Tutalia. Tutasahau. Tutaendelea kama kazi. Mpaka wafe wangapi ndio tuwe serious?
Huu ujenzi wa kubahatisha utaisha lini?
kinachoshangaza zaidi ni pale watu wanaporuhusiwa kuwa eneo hilo wakati inaonekana wazi kuwa jengo linaweza kuendelea kuanguka. Mkuu wa mkoa pamoja na polisi wapo pale lakini hawazuiii watu kuingia na kutoka hapo bila mpangilio maalum...hii ni hatari kwani watu zaidi wanaweza kufa ikiwa sehemu zilizobaki zitaanguka. nguzo zinaonekana si imara na wakati wowote zitaanguka
msingojee majibu ya tume ya lowasa, yalikuwa ni kusaka umaarufu tu. pia msikimbilie kumhukumu manispaa engineer. ninavyojua, kazi kubwa ya ujenzi wa ghorofa kubwa kama hili huwa inaangaliwa na wafuatao
1. architect-huwa anatengeneza michoro ya jengo lenyewe, na working drawings, kazi yake ni kuangalia kama ujenzi ukianza unafuata michoro aliyochora mwenyewe. ni kazi yake pia kuwasimamia washauri wengine walioko kwenye huo mradi(nitawataja hapa chini
2. quantity surveyor-huyu ni mtaalamu wa gharama za ujenzi, pia ni msomi katika karibu ya fani zote zilizoko kwenye ujenzi, ni wazi kuwa ili ufahamu gharama ya kitu ni lazima ujue kinavyotengenezwa na kinaavyofanya kazi, yeye humshauri cleint kuhusu mambo ya gharama.
3. structural engineer-huyu ndiye mtaalamu wa ubora wa jengo lenyewe, ni lazima atengeneze michoro ya nondo, asimamie ubora wa zege, na mambo mengine yanayohusu ubora na uimara wa jengo lenyewe
4. service engineer-hawa ni pamoja na mhandisi wa umeme, maji, airconditions, lift installation, alarms etc
5. municipa engineer/local authority-kuhakikisha ujenzi umefuata kanuni zote zinazohusu mahali hapo, building permit etc
6. mkandarasi aliyesajiliwa, kwa majengo makubwa kama hili angalau class 111, kutegemeana na gharama
ni wazi kuwa wa kwanza kukammatwa hapo juu ni structural engineer. lakini utashangaa wataanza kupoteza na muda na municipa engineer.
visit pia www.crbtz.com
msingojee majibu ya tume ya lowasa, yalikuwa ni kusaka umaarufu tu. pia msikimbilie kumhukumu manispaa engineer. ninavyojua, kazi kubwa ya ujenzi wa ghorofa kubwa kama hili huwa inaangaliwa na wafuatao
1. architect-huwa anatengeneza michoro ya jengo lenyewe, na working drawings, kazi yake ni kuangalia kama ujenzi ukianza unafuata michoro aliyochora mwenyewe. ni kazi yake pia kuwasimamia washauri wengine walioko kwenye huo mradi(nitawataja hapa chini
2. quantity surveyor-huyu ni mtaalamu wa gharama za ujenzi, pia ni msomi katika karibu ya fani zote zilizoko kwenye ujenzi, ni wazi kuwa ili ufahamu gharama ya kitu ni lazima ujue kinavyotengenezwa na kinaavyofanya kazi, yeye humshauri cleint kuhusu mambo ya gharama.
3. structural engineer-huyu ndiye mtaalamu wa ubora wa jengo lenyewe, ni lazima atengeneze michoro ya nondo, asimamie ubora wa zege, na mambo mengine yanayohusu ubora na uimara wa jengo lenyewe
4. service engineer-hawa ni pamoja na mhandisi wa umeme, maji, airconditions, lift installation, alarms etc
5. municipa engineer/local authority-kuhakikisha ujenzi umefuata kanuni zote zinazohusu mahali hapo, building permit etc
6. mkandarasi aliyesajiliwa, kwa majengo makubwa kama hili angalau class 111, kutegemeana na gharama
ni wazi kuwa wa kwanza kukammatwa hapo juu ni structural engineer. lakini utashangaa wataanza kupoteza na muda na municipa engineer.
Mfano mwingine ni Mafuta House... Ni bomu litalolipuka siku za usoni. Kwa waliofika pale na wamesomea Engineering haswa waliosomea Ujenzi wanaweza kukiri jengo liko low quality ile mbaya!
Ile stationary inayosadikiwa imefukiwa ipo upande wa kulia wa picha hizi ndo watu wanako hangaika kuwaokoa wakuu nimeshindwa kupiga picha ya ile bord kuonyesha contractors na client nitajitahidi kupenyeza camera ili nilete news hapa jamvini.
Ooops, nondo zake mkuu. Zimetengenezwa humu humu kwa kutumia chuma chakavu. They're not tested either.INVISIBLE,Unasema majengo mengi ya Kariakoo yamejengwa kwa kutumia chuma cahakavu, hapo sijakuelewa mkuu naweza pata ufafanuzi kidogo?
Hivi Mafuta House ndiyo BWM Tower. Hili lilisimamisha kwa muda wakati wa ujenzi kwa kuwa wakaguzi waliliona limepinda na kushauri libomolewe. Ila baada ya mjadala ulionekana huo udhaifu ni mdogo kulingana na thamani ya jengo. Kama ulivyosema hili ni bomu litakalolipuka muda wowote mbeleni tulipe kama 20 years hivi tukisubiri breaking news.mwikimbi unaonekana kuujua ujenzi na mtiririko mzima ulivyo.
Anyway, tayari Municipal Engineer kakamatwa na wale waliokuwa wanatazama thru ITV wameona akikamatwa live na kuchukuliwa palepale.
Hii ndiyo Bongo!
Ujenzi holela umeenea kwa kasi kubwa na nikipewa muda wa kupitia majengo mengi ya Dar naweza kuwatia ndani wengi kwa ujenzi wao wa kuudhi!
Mfano mwingine ni Mafuta House... Ni bomu litalolipuka siku za usoni. Kwa waliofika pale na wamesomea Engineering haswa waliosomea Ujenzi wanaweza kukiri jengo liko low quality ile mbaya!
Kariakoo hakuna jengo imara kabisa, nondo zilizojengea majengo mengi ya Kariakoo ni za chuma chakavu na ujenzi wenyewe umefanywa kwa deals tu ambapo ni wazi siku za usoni tuna matukio ya aina hii mengi.
Kwa wenye kumbukumbu nzuri (kuna wahandisi nawafahamu na mpo humu JF) mnaweza kukumbuka Linza Concrete Design walifutiwa leseni (sijui waliruhusiwa vipi) lakini mpaka naandika leo majengo mengi Structural Designer ni Linza!
Wahandisi wengi wanadharirishwa na wapuuzi wachache wanaoendekeza rushwa katika ujenzi na kuwa na upofu wa kufanya Quality Control. Inatia kichefuchefu kwa mhandisi mwenye akili timamu kusimama mbele ya magorofa ya Kariakoo na kuruhusu ujenzi uendelee huku akichekelea eti design nzuri akisahau kuwa linajengwa kwa vifaa dhaifu kabisa ili mradi ana 10% yake.
Tunaelekea kubaya zaidi na serikali isipochukua hatua madhubuti itajikuta kuna miaka kama 5 tu majengo zaidi ya 20 yameporomoka jijini Dar es Salaam.
Huu ni mwanzo tu, bado mengine yatadondoka kwa mwendo huu huu.
Inasikitisha lakini ndivyo tulivyo!