JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Jengo la PBZ lililopo Forodhani limeanguka, inadaiwa kulikuwa na watu kadhaa ndani ya jengo hilo lakini bado hakuna taarifa rasmi juu ya chanzo cha tukio hilo na madhara yaliyojitokeza.Jengo la PBZ lililopo Forodhani limeanguka, inadaiwa kulikuwa na watu kadhaa ndani ya jengo hilo lakini bado hakuna taarifa rasmi juu ya chanzo cha tukio hilo na madhara yaliyojitokeza.
==============
Jengo lilokuwa makao Makuu ya Benki ya Watu wa Zanzibar [PBZ] katika eneo la Forodhani limeanguka sehemu ya nyuma ya jengo hilo wakati likiendelea kufanyiwa ukarabati mkubwa ambapo ajali hiyo imejeruhi mtu mmoja kati ya watu 16 walikuwepo katika Jengo hilo
Akizungumza na wandishi wa habari Mkuu wa Operesheni Zimamoto na Uokozi Mrakibu Mbarouk Ali Juma amesema jengo hilo limeporomoka majira ya saa 8 mchana na kusababisha majeraha ya mtu mmoja kati ya watu kumi na sita waliokuwepo katika jengo hilo wakiwemo mafundi na mama ntilie
Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Simai Mohamed Said amesema tayari amemuagiza Mkurugenzi wa Mji Mkongwe kuyafanyia ukaguzi majengo yote ya mji mkongwe ili kubaini majengo hatarishi huku akiwaasa wananchi kuwa tayari kuyahama majengo ambayo yatabaika kuwa na dosari.
==============
Jengo lilokuwa makao Makuu ya Benki ya Watu wa Zanzibar [PBZ] katika eneo la Forodhani limeanguka sehemu ya nyuma ya jengo hilo wakati likiendelea kufanyiwa ukarabati mkubwa ambapo ajali hiyo imejeruhi mtu mmoja kati ya watu 16 walikuwepo katika Jengo hilo
Akizungumza na wandishi wa habari Mkuu wa Operesheni Zimamoto na Uokozi Mrakibu Mbarouk Ali Juma amesema jengo hilo limeporomoka majira ya saa 8 mchana na kusababisha majeraha ya mtu mmoja kati ya watu kumi na sita waliokuwepo katika jengo hilo wakiwemo mafundi na mama ntilie
Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Simai Mohamed Said amesema tayari amemuagiza Mkurugenzi wa Mji Mkongwe kuyafanyia ukaguzi majengo yote ya mji mkongwe ili kubaini majengo hatarishi huku akiwaasa wananchi kuwa tayari kuyahama majengo ambayo yatabaika kuwa na dosari.