Jengo la ghorofa kadhaa laanguka mjini DSM!

hiyo sign board iko upande wa kulia wa picha yako mkuu, tuiwahi na majina ya walio hapo tuanze kumkomalia nyani mchana kweupe
 
Ile stationary inayosadikiwa imefukiwa ipo upande wa kulia wa picha hizi ndo watu wanako hangaika kuwaokoa wakuu nimeshindwa kupiga picha ya ile bord kuonyesha contractors na client nitajitahidi kupenyeza camera ili nilete news hapa jamvini.
 
kama inawezekana, tuletee pia piicha za signboard, ule ubao unaonyesha client, consultant, structural engineer, nk. ni muhimu kufahamu hawa watu waliotufikisha hapa. kwa kuwa inasemekana tangu jana jengo lenyewe lilionekana kuegemea upande mmoja. baadaye nitwaambia wakuu wangu, majengi mengi yanayojengwa dsm, si salama, kuna uhuni mwingi. nitaupasua hapa jamvini kwa kuwa hii ndo taaluma yangu. tumepiga kelele mingi sana kwenye semina, warsha nk, lakini taasisi zinazohusika kama ERB, AQRB, CRB, NCC, wameweka pamba maskioni.

Ukweli ni kuwa bei ya maisha ya mtanzania iko chini sana. Hao wanaojiita wawekezaji wanataka ku'maximise profit' kwa kutumia the cheapest consultants and contractors. Baadhi ya hao consultants na contractors wameji'prostitute' kufikia hatua ya kukodisha majina yao yatumike na watu ambao hawako 'qualified'. Wajenzi/mafundi hawaogopi kujiingiza kichwa kichwa kwenye miradi ambayo hawana utaalamu/ujuzi nao. Tunafanya dhihaka katika kuhakikisha ubora wa bidhaa za ujenzi, kuanzia nondo, simenti, mchanga, kokoto n.k. Sasa tuwangoje watakaokuja, watalia, watafoka na wachache watatolewa kafara, na biashara itaendelea.
 
Ghorofa jipya lililokuwa likijengwa mitaa ya mtendeni/kisutu limeanguka na kuangukia jengo dogo ambalo watu walikuwa wanaishi. Jengo hilo linasemakana lilikuwa na ghorofa 7 au 8 lilionekana kuegemea upande moja hadi kufikia jana. Nitawaletea taarifa zaidi kadri nitakavyozipata.

Hii kali, yaani jengo linainama na hakuna anayechukua hatua yoyote mpaka linaanguka! Nani alikuwa anasimamia ujenzi huu?
Ebu tupeni habari zaisi, nani anamiliki hilo jengo?
 
Hii ni aibu kwa wahandisi na bodi zote zinazohusika na majengo, pia inawezekana wataalam wetu wa Halmashauri hawana utaalam wa kutosha kwani wangeweza kugundua na kuzuia mapema. sasa jengo hili lingeanza kutumika ingekuwaje? si maafa yangekuwa makubwa zaidi. mbaya sana, Mungu awaponye waliojeruhiwa kwani hawana kosa jamani.
 
Hivi Tanzania tuna vifaa maalumu vya Uokoaji au wataalamu wa majanga kama haya.... au ndio hadi tukaazime nguvu kazi ktk Majeshi yetu (JKT na JWTZ)?? Maana nahisi wahanga wengi watapoteza maisha yao kwa kukaa muda mrefu ndani ya vifusi kwasababu ya ukosefu wa vifaa......
Bodi ya wakandarasi ikowapi hadi tunapata majanga haya nguvu kazi ya taifa inapotea... kipindi cha nyumanyuma hapa walidai wanapita kila mara kuangalia mwenendo wa majengo yanayojengwa hapa nchini maana huku mjini ujenzi wa magorofa umeshamiri sasa walikuwa wanaangalia nini?? ama walikuwa wanapita kuangalia kama viparua wamevaa safte equipment?? sio ubora wa jengo au walikuwa wakipita wanaondoka na vibahasha ukaguzi ndio unakuwa umekamilika??
Tutaendelea na hali hii ya kuwa na Bodi zembe ya wakandarasi mpaka lini? Ama watatuambia hilo jengo lilikuwa halijafikiwa siku ya ukaguzi tangu lianzwe kujengwa hadi sasa lilikuwa na hizo gorofa 7 or 8???

Inatia uchungu kuona ndugu zetu wanavyopoteza maisha yao huku wengine wakipeta.
 
waokoaji wakujitolea kama kawaida wameshaanza kazi ingawa nimeliona hata gari la fire nalo limetia timu katika eneo la tukio.
View attachment 1712
Wamiliki ni wahindi wa hili jengo.Limetitia lote.
View attachment 1713
Ngoja tusubili taarifa rasmi kuhusu majeruhi na idadi kamili ya walio kuwemo.

