Jeshi letu linaonyesha umahiri wa kupigwa na tofali zama hizi!? Hawaoni wenzao huko duniani?

naomba kuuliza kwa aliyeangalia Yale maazimisho hv yule mama aliyekaa katikati ya kikwete na majaliwa ni nani au anaitwa nan?
 
Mkuu...

Sitaki kuwatetea kwamba wamefanya vyema sana... Lakini kwenye ukweli tushabikie na kwenye uongo tuupinge.

Ulitaka kwenye uwanja kama ule warushe risasi za ukweli au warushe mabomu ya ukweli kama wapo uwanja wa medani?

Ulitaka waje na mizinga pale au vifaru vizito na wapigane kama wapo uwanja wa medani?

Au hizo ndege zije mule uwanjani na kumwaga risasi na makombora kama wapo uwanja wa vita?

Makomandoo wote duniani maonesho yao yanalingana... Hebu google maonesho ya urusi uone kama komandoo wao "SPETNAZ" hawafanyi haya waliofanya watanzania wetu Leo... Ikiwa urusi yenye technolojia kubwa nayo inafanya maonesho hayahaya ya kuvunza tofali,kupasua mbao na kadhalika,ulitaka sisi tufanye nini?.

Angalia Special Force ya China katika maonesho yao kama hawafanyi hayahaya tuliofanya sisi Leo... Au Special Force ya North Korea kama hawapasui matofali,kupinda nondo na mengineyo.

Maonesho yote ya makomandoo ulimwenguni ulingana kwa kuwa yamelenga kwenye ukakamavu na utimamu wa mwili na akili.

Ebu katazame pia mafunzo ya Navy Seal ya Marekani uone kama hawayafanyi haya... Tena ni magumu zaidi ya haya uwa wanalalishwa baharini na mawimbi yakiwafunika.

Komandoo ni wanajeshi wa kazi maalumu... Sasa unataka akienda kukomboa mateka kwenye guest house aingie na vifaru au drones?... Hapo lazima utimamu wa mwili na mafunzo ya ngumu yatumike.

Kingine msipende kufananisha technolojia ya nchi za wenzetu na yetu... Marekani ina rais wa arobaini na kitu sisi ndio kwanza rais wa tano halafu tunataka tushindanishe technolojia.

Pia yale ni maonesho... Hivyo lazima yabaki kuwa maonesho ile ni 1/10 ya mafunzo alionayo komando.

Lazima jeshi liwe na mipaka ya kuonesha siri zake ili kuavoid kuwa dhaifu kwa adui.

Tuwe wazalendo na nchi yetu jamani.

Wakati mwingine mkuu, asiyejua maana usimwambie maana. Hata wahenga walituonya hilo.
Tatizo linalotusumbua wabongo ni kutokujua na kutokujua kwamba hatujui. Humu mtu hajui ila atakuja na uzi wake mreeefu wa kuponda jambo kumbe anasubiri watu wenye uelewa wamjibu naye ndio apate kuelewa. Hatuna desturi ya kuuliza ili tujue bali ni kuponda na kubisha ili tujue.
Tatizo ni kubwa!!
 
Juzi juzi tu, jwtz imepewa tuzo huko DRC
Kujilinganisha na DRC hakuondoi haja ya jeshi letu kubadili mafunzo yake yawe ya kisasa zaidi.

DRC kumejaa Child soldiers, ambao wamedumaa. Kama kweli ni bora basi waende wakawapige ISIS
 
Sherehe za Muungano hazina mvuto kabisa. Ni bora tuwe tunapumzika kama tufanyavyo siku za Nyerere na Karume days. Vinginevyo Rais awe analihutubia taifa moja kwa moja toka Ikulu. Kama vipi yafanyike makongamano ya kujadili kero za Muungano.

Nimekuwa nikifuatilia maonyesho ya mbinu za kijeshi za majeshi yetu kuanzia makomando mpaka jeshi la polisi, hakika hazionyeshi kwenda na wakati.

Katika zama hizi za teknolojia ya ndege zisizokuwa na rubani na kurusha makombola ya masafa marefu... Ninyi mnaonyesha kupigana na matofali na vipande vya mbao? Ni lini utakutana na adui umpige na tofali? Labda kama ni mbinu za kuwadhibiti wapinzani hapo sawa.

Mapambano dhidi ya wahalifu au Vita katika zama hizi yanafanywa kiakili na kiteknolojia zaidi. Mahitaji ya mtu anayeweza kuhimili kupigwa na nondo ama tofali yamepungua sana kama siyo kwisha kabisa.

Wahalifu wengi hawana maguvu ya mwili wala hawatumii nguvu katika kutekeleza mambo yao. Na hata wapiganaji wa zama hizi hawatumii tena magumi wala maguvu kubeba matofali. Kuna vifaa vya kiteknolojia vinavyofanya yote haya.

