JF Exclusive: CAG Report on IPTL/Tegeta Escrow Account

JF Exclusive: CAG Report on IPTL/Tegeta Escrow Account

te!



Wakuu,

Dodoma kumekucha. Naomba kwa ufupi niwafahamishe kinachojiri maeneo haya (nimepiga kambi huku).

MOSI:
Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond, Edward Lowassa anataka PM Pinda atoke kwa sababu mbili, moja ili njia ya kupata Urais iwe nyeupe lakini pili ili asiwe PM peke yake aliyewahi kujiuzulu kwa tuhuma za rushwa. Watu wake Edward wanahangaika sana kushawishi watu ili azma hii itimie.

PILI:
Membe naye anataka PM ang'oke kwa sababu kuu mbili, moja ili njia ya Urais iwe rahisi lakini pia kwa matumaini kwamba anaweza kupata yeye uPM japo kwa muda tu ili nyota ing'are zaidi.

TATU:
Wassira naye anatakaPinda aanguke ili njia iwe rahisi lakini pia kwa matumaini kwamba anaweza kupata yeye uPM.
Mwandosya naye anataka PM adondoke kwa matumaini ya kupata uPM kutokana na utu uzima.

Sitta naye vivyo hivyo.

NNE:
Mawaziri walioondolewa huko nyuma wakiongozwa na Kagasheki, Nchimbi na Maige nao wanaomba Serikali idondoke kwa sababu wanaamini Pinda aliwatosa ili apone yeye na sasa wanataka na yeye awajibike kwa udhaifu wake. Yupo mtu kama Mwigulu ambaye anautaka Uwaziri kamili kwa udi na uvumba na anataka Serikali ianguke ili Baraza la Mawaziri lisukwe upya awe Waziri kamili.

Nauona ukweli kwa mbali sana lakini jitihada zao sijui kama zitafua dafu.
 
No CCM wanataka watawale milele kwa vile wamegundua kuwa Watanzania ni mazuzu ............................!!! Hili ni Upepo tu, utapita....................!!

mzuzu ni ukawa pekee hapa tanzania.
 
Usikute jf mnafanya biashara na hao jamaa,
iweje tusiamini kwamba mmewa beep then,
wana wapa mgao halafu hamuiweki report kamili?
(Nashawishika kuamini kuna game inaendelea)
FEDHA INA NGUVU.
 
Wacha ujuha.

Huu sio ujuha, ni wendawazimu.....

FaizaFoxy....leave this ----. Napenda leo uongelee hii issue, naona mpaka sasa hujaongelea. wewe ni supporter mkubwa wa JK na CCM, Can you say something on this???

Matendo yao yanastahili huruma na upendo wako kwao? uteteaji wako kwao unastahiki au wanakusaliti?
 
inaonekana hivyo .... ila hapo kwenye page 57 - 59 kuna nini? .... na je hii ndio original aliyofanyia kazi Otuoh?

Kama ripoti ndo hii, usitegemee kuwa na chochote katika hizo pages, kwa sababu, mapendekezo yote yako katika kila hadidu, hizo page zilizochomolewa labda zitakuwa ni appendixes
 
Huu sio ujuha, ni wendawazimu.....

FaizaFoxy....leave this ----. Napenda leo uongelee hii issue, naona mpaka sasa hujaongelea. wewe ni supporter mkubwa wa JK na CCM, Can you say something on this???

Matendo yao yanastahili huruma na upendo wako kwao? uteteaji wako kwao unastahiki au wanakusaliti?

Issue tuiongelee zitapotoka rasmi ripoti za CAG, PCCB na PAC, sasa hivi tunapiga porojo za hapa na pale.
 
Ooh,nchi itatingishika,..itingishike wapi wewe?.

Kuna kitu inaitwa causal-effect relationship ya matukio sasa kinachoangaliwa ni cause na sio effect hivyo yeyote aliye timamu huwa haangalii mwisho wa tukio ila mwanzo na uhusiano wa kila tukio na mwisho ulivyoandikwa!!!

Thus kwa wanaotaka kuaminisha watu kuwa "composition" ndio "reality" kama wewe mko busy kutaka watu wote wa bank on the "written" hata kama hai reflect mtiririko huo hapo juu!!!!
 
Invisible tunaomba utuweke ripoti Kamili tumeshachoka na hizi danadana.
Na taasisi yoyote inayoweza kuorganize maandamano wafanye hivyo tukinukishe.
Nimechoka na hizi porojo zisizo na hitimisho.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom