekwa hapo juu?.

Kama kuna documents zingine, hilo ni suala lingine lakini kwa sasa tunajaribukujenga hoja kulingana na documents ambazo ziko hapa mezani.
Ikulu imo,kwa maana kuwa iwe malipo ni halali na hakuna tatizo au lipo tatizo, Ikulu imeonekana katika taarifa ikishauri malipo yafanywe.

Kuna kifungu kinasema,waziri wa fedha apewe fursa kuijulisha ofisi ya waziri mkuu na rais kama malipohayo yanafaa kuidhinishwa.


Kwamba rais yupo moja kwa moja, hilo ni swali, lakinilazima tujiulize, katibu wa rais anapotoa maelekezo, je anafanya hivyo kwamaelekezo ya nani.

Kumbuka katibu wa rais hana mtu mwingine katikati baina yakena rais, na ndio maana anaitwa katibu wa rais.


Sasa sijui kwamba katibu wa rais anawajibika kwa katibu mkuu kiongozi au anawajibika kwa nani.
Hilo ndilo swali weledi watujuze.Tunachojua katibu wa Rais kahusika


Pili, mkuu wa wilaya anawajibika kwa waziri mkuu na mkuu wa mkoa.
Makosa yake yanapitia kwa wakuu wengine kabla ya kufikia Ikulu, nakutoa nafasi ya Ikulu kuwa mbali na makosa yake


Kwa document zilizopo mezani, aliyesaini maidhinisho nikatibu wa Rais. Sasa sijui anawajibika kwa nani.
Sina uhakika. Labda utusaidiekatibu wa rais anaweza kufanya maamuzi bila kumshirikisha bosi wake? Hilosijui.


 
Wakuu hivi katika taratibu za serikali ni spending authorization ya kuanzia sh. ngapi inahitaji waziri mkuu au raisi ahusishwe? Na je wana-authorize kwa signature ya mkono au digital. Au kwa mdomo? Ikumbukwe kuwa ni ktk makampuni utaratibu upo namna hiyo, kwamba kuna kiwango kikifika lazima CEO ahusishwe na asign. hili huwa halidhaniwi, halihisiwi ni utaratibu na lazima ufuatwe.

Ukisoma hii paragraph:

rj12qf.jpg


Ni kama vile wahusika wanarespond kwa hisia na si kanuni.

Nauliza haya maana naona tunarudi kule kule 2006 - 2008, JK ataibuka na kuonekana yeye ndiye mwenye busara and a big brother in the room.
Una hoja nzito! nimeziona
 
Mpiganaji, hongera sana mkuu na Mungu akulinde dhidi ya haya majamabzi kwani yanahaha hata kutoa roho za watu yapo tayari.
 
Back
Top Bottom