Je, unaweza kumwambia Mwenzi wako ukweli kuwa yeye sio Mke/Mume wa ndoto yako?

May Day

JF-Expert Member
May 18, 2018
6,162
8,820
Ingawa baadhi yetu twaweza kuleta ubishi juu ya hili lakini ni ukweli unaowakuta zaidi ya asilimia 80 kama sio 90 ya Wanandoa wamejikuta wameoana kutokana na sababu moja au nyingine, wengi ikiwa ni baada ya kuona miaka inasonga bila kupata Mwenza anayekidhi ndoto zake.

Binaadamu yeyote mwenye mipango ni lazima atakuwa na mipango ya namna anavyotamani aishi siku za usoni, miongoni mwa mipango hiyo ni kupata Mke/Mume wa aina fulani, kimuonekano, asili yake, imani yake n.k.

Huenda nyote wawili mnalijua hilo lakini hakuna anayethubutu kuweka hisia zake hadharani ili kutomkwaza Mwenza wake.

Labda kwa zile ndoa zinazoingia kwenye misukosuko ya mara kwa mara inayopelekea kutoleana maneno makali yasiyojali hisia za mwingine.

Bila shaka mpo wengi mnaoweza kukiri kuwa hamuishi na Wenza wa ndoto zenu.

1623414365143.png
 
Unaweza ukawa unamkubali mwanzoni akabadilika si unajua binadamu ana tabia mbili ya kabla na ya baada ya ndoa
Mkuu akibadilika inategemea amebadilika kitu gani, kama ni mambo madogo madogo ya kuwekana sawa ni kawaida maana hakuna mkamilifu

Ila akianza kuleta mambo mengi yenye kuzingua daah aisee hakuna mbili Kwenye moja.....unaachana nae tu
 
Aisee kukaa na mtu ambaye humkubali moyoni daah itakufanya usienjoy ndoa kabisa ani
Ila ndoa nyingi zipo hivyo.

Kuna wakati labda ungemtamani Mwanamke fulani Mtaani, Kazini au kwenye sehemu fulani ya huduma unapokutana naye lakini kutokana na kukosa sifa fulani, labda ya uwezo wa kifedha, tofauti ya kielimu, kuwahiwa na mwingine n.k. unaishia kuona kwa macho tu.
 
Mkuu akibadilika inategemea amebadilika kitu gani, kama ni mambo madogo madogo ya kuwekana sawa ni kawaida maana hakuna mkamilifu

Ila akianza kuleta mambo mengi yenye kuzingua daah aisee hakuna mbili Kwenye moja.....unaachana nae tu
Wengi ubadilika kulingana na hali, mazingira, kipato isipokuwa wenye Mungu ndani yao awabadiliki
 
Ila ndoa nyingi zipo hivyo.

Kuna wakati labda ungetamani Mwanamke fulani Mtaani, Kazini au kwenye sehemu fulani ya huduma unapokutana naye lakini kutokana na kukosa sifa fulani, labda ya uwezo wa kifedha, tofauti ya kielimu, kuwahiwa na mwingine n.k. unaishia kuona kwa macho tu.
Kuna tofauti kati ya kutamani na kupenda mkuu

Kutamani ni kawaida hata ukiwa na mtu umeridhika nae kabisa ila unaweza ukaona kitu fulani kwa mtu ukamuelewa kwa wakati huo

Ila swala la ndoa inabidi ujitahidi hata mtu unayekua nae asipofikia 100% ya vigezo vyake basi walau awe na kuanzia 80%--90% ya vigezo ili usizidishe tamaa nje
 
Back
Top Bottom