Asante kwa picha zako, Fidel. Waokoaji wa kujitolea watafanya nini bila ya kuwa na uongozi unaojua kinachotakiwa? Wakati mwingine pamoja na nia njema hii kutegemea adhoc inaleta gharama kubwa! Kazi ya uokoaji ina utaalamu wake.
 
kama sikosei iliundwa tume ya kuchunguza magorofa yote yaliyojengwa dar,lakini hiyo ripoti mpaka leo hatujui ilisema nini.
 
ni hivi, majengo mengi yanayojengwa mjini dsm.hutumia majina ya wakandarai kama geresha. wkandarasi waliosajiliwa huwauzia wahindi hilo bango kuonyesha kuwa wao ni wajenzi kwa laki tano. mwenye jengo huajiri mafundi wazoefu kufanya hizo kazi. hakuna cha engineer, architect, au quantity surveyor anayeajiriwa hapa, kisa kukwepa gharama. kuwashugulia hawa matapeli imekuwa ngumu kwa kuwa wanasiasa wengi nao siku hizi ni wkandarasi na ndo wanacheza huu mchezo mchafu. nitawapa na majina yao baadaye. natamani kwenye bango la leo awe ni mateo quares na kampuni yake ya BQ contractors au dr mzeru!

nikipata hicho kibao nitakuwa kwenye nafasi ya ku-comment zaidi
 
Wahindi na hongo ni shida sana .Jengo la Mhindi na walio angukiwa I hope ni wahindi pia .Mali kwa mali itakuwa na hapo sasa sijui watasemaje watu wa kutaka siri za Seikali zifichwe .
 
Eee mwenye enzi Mungu mtukuka, tuepushie mbali maafa katika nchi yetu! AMINA!
 
Tunashukuru kwa taarifa na tunatoa pole kwa wote ambao wamekumbwa na huo mkasa huo, tuombe Mungu madhara yasiwe Makubwa kwa binadamu
 
wataalam wetu wamekuwa na tamaa hawazingatii miiko ya taaluma zao! inawezekana vipi jengo lifikie hatua hiyo bila kugundulika kwa hitilafu zilizopelekea madhara haya kutokea. hivi haya mambo pia yanahitaji Rais au Waziri mkuu kusimamia?hakuna proffesional ethics hapa.tumuombe mwenyezi mungu anusuru roho za watu tena sana sana utakuta ni wale vibarua wabeba zege.
 
Hizi board zinazosimamia sekta ya ujenzi kwa ujumla zinatia aibu. wanakusanya ada lakini kusimamia miradi na kujenga maadili katika taaluma husika hawajali kabisa. matokeo yake wataalamu wanafikia mahali pa kuuza majina ya kampuni kwa wahind na kuweka vibao kwenye miradi kwa kupewa hela kidogo ya kula. laiti kama hizi boards singesimamia ipasavyo taaluma husika naamini miradi mingi ingejengwa kwa kiwango stahili na pia hali ya kiuchumi kwa wanataaluma wetu (wahandisi, wasanifu na wakadiriaji wa majengo) ingekuwa alhamdulillah. Lakini tatizo ni lile lile itendaji mbovu almost kwa vyombo vyote vya serikali.
 
kama sikosei iliundwa tume ya kuchunguza magorofa yote yaliyojengwa dar,lakini hiyo ripoti mpaka leo hatujui ilisema nini.

Hapo ndipo unapoghafirika na statement za viongozi...(https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=14641) angalia huyu hapa anatahadharisha wanahabari kutotoa siri (maana maelezo kwa wananchi wao wana classify kama siri) kwenye magazeti.... ni siri zipi hizo?

Katibu Tarafa, basi na hiyo ripoti unaweza kukuta imekuwa classified kama SIRI!!
---------------
Picha zaidi za tukio hizi hapa:

2w3s3mf.jpg


zt9e2g.jpg


16jq87r.jpg


Pictures, credit to issamichuzi.blogspot.com


SteveD.
 
mkuu fidel 80, kuna signboard inaonekana kwenye picha ya kwanza, tungeiwahi itatusaidia sana, kama ninavyojua, mwenye hili jengo na mhandisi wake watakimbilia kuingoa sasa hivi kuficha ushahidi, tafadhali muiwahi, wenzio tuko mbali sana na dsm.

Natumaini mzee unamaanisha awahi kuipiga picha, usije Fidel 80 akaibeba signboard nzimanzima
 
Kheee! wallahi tena mwaka wa shetani huu...EPA,RICHLOWASSA,BOT,Balali......
 
kinachoshangaza zaidi ni pale watu wanaporuhusiwa kuwa eneo hilo wakati inaonekana wazi kuwa jengo linaweza kuendelea kuanguka. Mkuu wa mkoa pamoja na polisi wapo pale lakini hawazuiii watu kuingia na kutoka hapo bila mpangilio maalum...hii ni hatari kwani watu zaidi wanaweza kufa ikiwa sehemu zilizobaki zitaanguka. nguzo zinaonekana si imara na wakati wowote zitaanguka
 
Tatizo letu bongo kazi tunapeana kiujomba zaidi .... hii inanikumbusha ile habari ya kule maeneo ya Keko lile jengo nalo lilivyo anguka sijui yule mkandarasi alihukumiwa au kesi bado iko mahakamani uchunguzi haujakamilika....?

..ina maana wahindi wajomba zetu?
 
Back
Top Bottom