Jeshi la wananchi Egypt lampindua Rais Morsi

Jeshi la wananchi Egypt lampindua Rais Morsi

Haya ya leo yalikuwa mapinduzi ya jeshi?

Au yale ya mwaka 2011 yalikuwa mapinduzi ya jeshi?

Mapinduzi ya kijeshi Misri yameanza toka mwaka 1952.
 
Mkuu EMT, hiyo ilikuwa leo mchana na akaja kuongea mambo tofauti na ile Ultimatum ya 48 hours aliyopewa na Al-Sisi

Mohamed Mursi yupo chini ya ulinzi wa SCAF masaa zaidi ya nane sasa.

Amerudisha pasi ya kusafiria yeye na watu wake wote wa karibu kuwazuia kukimbialia nje ya Misri.

Atawekwa kizuizini na akileta za kuleta atatiwa adabu.

Mursi%20Arrested%20Egypt%20Daily%20News.jpg

Mursi chini ya ulinzi , picha kwa hisani ya gazeti la Misri la Daily news

 
tatizo letu hatuna uzalendo
jeshi limepoozwa kwa kupewa vitu vya bure na kwa sasa wana supermarkets na maduka yakwao
wamepewa na hyundai nk kama rushwa iliofichika ili kuwafunga midomo
tena hapa serikali ya CCM inatakiwa kushtakiwa kwa kuwafunga jeshi midomo kwa kuwahonga
jeshi kama jeshi hawatakiwi hizo fadhila ni hatari kwa usalama wetu.

...weeeee mwenzio unataka akose ubalozi akistaafu
 
Mapinduzi ya kijeshi Misri yameanza toka mwaka 1952.

Sikukuuliza mapinduzi ya kijeshi Misri yalianza mwaka gani.

Nimekuuliza yaliyotokea leo na mwaka 2011 ni military coups?
 
Hii ni nchi ngumu sana kutawalika,ina idadi ya watu zaidi ya milioni 90 wengi wao wakiishi maisha duni kabisa bila kazi yoyote,kwa mda mrefu walitawaliwa kibabe na Mubarak,kwa kuwa alikuwa mjeshi alikuwa na sapoti kubwa sana toka kwa jeshi na katika fani yenye pesa na heshima kubwa Misri ni jeshi.Japo hakupendwa sana nchini kwake Hosni Mubarak alikuwa rafiki mkubwa wa nchi za kiarabu na kipindi chake wamisri wengi walikuwa wanafanya kazi Arabuni zaidi kwenye nchi za G.C.C.Baada ya kupinduliwa kwa Mubarak nchi nyingi za Arabuni zilikataa kuwapa visa na misaada wamisri hivyo maisha yao yakazidi kuwa magumu zaidi.
Wamisri wana umoja sana lakini tatizo nchi yao ilinyonywa mda mrefu sana,na vuguvugu la kumng'oa Hosni lilikimbiza watalii wengi na uchumi wao ukayumba,mategemeo yao ni kwamba ndani ya kipindi kifupi cha mwaka mmoja raisi Morsi angekuza uchumi !!!haikuwezekana
 
So, was this a military coup Sir?

Do you agree with the latest statement released by Morsi that kilichotokea ni military coup?

Absolutely; nadhani watu wanasahau tu kuwa mapinduzi ni njia pia ya kuleta utawala; lakini ni njia ya mwisho. Mapinduzi yanaweza kuwa ya watu (popular revolution) au ya kijeshi (military). Na yote hayo yanaweza kuwa ya damu au ya kutokumwaga damu. Mapinduzi yaliyomuondoa Mubarak yalikuwa ni ya watu na hayakuwa na umwagikaji damu; haya ni ya jeshi na so far hakuna umwagikaji damu.

Mapinduzi ya jeshi hasa yanapofanyika kwa kumwaga damu damu inamwagika kwelikweli. Hata hivyo katika hili jeshi halikwenda hatua zote za kinadharia za kufanya mapinduzi. Limempa mtawala nafasi kubwa ya kujirekebisha na akakataa; hata leo hii hili haikuwa lazima kama Morsi angekuwa na hekima ya kusikiliza na kusoma alama. Watu wengi wanafikiria - kwa makosa - kuwa kwa vile mtu kachaguliwa na wengi basi anaweza kufanya lolote, popote na kwa vyovyote bila kujali maslahi na madai ya minority group. Hili ndio kosa la Morsi na la viongozi wengine wengi ambao walijikuta wanalazimishwa kutoka madarakani kwa mapinduzi.

Kuchaguliwa tu hakukufanyi uwe wa demokrasia. Jinsi gan iunatawala na jinsi gani unalinda maslahi ya minority group.
 
hahaha kwa sababu walikuwa ni wakatoliki n' they were taking orders frm vatican.pls foward hilo gbu to ur fellow team gerezani n' lumumba.

