Je, unaziona ndoto zako rohoni?

Je, unaziona ndoto zako rohoni?

asante kututoa usingizini


kuna hii ndoto ni mbishi sana (PESA) yaani hii inaringa utazani mwanamke mwenye msambwada.
Hahahaa,inaringa kwasababu sisi wenyewe ndo hatuwazi 'mwanzo wa kufikia kupata' kiukamilifu,hii hatua hua mara nyingi haidumu kwa muda mrefu kwenye fikra aisee,yaani ukianza tu kupanga plan kabla haija kamilika vizuri automatically tu tunajikuta 'mwisho wa matokeo ya kupata na kutumia' (hapa sasa ndo tunajikutaga tunatabasam automatic tuuuu)hahaaa
 
giphy.gif
 
Bro, niliota usiku mimi na wife tumepata mapacha wa kike ila wakawa wameshikana vidole then mmoja kati ya ndugu akasema usijali wataacha nishwa, then baadae wakawa wamwachanika katika hali nzuri na afya , hii ina maana gani bro kama unajua
Mshana Jr
 
Utimilifu wa ndoto katika maisha ya mafanikio huanzia rohoni na si mafanikio tuu bali kila jambo katika maisha bila kujali uzuri ama ubaya wake! Kwakuwa roho ndio asili na ndio chanzo cha kila kitu katika ulimwengu wa mwili?

Je unaziishi ndoto zako? Ama bado hazijatimia? Je unaziona ndoto zako katika uhalisia wake! Ni kama vile upandavyo mazao kondeni.. Unajiona tangu maandalizi ya shamba, kupanda palizi kukomaa na hatimaye mavuno! Utimilifu wa ndoto..! Je unaiona hii picha kwa vipande? Hatua kwa hatua?

Hapa tofautisha ndoto hizi za rohoni na ndoto zile za kichwani. Ndoto za Alinacha. Ndoto za kuota una pesa mingi bila mipango, unaendesha ndinga kali unachukua bebes za viwango, kasri lenye kila aina ya starehe nknk.. Sio ndoto hizi ambazo waotaji wake hawawazi mwanzo wa kufikia kupata bali wanawaza mwisho wa matokeo ya kupata na kutumia..ndio maana ziko kichwani juu na sio rohoni ndani!

Unataka kuwa nani maishani.. Unataka kufanya nini maishani. Hiyo roadmap utaiona rohoni mwako kila uendapo, kila ufanyalo na hata katika usingizi na uchovu mwingi utajiona wewe katika uhalisia wako ndani ya hizo ndoto zako

Haijalishi utachelewa muda gani kuzifikia Kila mmoja wetu ana muda wake wa kupata. Wengine wanachelewa na wengine wanawahi. Sometimes ni heri kuchelewa lakini ufike milele kuliko uwahi kisha ufeli kabla kesho haijapambazuka. Kuchelewa kupata utakacho ni maono pia.

Usiishi kwa kihoro cha kuchelewa kutimiza ndoto. Usibabaike na waliokutangulia.. Jenga msingi wako rohoni ukitumainia yajayo. Lakini usibweteke ila usitumie mkato pia. Usiyalazimishe mafanikio yako kupitia njia zisizo sahihi. Usitumie kafara na nguvu za giza. Utapata kwa wakati huo. Lakini itakapofika kupata kwa halali. Haramu itakuwa imeshanajisi njia yako na anguko lako litaanzia hapo.

Maisha sio leo maisha ni kesho na kesho ni kubwa kuliko Jana, kuliko juzi, kesho ni kaka mkubwa wa leo. Usibweteke ila ziishi ndoto zako katika njia sahihi. Hata kama hujapata na hata kama muda haujatimia lakini ishi kwenye maandalizi ya KUWA utakaye kuwa!
Dressing code yako
Matendo yako
Mienendo yako
Maono yake vyote viashirie utakayekuwa baadae. Haijilishi ndoto zako ni kuwa
Mama wa nyumbani anza sasa
Msanii mkubwa anza sasa
Kiongozi mkubwa anza sasa
Mfanyabiashara mwenye mafanikio anza sasa
Mtu maarufu anza sasa
Paroko, Sheikh, mchungaji anza sasa
Mtunzi maarufu anza sasa
Mwanasayansi na jasusi anza sasa!

Kuna baadhi ya ndoto za rohoni hujidhihiri kwa watoto wadogo tangu mwanzo.. Maana matendo na mienendo yake huchora ramani inayoonekana!

Kumbuka hakuna ndoto za rohoni zinazojifunua uwe
Tena
Malaya
Jambazi
Mdangaji
Tapeli
Mwizi
Muongo nknk
Hayo ni matendo ya giza baada ya ndoto kufa kwa sababu zozote zile!

Kama kila ukijiangalia mawazoni kuna mahali unatamani kuwa lakini rohoni unaona kiza..achana na hizo fikra.. Hutafika popote..

