MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,224
- 22,306
Kuna vitu na mambo yanayopendwa sana hapa duniani ambavyo sio dhambi lakini ni kuwa hivyo vyote havitakuwepo. Kwa mfano sisi tunaopenda misosi mitamu kama ile ya Shishi food, white rose na Marry brown ni kuwa haitakuwepo. Kitu nachosikia kinatajwa tajwa ni maziwa na asali. Pia huenda kikawepo chakula kiitwacho MANA walichopewa wana wa Israel jangwani. Kiukweli bado haijathibitishwa chakula gani kitakuwepo huko ila uhakika ni kuwa hizi biriani, pilau, makange, nyama choma, kitimoto rosti na vingine pendwa havitakuwepo. Kama unakula hakikisha unakula kwelikweli. Huko tuendako havitakuwepo.
Wale wapenzi wa mpira wa miguu mtambue pia nayo pia haitakuwepo. Kama kuna timu unaipenda hakikisha unaishangilia sana ukiwa hai. Kwa sisi wakristo tunaambiwa starehe kubwa itakuwa kuimba mapambio ya kusifu. Yaani shughuli kuu huko ni kusifu na kuabudu. Hata wale wapenda hela wajue kuwa dhahabu na almasi zitakuwa sio chochote kwa sababu hizo biashara hazipo.
Je, nini kifanyike? Biblia kupitia Mhubiri 9:10 inasema chochote utakachopata kufanya kifanye kwa nguvu zako zote kwa sababu huko uendako hautapata nafasi ya kukifanya. Lakini Je, ni wakati sasa wa viongozi wetu wa dini kubadili maneno ya hamasa kwenye kuhimiza safari ya kwenda mbinguni? Wenzetu nasikia wanasema tukifika huko tutakabidhiwa mabikra kadhaa. Hii kiukweli ni hamasa yenye uhalisia.
Wale wapenzi wa mpira wa miguu mtambue pia nayo pia haitakuwepo. Kama kuna timu unaipenda hakikisha unaishangilia sana ukiwa hai. Kwa sisi wakristo tunaambiwa starehe kubwa itakuwa kuimba mapambio ya kusifu. Yaani shughuli kuu huko ni kusifu na kuabudu. Hata wale wapenda hela wajue kuwa dhahabu na almasi zitakuwa sio chochote kwa sababu hizo biashara hazipo.
Je, nini kifanyike? Biblia kupitia Mhubiri 9:10 inasema chochote utakachopata kufanya kifanye kwa nguvu zako zote kwa sababu huko uendako hautapata nafasi ya kukifanya. Lakini Je, ni wakati sasa wa viongozi wetu wa dini kubadili maneno ya hamasa kwenye kuhimiza safari ya kwenda mbinguni? Wenzetu nasikia wanasema tukifika huko tutakabidhiwa mabikra kadhaa. Hii kiukweli ni hamasa yenye uhalisia.