Jengo limeanguka Zanzibar, mtu mmoja ajeruhiwa, wengine 15 wameokolewa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Jengo la PBZ lililopo Forodhani limeanguka, inadaiwa kulikuwa na watu kadhaa ndani ya jengo hilo lakini bado hakuna taarifa rasmi juu ya chanzo cha tukio hilo na madhara yaliyojitokeza.Jengo la PBZ lililopo Forodhani limeanguka, inadaiwa kulikuwa na watu kadhaa ndani ya jengo hilo lakini bado hakuna taarifa rasmi juu ya chanzo cha tukio hilo na madhara yaliyojitokeza.

fa10c175-b931-430c-a927-34b296378e6d.jpeg



==============

Jengo lilokuwa makao Makuu ya Benki ya Watu wa Zanzibar [PBZ] katika eneo la Forodhani limeanguka sehemu ya nyuma ya jengo hilo wakati likiendelea kufanyiwa ukarabati mkubwa ambapo ajali hiyo imejeruhi mtu mmoja kati ya watu 16 walikuwepo katika Jengo hilo

Akizungumza na wandishi wa habari Mkuu wa Operesheni Zimamoto na Uokozi Mrakibu Mbarouk Ali Juma amesema jengo hilo limeporomoka majira ya saa 8 mchana na kusababisha majeraha ya mtu mmoja kati ya watu kumi na sita waliokuwepo katika jengo hilo wakiwemo mafundi na mama ntilie

Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Simai Mohamed Said amesema tayari amemuagiza Mkurugenzi wa Mji Mkongwe kuyafanyia ukaguzi majengo yote ya mji mkongwe ili kubaini majengo hatarishi huku akiwaasa wananchi kuwa tayari kuyahama majengo ambayo yatabaika kuwa na dosari.
b46476a3-f3cc-482d-887d-40d23c5b5db0.jpeg

e0cc560c-e1bf-447a-a575-ad9a60010487.jpeg
 
Inaonekana ni jengo la matope tupu.. Poleni majeruhi hope hakuna walioumia sana.

Mamlaka husika fanyeni kazi kuokoa ndugu zetu mapema.
 
Jengo la PBZ lililopo Forodhani limeanguka, inadaiwa kulikuwa na watu kadhaa ndani ya jengo hilo lakini bado hakuna taarifa rasmi juu ya chanzo cha tukio hilo na madhara yaliyojitokeza.Jengo la PBZ lililopo Forodhani limeanguka, inadaiwa kulikuwa na watu kadhaa ndani ya jengo hilo lakini bado hakuna taarifa rasmi juu ya chanzo cha tukio hilo na madhara yaliyojitokeza.


==============

Jengo lilokuwa makao Makuu ya Benki ya Watu wa Zanzibar [PBZ] katika eneo la Forodhani limeanguka sehemu ya nyuma ya jengo hilo wakati likiendelea kufanyiwa ukarabati mkubwa ambapo ajali hiyo imejeruhi mtu mmoja kati ya watu 16 walikuwepo katika Jengo hilo

Akizungumza na wandishi wa habari Mkuu wa Operesheni Zimamoto na Uokozi Mrakibu Mbarouk Ali Juma amesema jengo hilo limeporomoka majira ya saa 8 mchana na kusababisha majeraha ya mtu mmoja kati ya watu kumi na sita waliokuwepo katika jengo hilo wakiwemo mafundi na mama ntilie

Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Simai Mohamed Said amesema tayari amemuagiza Mkurugenzi wa Mji Mkongwe kuyafanyia ukaguzi majengo yote ya mji mkongwe ili kubaini majengo hatarishi huku akiwaasa wananchi kuwa tayari kuyahama majengo ambayo yatabaika kuwa na dosari.
kafara la 2025 lazima lianzie nyumbani
 
Hata mwaka juzi kuna jengo lilianguka ngome kongwe, utalii wa mij iya zamani na changamoto zake.
 
Kizuri ni kuwa hayo majengo yapo katika hifadhi ya UNESCO ya urithi wa dunia lakini kibaya zaidi yanaporomoka siku baada ya siku na kupelekea majeruhi na vifo kwa ndugu zetu. Ifike mahali/siku Serikali ione umuhimu wa kuyajenga upya kwa jinsi kama yalivyokuwa bila kupoteza uhalisia wake.
 
Kwa ufupi nilipopita na kuona majengo mengi pale mji mkongwe ni hayafai binadamu kuishi, yamechoka.

Ukiongea na wenyeji waliozaliwa humo stone town wansena hawawezi kuhama kirahisi sababu wamezoea na ndiyo kijijini kwao hapo ila sasa, yakiwakuta kama hilo la jana wana kauli nyingine tena wanaisema serikali 😂!.

Kuna eneo nilipita nimeona wanachofanya ni kuyajenga upya kwa saruji na mawe ila jengo linatakiwa liwe kama lililokuwepo awali.

Serikali ya mapinduzi zanzibar inapaswa kuwapa tenda wenye uwezo kuyafanyia ukarabati au ujenzi upya vinginevyo madhara yatakuwa makubwa kuliko kawaida.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom