Je, watendaji wa mitaa/ vijiji au mabalozi wa nyumba 10 wangalitumika kama makarani wa sensa, zoezi la sensa lingalikamilika ndani ya siku moja tu?

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,953
4,326
Nilikuwa nawaza tu kwa sauti (just thinking aloud):

"Kuna kama kusua sua kwa zoezi hili la sensa ya watu na makazi kwenye baadhi ya maeneo. Kuna uwezekano baadhi ya kaya zisiweze kufikiwa ndani ya muda uliopangwa wa siku saba. Kuna kaya ambazo makarani wa sensa watazikuta zimefungwa kwani wanakaya watakuwa kwenye pilika pilika zao.

Jee tungalitumia mabalozi wa nyumba kumi au watendaji wetu wa mitaa/ vijiji hatungaliweza kweli kuzifikia kaya zote nchini ndani ya siku moja tu? Kwani hawa wangalishindwa kutumia hivyo vishikwambi baada ya mafunzo? Wangaliweza hata kujaza hizo takwimu manually kwenye jedwali lililoandaliwa ambazo baadaye zikaingizwa kwenye vishikwambi".

Hawa watendaji wa mitaa/ vijiji ni waajiriwa wa serikali na hivyo figisu figisu tunazozisikia zikitokea kwa baadhi ya makarani wa sensa hazingalitokea. Hawa wanazifahamu sana kaya zilizo kwenye maeneo yao.

Hata namba za simu za wakuu wa kaya wanazo na hivyo hizo takwimu za sensa wangaliweza kuzipata hata kwa njia ya simu tu.

Mojawapo ya kazi za watendaji hawa ni kutunza hizo takwimu kwenye maeneo yao na kuzi update mara kwa mara, na si kusubiri hadi baada ya miaka 10.
 
Hata kama ingefanyika zaidi ya siku moja wangeweza kutoa nakala kwa kila mwanachi kujaza na kisha kuzituma huko NBS
Nilikuwa nawaza tu kwa sauti (just thinking aloud):

"Kuna kama kusua sua kwa zoezi hili la sensa ya watu na makazi kwenye baadhi ya maeneo. Kuna uwezekano baadhi ya kaya zisiweze kufikiwa ndani ya muda uliopangwa wa siku saba...
Japokuwa ni vizuri pia na vijana walambe asali ya nchi
 
Nilikuwa nawaza tu kwa sauti (just thinking aloud):

"Kuna kama kusua sua kwa zoezi hili la sensa ya watu na makazi kwenye baadhi ya maeneo. Kuna uwezekano baadhi ya kaya zisiweze kufikiwa ndani ya muda uliopangwa wa siku saba.
Ilikuwa lazima iwe hivi ili watu wapige hela. Pia tangu uchaguzi mkuu wa 2020 kuna vijana wengi wa CCM walioahidiwa mema ya nchi ambayo hawakuyapata hadi walianza kuwa wakabaji huku mitaani hivyo zoezi hili lilitumika kuwapoza ndiyo maana wote waliopewa ajira hii ya muda ni wanaccm tupu.
 
Hata kama ingefanyika zaidi ya siku moja wangeweza kutoa nakala kwa kila mwanachi kujaza na kisha kuzituma huko NBS

Japokuwa ni vizuri pia na vijana walambe asali ya nchi
Wamelamba asali ya kiasi gani?
 
Mojawapo ya kazi za watendaji hawa ni kutunza hizo takwimu kwenye maeneo yao na kuzi update mara kwa mara, na si kusubiri hadi baada ya miaka 10.

 
Ilikuwa lazima iwe hivi ili watu wapige hela. Pia tangu uchaguzi mkuu wa 2020 kuna vijana wengi wa CCM walioahidiwa mema ya nchi ambayo hawakuyapata hadi walianza kuwa wakabaji huku mitaani hivyo zoezi hili lilitumika kuwapoza ndiyo maana wote waliopewa ajira hii ya muda ni wanaccm tupu.
Mhhh, kumbe
 
Shida ya hao ulio wataja wanachangamoto kadhaa ikiwemo kutokujua kusoma na kuandika kwa baadhi yao. Niliwah shiriki ktk zoezi fulani ktk ngazi ya kata tulikuwa tuna wahusisha na wenyeviti wa serikali za mitaa na wajumbe wao. Aisee unakuta ni mama mtu mzima lkn kusoma ni issue
 
Shida ya hao ulio wataja wanachangamoto kadhaa ikiwemo kutokujua kusoma na kuandika kwa baadhi yao...niliwah shiriki ktk zoezi fulani ktk ngazi ya kata tulikuwa tuna wahusisha na wenyeviti wa serikali za mitaa na wajumbe wao ...aisee unakuta ni mama mtu mzima lkn kusoma ni issue
Ni nadra sana (negligible) kukuta balozi wa nyumba 10 au mwenyekiti wa mtaa/ kijiji asiyejua kusoma na kuandika. Hao watendaji wa mitaa/kijiji niliowataja elimu yao ni ya ngazi si chini ya diploma, na wengi wao wana degree zinazohusiana na utawala wa serikali za mitaa.
 
Ni nadra sana (negligible) kukuta balozi wa nyumba 10 au mwenyekiti wa mtaa/ kijiji asiyejua kusoma na kuandika. Hao watendaji wa mitaa/kijiji niliowataja elimu yao ni ya ngazi si chini ya diploma, na wengi wao wana degree zinazohusiana na utawala wa serikali za mitaa.
Utendaji wa kata na mtaa highest level of education ni diploma ...degree holder ni over qualification unless mtu awe na diploma kisha na iyo degree yake awe nayo tu lkn huwezi kuombea kazi ya utendaji wa mraa au kataa ila Afisa Tarafa ndio being degree holder ni requirement.
 
Anna Makinda ni old fashioned lady nilijua atashindwa tuu kama alivyo shindwa NHIF ambako amepewa u mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi.
NHIF iliyoanza vizuri sasa hivi imedorora huduma zake na kuwa sio Bima tena
 
Back
Top Bottom