Jeshi latanda Mjini Songea

Jeshi latanda Mjini Songea

Habari wakuu.

Kuna hali ambayo siyo ya kawaida hapa Songea kwani asubuhi ya leo kila kona hapa Mjini na nje ya Mji Wanajeshi wametapakaa mitaani na hakuna taarifa yoyote ya uhakika iliyopatikana, watu wameingiwa hofu hata vyombo vya usafiri ikiwemo bodaboda kama ilivyozoeleka hakuna.


Mji umepoa sana.


Kwa mwenye taarifa zaidi tujuzane waungwana.
Watanzania wapasha habari Bwana tabu tupu wakilindwa shida!!! wasipolindwa serikali gani hii??? mambo ni ilimradi tu wamelaumu hivi au vile
 
Ni kweli mkuu nipo na gari ndogo tinted imenilazimu nizitoe zote imebaki clear! wanaweza wakakushuku wakakupasua ubongo ndan ya gari

Hahahahaha...mkuu umenifurahisha sana..ila JWTZ hawako hivyo..
 
Basi la superfeo la Dar mbinga lilizuiliwa eneo la national milling Usiku huu Kwa Muda wa saa nzima. wananchi hawaelewi kinachoendelea wanaogopa yasije yakawa ya 2005
 
Basi la superfeo la Dar mbinga lilizuiliwa eneo la national milling Usiku huu Kwa Muda wa saa nzima. wananchi hawaelewi kinachoendelea wanaogopa yasije yakawa ya 2005
Tena pale karibu kabisaa na kambi ya jeshi ya Ruhuwiko
 
Ni mazoezi ya kawaida kucheki battle readiness,deployment etc

Yalianza saa kumi na mbili asubhi na kuisha saa nne usiku
 
updates jamani mliopo songea, familia ipo huko likizo na simu zimekuwa offline
 
Hivi ni kambi z0ote za jesh songea .chabruma chandamali chandarua na ruhuwiko vimetawanyika hapo mjini
 
Acha unanga route match ya kuzagaa mtaani ni ya jeshi gani?

Vijana wa JKT mujibu wa sheria wanajiona wameiva sana Mkuu, mimi nadhani huo mkusanyiko wao utakuwa ni sehemu ya mafunzo yao, mara nyingi huwa wanajigawa makundi mawili, kundi la Adui na kundi la mapambano. Wanweza anzia porini na kuja mpaka mjini kulingana na mwelekeo wa Adui.

Nafikiri ndicho walichokuwa wanafanya hao Walinzi wetu, Watu wa Songea toeni hofu.
 
Vijana wa JKT mujibu wa sheria wanajiona wameiva sana Mkuu, mimi nadhani huo mkusanyiko wao utakuwa ni sehemu ya mafunzo yao, mara nyingi huwa wanajigawa makundi mawili, kundi la Adui na kundi la mapambano. Wanweza anzia porini na kuja mpaka mjini kulingana na mwelekeo wa Adui.

Nafikiri ndicho walichokuwa wanafanya hao Walinzi wetu, Watu wa Songea toeni hofu.

Hapo kidogo umetuelewesha mkuu.
 
Back
Top Bottom