Je, Wasanii wa nchi hii wanatumiwa na watawala wetu kama askari wa kukodiwa?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Tumeshuhudia wasanii wote wenye majina makubwa wasiopungua 200, wakishiriki kwa pamoja kwenye tamasha lililoandaliwa na CCM, katika uwanja wa Uhuru hapo jana, kwa kile kiliichoitwa tamasha kubwa kabisa la kimuziki, kwa wasanii hao wote wanaodaiwa kuwa ni mashabiki wakubwa na wanaiunga mkono CCM katika uchaguzi mkuu ujao, unaotarajiwa kufanyika mwezi wa October mwaka huu.

Wengi wetu tutakuwa tunajua kuhusu hao wanaoitwa askari wa kukodiwa, au kwa jina lingine wanaitwa mamluki, ambao kwa lugha ya kiingereza wanaitwa "mercenaries" kwa tabia zao za kupenda pesa na wako tayari kwa atakayewapa pesa watakayoridhika nayo kupigana kwa yeyote, hata kama watafahamu kuwa hao wanaotakiwa kupigana nao ni ndugu zao wa kuzaliwa, ili mradi tu umewapa pesa watakayokubaliana nayo kwa ajili ya kazi hiyo!

Hiyo ndiye tabia ya "mercenaries" kuwa wapo tayari kupigana na adui yeyote, ilimradi yule aliyewakodi, atakuwa ameweka mezani "kibunda" ambacho wataridhika nacho.

Hiyo tabia ya "mercenaries" siwezi kuitofautisha na wasanii wetu waliojitokeza kwa wingi pale uwanja wa Uhuru ili kuwaunga mkono CCM, katika kuwakandamiza wazalendo ambao maisha yao yameathirika vibaya kutokana na utawala huu wa CCM wa miaka yote 60 baada ya Uhuru.

Tunajua kabisa tabia ya wasanii wa nchi yetu kuwa huwa hawaendi kwenye "show" yoyote kabla ya kuwekewa donge nono, ambalo wenyewe watakuwa wamekubaliana nalo, ndipo hapo wanapotokea kwenye onyesho hilo.

Hawa jamaa tunawajua kwa tabia yao kuwa hawana mapenzi na mtu, bali kinachopendwa ni pesa tu, ndiyo itakayoamua kuwa waende kwenye onyesho hilo au laa.

Kutokana na tabia hiyo ya wasanii wetu, kwa hiyo tunakuwa na uhakika kuwa CCM "imekamuliwa" pesa za kutisha ili kuwaleta kwa pamoja wasanii wakubwa wote tuliowaona jana.

Kwa upande wa ile "nyomi" iliyojazana pale katika uwanja wa Uhuru, hao CCM wasichukulie kuwa ule umati wote uliojazana pale kiwanjani, kuwa ni wafuasi wao na wenye ukereketwa wa kindakindaki wa chama chao cha CCM, bali ule umati ulijazana pale uwanjani kuja kuwashangaa kina Diamond na Ali Kiba katika show hiyo ya bure na wala sivyo watakavyokuwa wanachukulia viongozi waandamizi wa CCM kuwa ule umati wote ni mashabiki wao wa CCM!
 
Tumeshuhudia wasanii wote wenye majina makubwa wasiopungua 200, wakishiriki kwa pamoja kwenye tamasha lililoandaliwa na CCM, katika uwanja wa Uhuru hapo jana, kwa kile kiliichoitwa tamasha kubwa kabisa la kimuziki, kwa wasanii hao wote wanaodaiwa kuwa ni mashabiki wakubwa na wanaiunga mkono CCM katika uchaguzi mkuu ujao, unaotarajiwa kufanyika mwezi wa October mwaka...
Wanalipwa kwa kazi zao; usidhani wanatumiwa bure.

Chama chochote kinaweza kuwakodi kufanya hivyo hivyo mradi kiwalipe stahiki yao.
 
Huo unaoeleza Mkuu Kichuguu ni uwongo wa dhahiri!

Chadema hata waje na kibunda cha kiasi gani, hao wasanii wataogopa "ku-perform" kwa woga tu wa kushughulikiwa!
Hakuna ushahidi wowote; mwaka 2015 waliperform kwa CHADEMA na kwa CCM. Wanajua kabisa jinsi ya kumtumikia kafiri wapate mradi wao.

Asante kwa kuniita mwomgo.
 
Mwaka huo unaousema hukumbuki kuwa nchi yetu ilikuwa inaruhusu vyama vya upinzani?
Basi mzee! Hhata hivyo nasisitiza kuwa hakuna mtu aliyeleta taarifa kuwa chama cha upinzani kimemkodi msanii kwenye shughuli zao akakataa kwa kuogopa serikali. Ni speculations tu.
 
Sijui kama "mercenaries" inaweza kuwa jina sahihi kwa hao wasanii. Sababu sifa kuu ya "mercenaries they are outsider to the conflict" ?

Maana yake si wanufaika na magomvi yenu wanachohitaji ni ngawila tu. Ndiyo maana wanakodiwa toka nje.

Sasa sijui kama Wasanii wetu hawa si wanufaika na uchaguzi wa Rais wao.
 
Basi mzee! Hhata hivyo nasisitiza kuwa hakuna mtu aliyeleta taarifa kuwa chama cha upinzani kimemkodi msanii kwenye shughuli zao akakataa kwa kuogopa serikali. Ni speculations tu.
Ni ukweli usiopingika, waki preform kwenye shughuli za upinzani.

1. TRA wanawapa Bill ya miaka 10 nyuma.

2. Uhamiaji wanagundua kuwa si raia wa Tanzania.
 
Basi mzee! Hhata hivyo nasisitiza kuwa hakuna mtu aliyeleta taarifa kuwa chama cha upinzani kimemkodi msanii kwenye shughuli zao akakataa kwa kuogopa serikali. Ni speculations tu.
Nakubaliana na wewe kwa asilimia zote. Lakini unafikiri kuna mtu atathubutu kusema siwezi kumpigia kampeni Hashimu Rungwe kwa mfano kwasababu naogopa vitisho vya sirikali? Weee ukiulizwa ushahidi utasemaje?
 
Nakubaliana na wewe kwa asilimia zote. Lakini unafikiri kuna mtu atathubutu kusema siwezi kumpigia kampeni Hashimu Rungwe kwa mfano kwasababu naogopa vitisho vya sirikali? Weee ukiulizwa ushahidi utasemaje?
Anaweza asimpigie kwa sababu ya masoko. Kwa mfano Hashim akitaka pafomensi moja tu kwa shilini millioni mbili, lakini CCM wakawa wamehahid kumpa pafomensi 10 kwa sh miliini 15, ni wazi anaweza kupima biashara yake akaona kuwa CCM kuna mshiko zaidi ya Hashim.
 
Ni ukweli usiopingika, waki preform kwenye shughuli za upinzani
1. TRA wanawapa Bill ya miaka 10 nyuma
2. Uhamiaji wanagunduua kuwa si raia wa Tanzania.
Ni ukweli usoopingika kuwa serikali hii inatumia kila aina ya vitisho ili kuendelea kubaki madarakani.........

Huo ndiyo mchezo ambao umezoekeka kwa immigration, wale wasanii ambao watakuwa tayari ku-perform katika shughuli za Chadema, wataambiwa wao siyo raia wa nchi hii, bali warudi "kwao" Congo waende waka-perform
 
Back
Top Bottom