Huu uzi siyo wa Bavicha nakushari ungekuwa msomaji tu kuliko kujidhalilisha.
 
El Baradei amefanya kazi sana UN na ni mtu ambae ndie alitarajiwa kushinda uchaguzi uliopita kwahio wananchi wameona kwa kuwa ana medali ya Nobel basi ashike madaraka ya uraisi na kuipanga upya nchi na kuitayarisha kwa ajili ya uchaguzi ndani ya wiki chache zijazo.

It was believed that hana experience na siasa za ndani za Misri kwa sababu amespend muda mwingi nje ya nchi.
 
Nilidhani chief justice ndiye anakuwa kiongozi wa serikali ya mpito?

Sidhani kama ni vyema kumteua Mohamed El Baradei kuwa kiongozi wa serikali ya mpito ikizingatiwa alikuwa opponent wa aliyepinduliwa.
hata mim nipo confused hapo.
 
Kwa nini usikamatwe kwa kuchochea uhaini au wewe ni chadema? hakuna manufaa kwa jeshi kuipindua serikali. leo wamisri wana lipi la kujivunia maandamano na vurugu?

Mawazo yako mafupi kama akili zako!
JWTZ wana cha kujifunza kuwa "will of the people should be accepted and if denied must be enforced". Hii ina maana si tu kuwa kumwondoa rais au yeyote ambaye wananchi wengi hawamtaki bali pia kuzuia kumwondoa yule ambaye wananchi wengi wanamtaka na wachache hawamtaki.

Sioni tatizo hapo na wala hajasema JW wampindue Rais Kikwete. Kwanza umeona hata maandamano hapa?
 
Hivi mnajua kuwa kuna watu milioni 22 waliosaini petition ya kumkataa Morsi?
 
Absolutely; nadhani watu wanasahau tu kuwa mapinduzi ni njia pia ya kuleta utawala; lakini ni njia ya mwisho. Mapinduzi yanaweza kuwa ya watu (popular revolution) au ya kijeshi (military). Na yote hayo yanaweza kuwa ya damu au ya kutokumwaga damu. Mapinduzi yaliyomuondoa Mubarak yalikuwa ni ya watu na hayakuwa na umwagikaji damu; haya ni ya jeshi na so far hakuna umwagikaji damu.

Tukisema kilichotokea leo ni military coup siyo kama tuna-igonre efforts za Wamisri walioshinikiza mpaka haya kutokea?

Could this be a mixture of popular revolution and military coup? Or something else? http://www.harvardilj.org/wp-content/uploads/2010/05/HLI203.pdf
 
Sikukuuliza mapinduzi ya kijeshi Misri yalianza mwaka gani.

Nimekuuliza yaliyotokea leo na mwaka 2011 ni military coups?

Ndiyo yote ni mapinduzi ya kijeshi, mwaka 2011 yalikuwa chini ya Field Marshal Mohamed Tantawi.
 
It was believed that hana experience na siasa za ndani za Misri kwa sababu amespend muda mwingi nje ya nchi.

Ni kweli, lakini hii ndio kasumba ya watu wengi kwamba kama upo nje ya nchi basi hufahamu kinachoendelea nchini kwako.

Watu wanakosea sana kwamba siku hizi dunia ni utandawazi na imejaa kila kifaa cha mawasiliano.

Nchi ya Misri ndio nchi pekee ambayo njia za mitandao ya internet ipo wazi kwa kila mwananchi mwenye uwezo wa kutumia.

Kinachofanyika ni careful planning, mobilization na staging ambayo ndio ipo kwenye Facebook, Twitter na other sicial media.
 
Hakuna ushabiki au uzalendo katika kumwaga damu. Bibi yangu ana zaidi ya miaka 100, balaa likiibuka nani atamsaidia? Mke wangu anategemea, balaa likiibuka atakwenda wapi. Tulipata ukombozi 1961, bila ya damu na history repeats itself

You are such a fool like a sheep! Huyo bibi yako ataishi milele??
 
Tukisema kilichotokea leo ni military coup siyo kama tuna-igonre efforts za Wamisri walioshinikiza mpaka haya kutokea?

Could this be a mixture of popular revolution and military coup? Or something else? http://www.harvardilj.org/wp-content/uploads/2010/05/HLI203.pdf

Au tuseme watu milioni 22 wasingesaini ile petition...halafu wasingejitokeza kwa wingi sana kwenye bustani ya Tahrir...jeshi lingeweza kweli kumuondoa?

The people deserve a lot of the credit too. They started it by thoroughly rejecting him and the military joined them.
 
Back
Top Bottom