Niombe mtuonyeshe mambo yanayoendana na mabadiliko ya zama. Onyesheni show za kisasa kama zile za Korea Kaskazini.
Kila kinachofanyika ni kwa sababu maalum, kwani unahisi adui atakupiga na tofari? Pale walikuwa na lengo la kuonyesha ukakamavu wa askari wetu(komando). Nchi haiwezi ikafanya jambo kukupendeza/kukuridhisha wewe pekee! Sisi tuna utaratibu wetu wa kufanya mambo yetu na wao wana utaratibu wao. Jivunie cha kwako, usowe mtumwa wa fikra!
 
Jambo la msingi ni kuacha kutumia majeshi yetu kwenye maonyesho yasiyokuwa na tija, mimi nafikiri yangefanyika kwenye maadhimisho ya siku ya majeshi. Kama ni kutisha upinzani hilo nalo neno manake nilimsikia MC yuko kisiasa zaidi.
 
FaizaFoxy why hawatuonesh technologies wapo busy na physical??? Dunia ina move so fast acha kutetea ... Waoneshe how fit they are digitally... Dunia ya wazee ishapitwa... Only fit shall survive
 
Huku kwetu waliofeli au kukosa ajira ndo wanajiunga na majeshi yetu. Yaani ni full maguvu, technologia ZERO
Waliofaulu na wamebaki uraiani, kipi wamekifanya hata kukopi baiskeli ya kichana tu wameshindwa, hata unadhani wakienda jeshini ndiyo watabadilika. Mbona huko walikobaki hata kukopi baiskeli ile ya kichina imeshindikana, wasomi wa nchi hii wataendelea kutumia teknelojia walizounda wengine tu.
 
mkuu Yale matofali sina uhakika kuwa yanafaa kwa matumizi ya kujengea maana haiwezekani tofali ya sementi ikapigwa nyundo moja ikawa mchanga kihasi kile
kuna chokochoko sana humu JF!!!! Kama vigae basi ujue ni vile vya zamani sana vilivyotolewa kwenye military barracks za wakoloni, vishajichokea kikipigwa ngumi moja tu hata na afande wa kike kinaitikia mapigo.
 
58ff5c0ac461889f398b4592.jpg
 
Waliofaulu na wamebaki uraiani, kipi wamekifanya hata kukopi baiskeli ya kichana tu wameshindwa, hata unadhani wakienda jeshini ndiyo watabadilika. Mbona huko walikobaki hata kukopi baiskeli ile ya kichina imeshindikana, wasomi wa nchi hii wataendelea kutumia teknelojia walizounda wengine tu.
...We we ulifaulu au ulifeli?
 
Huku kwetu waliofeli au kukosa ajira ndo wanajiunga na majeshi yetu. Yaani ni full maguvu, technologia ZERO
Hili nalo neno. Tunategemea ubunifu wa silaha ya kisasa toka kwa f4 failure? Acha watumie vichwa kukunja nondo ili hali nyundo zipo.
 
Kila kinachofanyika ni kwa sababu maalum, kwani unahisi adui atakupiga na tofari? Pale walikuwa na lengo la kuonyesha ukakamavu wa askari wetu(komando). Nchi haiwezi ikafanya jambo kukupendeza/kukuridhisha wewe pekee! Sisi tuna utaratibu wetu wa kufanya mambo yetu na wao wana utaratibu wao. Jivunie cha kwako, usowe mtumwa wa fikra!
...Kama kuvunja tofali la udongo ni ukakamavu vipi anayevunja msitu heka nzima kufungua Shamba?
 
mkuu Yale matofali sina uhakika kuwa yanafaa kwa matumizi ya kujengea maana haiwezekani tofali ya sementi ikapigwa nyundo moja ikawa mchanga kihasi kile
ZILE Ni sarakasi za KARAGOSI Tu. Nani atakuja kukushambulia na matofali dis karne. Ni ukakamavu na inaongeza tolerence but tuonesheni na vitu vya technologies ......sio matofali na tushayachoka Kila Mara matofali matofali matofali MISUMARI eeeeeeee
 
Kikundi cha Ya moto kimejidhalilisha kwa kuvaa ngu zenye rangi ya chama fulani na kuzuga kushika bendera ya Nchi.Kwaya ya Makongoro Mwanza imefunika.Nilikuwa sijawaelewa wanaosema Rais asome hotuba.Leo kasoma na ilikuwa Supa ingawa alikuwa anatoka kidogo kwa kujisahau.Mungu ubariki Muungano
Mbona unachanganya mambo sasa
 
Back
Top Bottom