Tanzania 1
Senior Member
- Oct 4, 2007
- 197
- 24
Hebrew,
Hata nami nilisikia kuwa col. Urio alifariki. Huyu alitukuta, nasi tulimkuta col. Meena.
Mnaukumbuka wimbo wa "Malela, Malela, Malelaaa, ... Malela, Malela, Male nakutafuta!!"? Tuliambiwa kuwa Huyu Malela alikuwa ni kuruta (msichana, nadhani). Siku moja alitoka yeye na kuruta mwenzake (naye ni msichana, nikumbukavyo) kwenda kwa "Babu". Njiani walikutana na kibibi kizee ambacho kilikuwa kinauza miwa. Malela na rafikie walikuwa wanataka kununua miwa.
Kwa kuwa miwa ilikuwa michache, yule bibi akamwambia Malela akachukue miwa ndani ya kibanda cha bibi ambacho kilikuwa jirani. Malela akaenda, na akakawia sana kurudi. Baada ya yule rafikiye kumsubiri kwa muda mrefu, ikabidi amuulize yule bibi. Bibi akamwambia : "Mbona rafiki yako alishaondoka muda mrefu sana! Hukumuona! Aliondokea kule kule kibandani".
Ilipofika jioni yule rafikie Malela hakumuona Malela. Alipoulizia kwa kuruta wengine, wakamwambia kuwa walikuwa hawajamuona kwa muda mrefu. Wasiwasi ulipomzidi, aliripoti suala la kutoweka kwa Malela kwa Sir Major. Walitumwa wanajeshi wakiongozwa na rafikie Malela kwenda ktk tukio. Walipofika, walishangaa kutokuta kibanda, kinyume na alivyosimulia rafikie Malela.
Mara kwa mara, inasemekana kuwa, rafikie Malela alikuwa akimuona Malela, lkn alipowaonesha wengine, hawakumuona! Hiki ndicho kisa cha kuzuka wimbo huu.
Mmh! Sijui km ni cha kweli au la.
Hata nami nilisikia kuwa col. Urio alifariki. Huyu alitukuta, nasi tulimkuta col. Meena.
Mnaukumbuka wimbo wa "Malela, Malela, Malelaaa, ... Malela, Malela, Male nakutafuta!!"? Tuliambiwa kuwa Huyu Malela alikuwa ni kuruta (msichana, nadhani). Siku moja alitoka yeye na kuruta mwenzake (naye ni msichana, nikumbukavyo) kwenda kwa "Babu". Njiani walikutana na kibibi kizee ambacho kilikuwa kinauza miwa. Malela na rafikie walikuwa wanataka kununua miwa.
Kwa kuwa miwa ilikuwa michache, yule bibi akamwambia Malela akachukue miwa ndani ya kibanda cha bibi ambacho kilikuwa jirani. Malela akaenda, na akakawia sana kurudi. Baada ya yule rafikiye kumsubiri kwa muda mrefu, ikabidi amuulize yule bibi. Bibi akamwambia : "Mbona rafiki yako alishaondoka muda mrefu sana! Hukumuona! Aliondokea kule kule kibandani".
Ilipofika jioni yule rafikie Malela hakumuona Malela. Alipoulizia kwa kuruta wengine, wakamwambia kuwa walikuwa hawajamuona kwa muda mrefu. Wasiwasi ulipomzidi, aliripoti suala la kutoweka kwa Malela kwa Sir Major. Walitumwa wanajeshi wakiongozwa na rafikie Malela kwenda ktk tukio. Walipofika, walishangaa kutokuta kibanda, kinyume na alivyosimulia rafikie Malela.
Mara kwa mara, inasemekana kuwa, rafikie Malela alikuwa akimuona Malela, lkn alipowaonesha wengine, hawakumuona! Hiki ndicho kisa cha kuzuka wimbo huu.
Mmh! Sijui km ni cha kweli au la.