Nawatakia Jumamosi njema ya Pasaka
Jr[emoji769]
16.04.2022
Nishayaona sana rohoni na nikafanya jitihada lakini hamna kitu
 
Kila nikianza urafiki na Mshikaji yeyote yule tukawa close hasa urafiki wa kikazi rafiki huyo anafanikiwa mm nabaki palepale.
Cha kushangaza Mara baada ya kufanikiwa urafiki unakufa,na sababu ya urafiki kufa ni gap LA kipato baina yetu linaloweka barrier.
Nasononeshwa na hali hii kiasi naogopa kuwa na rafiki sasa,nifanyeje hali hii isiwepo???
 
Bro, niliota usiku mimi na wife tumepata mapacha wa kike ila wakawa wameshikana vidole then mmoja kati ya ndugu akasema usijali wataacha nishwa, then baadae wakawa wamwachanika katika hali nzuri na afya , hii ina maana gani bro kama unajua
Mshana Jr
Kuota ni lazima kwakuwa ndoto ni sehemu ya maisha ya kiroho.. Lakini si kila ndoto ina impact ama ina tafsiri fulani.. Ni mpaka ijirudie zaidi ya mara moja ama iwe vivid
 
Kila nikianza urafiki na Mshikaji yeyote yule tukawa close hasa urafiki wa kikazi rafiki huyo anafanikiwa mm nabaki palepale.
Cha kushangaza Mara baada ya kufanikiwa urafiki unakufa,na sababu ya urafiki kufa ni gap LA kipato baina yetu linaloweka barrier.
Nasononeshwa na hali hii kiasi naogopa kuwa na rafiki sasa,nifanyeje hali hii isiwepo???
Unaweza kuwa kiroho wewe ni daraja la kuwavusha wengine ..Ila muda wako ukitimia nawe utajivushs
 
Kuota ni lazima kwakuwa ndoto ni sehemu ya maisha ya kiroho.. Lakini si kila ndoto ina impact ama ina tafsiri fulani.. Ni mpaka ijirudie zaidi ya mara moja ama iwe vivid
Ohh!Kumbe ndoto ikijirudia hua inamaanisha,mi nlikua napuuzia.

Em nambie hii inaweza kuwa na maana gani,inajirudia sana hii ndoto,inansumbua sana.

Kipindi cha nyuma nliwahi kumfanyia mtu kazi (ni baba,ana family ya mke na watoto 2)ni mwanajeshi,anavaa v3),lakini ktk malipo alinidhulumu 330k.Kuna siku nkamkumbusha akanijibu'usinifosi kukulipa,ukirudia tena kunikumbusha siku lipi.'basi mi sijawahi kumkumbusha mpaka leo ni miaka miwili yupo kimya. Huwa najiuliza sana,kwanini anidhulumu wakati uwezo wa kunilipa anao na katka kazi me nayeye hatukuwahi kuwa na tofauti au mgogoro wowote jamani?

Tangu mwezi wa6 mwaka jana nimekua nikiota bado natumikishwa kwenye ileile kazi na huyu boss wangu. Hii ndoto inanisumbua sana,kwa mwezi naiota mara 6.Yan hata alhamis ya juz nimeiota.
 
RAISI AJAYE SIJUI NITAPENYEA WAPI WAKATI HATA UBUNGE BADO HALAFU 34 YEARS!!!AISEH!!HALAFU KUNA KELELE NAFSINI ETI NIKASOME MASTERS KITU AMBACHO NISHACHUKIA ELIMU YA BONGO KABISA NAONA INAJAZA WAJINGA WENGI AMBAO WANAWAZA VYEO TU!!!!AISEH!!!
Kasome wewe acha ujinga,fursa inaeza kuja hicho kigezo kikakutoa nje 🤣🤣🤣
 
Ohh!Kumbe ndoto ikijirudia hua inamaanisha,mi nlikua napuuzia.

Em nambie hii inaweza kuwa na maana gani,inajirudia sana hii ndoto,inansumbua sana.

Kipindi cha nyuma nliwahi kumfanyia mtu kazi (ni baba,ana family ya mke na watoto 2)ni mwanajeshi,anavaa v3),lakini ktk malipo alinidhulumu 330k.Kuna siku nkamkumbusha akanijibu'usinifosi kukulipa,ukirudia tena kunikumbusha siku lipi.'basi mi sijawahi kumkumbusha mpaka leo ni miaka miwili yupo kimya. Huwa najiuliza sana,kwanini anidhulumu wakati uwezo wa kunilipa anao na katka kazi me nayeye hatukuwahi kuwa na tofauti au mgogoro wowote jamani?

Tangu mwezi wa6 mwaka jana nimekua nikiota bado natumikishwa kwenye ileile kazi na huyu boss wangu. Hii ndoto inanisumbua sana,kwa mwezi naiota mara 6.Yan hata alhamis ya juz nimeiota.
Pole sana .. Sorry to say this Lakini asilimia 90 kuna kitu cha kishitikina ulijaribu kufanyiwa kwenye hiyo kazi
 
Pole sana .. Sorry to say this Lakini asilimia 90 kuna kitu cha kishitikina ulijaribu kufanyiwa kwenye hiyo kazi
dah!!Sawa ngoja nimwachie mungu tu.

Na je! Mtu akiota anasali na kukemea mapepo hua inamaanisha nini?(hii nayo inanijia mara nyingi sana tokea january ya mwaka huu)yaan hata kama nimchana tu usingzi unipitie,inakuja hii ndoto.
 
Back
Top Bottom