sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,033
Binafs nakumbuka kulikuwa na mtoto flani wa kipare alikuwa kanizikimikia sana yani, ilikuwa ni chuoni miaka kama 8 iliyopita.
Basi mimi nnikavimba sana kichwa nikawa namletea mapozi flan ivi ili nioneka kidume ambacho ni ndoto ya wanawake, si mnajua tena vijana wadogo kwa kupenda sifa, Nakumbuka aliwahi kunizawadia peni kabla ya mtihani, kadi ya birthday, t shirt, n.k loh nikiri kusema kwamba nilikuwa bongela fara kwa kumpuuza.
Muda huo nilikuwa na girlfriend mwengine, huyo ambae alikuwa anafanya juhudi sana niwe nae nilikuwa napotezea flani ivi, ilikuwa sana sana ni stories chache.
Sasa siku nakuja kuambiwa na washkaji yule dem ambae namletea mapozi kaingia kingi kwa jamaa flani ivi, nikapuuza nikidhani ni stori tu, siku ikafika kwa macho yangu naona kwenye canteen sehemu ya kula chakula kweli dem yupo na jamaa mpya alafu wana furaha ile mbaya, jamani sikuingia humo nilienda moja kwa moja gheto, Niliumia sana, yani nilipatwa na wivu acha kabisa, nilihisi kaa la moto limepitishwakwenye moyo wangu.
Yule dem niliekuwa nae kimapenzi hata meseji zake zikiingia sijibu kabisa hata apige simu sipokei maana naugulia maumivu, kiukweli nisidanganye mwanaume mzima machozi yalinilenga.
Niliatwa na stress kama ya wiki hivi, maana karibu kila siku nilikuwa nawaona pamoja kitu ambacho kilikuwa kinaniuma sana.
Anyway, baada ya mwezi hivui kuna siku nilikaa nae uso kwa uso na nikamwambia nilchopitia, na jinsi ilivyonivuruga akili,