Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 12,890
- 11,356
Mimi nadhani tunaanza kuchanganya mambo. Hakuna haja ya kuunganisha issue hii na ya Kagoda. Hatari ni kuwa tukiipeleka huko itageuka kuwa suala la kiasi badala ya professional negligence and incompetence.
Hao watu wa bodi nao wana nafasi zao lakini mwenye mamlaka na maendelezi ya miji ni manispaa na si mwingine. Kwa hali hiyo, vibali vya ujenzi vinatolewa na yeye na ni yeye mwenye kuwajibika kuhakikisha ujenzi huo unaendana na malengo na sheria zake za maendelezi ya jiji. Hizo bodi wajibu wao ni kufuatilia ufanisi wa wale waliowaandikisha. CRB hawezi kumfuatilia architect au engineer na vile vile kwa AQRB. Wanachoweza kufanya ni kuwashtaki kwa bodi husika. Anayepaswa kubanwa hapa haswa ni manispaa, mwekezaji( kwa kuajiri na kutumia wataalamu na makandarasi wasiostahili na kutohakikisha usalama wa jamii) na wataalamu (architects na wahandisi) kwa kutotoa ushauri unaostahili. Napenda kutoa tahadhari kuwa inabidi hata michoro iliyopitishwa iangaliwe kama ilistahili kupitishwa. AQRB, wakishirikiana na AAT, wafuatilie suala la usimamizi wa architect. Kwa mfano,je palikuwa pakifanyika site meetings na inspections? Kama ndiyo, nani alikuwa akihudhuria na nini kilikuwa kikiamuliwa? CRB wamfuatilie mkandarasi wake kuhusu utendaji wake na kama alikuwa na haki na uwezo wa kazi hiyo. Bodi ya wahandisi wakishirikiana na IET na ACET wamfuatilie mhandisi wao. Hawa wote watoe taarifa itakayotolewa kwa wananchi.
Serikali kuu iangalie kwa undani taratibu za kutoa vibali vya ujenzi na usimamizi wa ujenzi. Mfumo tulionao tumeurithi toka kwa wakoloni, pengine kuna haja ya kuungalia tena. Manispaa zibanwe kuhakikisha kuwa watendaji wanapewa nyenzo za kufanya kile wanachopaswa. Ni aibu kuwa na building inspektaz wasio na usafiri (ingawa kwa hapa hilo halipo maana wangeweza kutembea kutoka ofisini kwao).
Sioni haja ya tume. Wasi wasi wangu ni bodi na mamlaka husika kuanza kunyosheana vidole na kutafuta ujiko kutokana na hii calamity.
Hao watu wa bodi nao wana nafasi zao lakini mwenye mamlaka na maendelezi ya miji ni manispaa na si mwingine. Kwa hali hiyo, vibali vya ujenzi vinatolewa na yeye na ni yeye mwenye kuwajibika kuhakikisha ujenzi huo unaendana na malengo na sheria zake za maendelezi ya jiji. Hizo bodi wajibu wao ni kufuatilia ufanisi wa wale waliowaandikisha. CRB hawezi kumfuatilia architect au engineer na vile vile kwa AQRB. Wanachoweza kufanya ni kuwashtaki kwa bodi husika. Anayepaswa kubanwa hapa haswa ni manispaa, mwekezaji( kwa kuajiri na kutumia wataalamu na makandarasi wasiostahili na kutohakikisha usalama wa jamii) na wataalamu (architects na wahandisi) kwa kutotoa ushauri unaostahili. Napenda kutoa tahadhari kuwa inabidi hata michoro iliyopitishwa iangaliwe kama ilistahili kupitishwa. AQRB, wakishirikiana na AAT, wafuatilie suala la usimamizi wa architect. Kwa mfano,je palikuwa pakifanyika site meetings na inspections? Kama ndiyo, nani alikuwa akihudhuria na nini kilikuwa kikiamuliwa? CRB wamfuatilie mkandarasi wake kuhusu utendaji wake na kama alikuwa na haki na uwezo wa kazi hiyo. Bodi ya wahandisi wakishirikiana na IET na ACET wamfuatilie mhandisi wao. Hawa wote watoe taarifa itakayotolewa kwa wananchi.
Serikali kuu iangalie kwa undani taratibu za kutoa vibali vya ujenzi na usimamizi wa ujenzi. Mfumo tulionao tumeurithi toka kwa wakoloni, pengine kuna haja ya kuungalia tena. Manispaa zibanwe kuhakikisha kuwa watendaji wanapewa nyenzo za kufanya kile wanachopaswa. Ni aibu kuwa na building inspektaz wasio na usafiri (ingawa kwa hapa hilo halipo maana wangeweza kutembea kutoka ofisini kwao).
Sioni haja ya tume. Wasi wasi wangu ni bodi na mamlaka husika kuanza kunyosheana vidole na kutafuta ujiko kutokana na hii calamity.