Je tuhahitaji tena Ze Utamu?

Je tuhahitaji tena Ze Utamu?

Status
Not open for further replies.
Itafutwe server ya utamu, kisha ifungiwe.
Hamna haja ya kuendelea kuichekea tovuti hii ya kijinga.
Waswahili wanasema ukicheka na mbwa atakufuata msikini, pia mchelea mwana kulia hulia yeye.
 
Itafutwe server ya utamu, kisha ifungiwe.
Hamna haja ya kuendelea kuichekea tovuti hii ya kijinga.
Waswahili wanasema ukicheka na mbwa atakufuata msikini, pia mchelea mwana kulia hulia yeye.

Mkuu kufungia haiwezi kuwa ufumbuzi, sababu zitaibuka nyingine nyingi tu (as long as the guys behind this are still kicking aroubd in the streets).
Watafutwe popote walipo ijumuishe waendeshaji wa moja kwa moja na wawezeshaji wengine.
They can't be that smart!
 
100% ninaafiki hawa wapuuzi wakamatwe mara moja na kupewa adhabu kali sana. Nadhani jana nilitoa hint za kutosha za kuweza kuwakamata wahusika. Nilitoa IP address, location, na muhusika alisoma chuo gani na college ID yake ilikuwa ni nini?.


Kidatu

Unafanya watu humu watoto wadogo. Hizo unazoziita wewe ni "hint" hakuna lolote. Kama kweli unawafahamu huyo/ hao wahusika basi tuma e-mail/fax/piga simu polisi uwasaidie na kazi yao hii [ya kuwatafuta ze utamu] ya kijinga; hapo utakuwa umesaidia hela yetu ya kodi isipotee bure.

Jeshi la Polisi ni lazima wawasiline na "mmoja wapo" wa host wa hiyo website ambaye kwa sasa ukiwa U.K anaonekana ni theplanet.com. Zaidi ya hilo, wewe huna namna yoyote ya kuwajua wahusika (unless ni ndugu yako/jamaa/rafiki/rafiki wa rafiki n.k) lakini sio kwa kutumia sijui ip tracer.
 
100% ninaafiki hawa wapuuzi wakamatwe mara moja na kupewa adhabu kali sana. Nadhani jana nilitoa hint za kutosha za kuweza kuwakamata wahusika. Nilitoa IP address, location, na muhusika alisoma chuo gani na college ID yake ilikuwa ni nini?.

Acha ujinga na utoto wewe! unataka nikufungulie thread alaaah
 
hiyo picha ya kikwete iko wapi? mbona mi sijaiiona? au ndo wameogopa nakuiondoa???? Naombeni link.
 
Maadili unayaona leo?
mbona hapa yanabadikwa mapicha machafu machafu hamuoni kama ni kinyume na maadili yatu watz......

Yo yo nasikia una hizo picha za kikwete can u please send me nione. thanks
 
Napenda kuungana na wana JF wenzangu kullani kitendo cha ZE UTAMU kubandika barua ya kumdharilisha mheshimiwa raisi wetu. Siwezi epuka kumlaumu MODERATOR /Administrator wa hi blog (kama yupo) kwa kutoibandua mapema hiyo picha kama ilibandikwa yeye akiwa hana habari. Napenda kuelimishwa, huuyu Mkuchika ana madaraka vilevile ya kufungia blogs?? Tumemsikia mara anakimbilia kufungia magazeti yakianika kashifa za VIGOGO lakini yakiaandika kashifa za walala hoi wana hana habari. Magazeti ya udaku utakuta yamepiga picha za maiti wa ajali za gari / mitumbwi lakini Mkuchika kimya!! Nina hasira naweza sema vibaya!!!
 
Meza panadol Mama mdogo maumivu ya kichwa hauanza pole pole!

Labda ninywe RED BULL nipate nguvu nyingi hata kutwanga mtu!!! Ila tu naogopa sheria kuchukua mkondo wake. Mambo mengine yanatia hasira ati, wana JF tuwe tunaombeana kheri kwa MUUMBA wetu maana hizi shughuli za kupambana na MAFISADI na Wabadhilifu wa maadili ni nzito!!!
 
Labda ninywe RED BULL nipate nguvu nyingi hata kutwanga mtu!!!

Ohhh my Goodness! Do you know the side effects of RED BULL....immunostimulants...Red Bull wil give you more than just wings....usiipende sana ....labda baba mdogo !
 
- Inaonekana kuingia bungeni kwako ndio mwanzo na mwisho wa dunia, samahani sio wote wenye hizo ndoto, ni zako tu! sisi tunatafuta hela kwanza siasa itakuja baadaye hatuna haraka nayo kama wewe!

- Na kama kuna bunge duniani linaloweza kuigiliwa kwa njia hii basi hilo sio bunge ila ni kilabu cha pombe cha walevi walevi hivi, hapa tunatota maoni yetu kulingana na ishu iliyopo mezani, na sio lazima wote tuwe na mawazo kama yako mkuu, ya kufurahia hii picha isiyo na heshima kabisa mbele ya jamii!

- Wazee wetu kama Society zetu, wengi hawajui kama Europe na US ni mabara tofauti, Nigga kwa akwaida huwa hajui kama Africa ina nchi zaidi ya 45, huwa anafikiri ni nchi moja tu, kama wazee wetu huamini kuwa mbongo yoyote anayeenda Ulaya, ni lazima akutane na wabongo wengine, huwa hawajui kwamba kuna nchi nyingi mbali mbali na miji tofauti na sio rahisi kwa wabongo walioko majuu kuonana, na sisi mabingwa wa Internent tunaofahamika na jamii hapa tumelowa maji machafu kwa sababu sio rahisi kuwashawishi wanaotusikia na Internent kwamba hatuhusiki na haya ya ajabu, tukipita sasa itkuwa huyu naye ni wa huko Internent ni fedheha kubwa sana kwa sisi wastaarabu na wapenda ukweli, hizi za picha zingekua za ukweli isingekuwa taabu,

- Narudia tena kwamba leo ni siku ya giza kwangu binafsi, sikutegema kwamba one day katika uhai wangu, kama M-Tanzania niliyelelewa kizalendo, niliyezaliwa bongo na kutahiriwa kitamaduni kijijini kwetu, na kufundishwa madhara ya utawala wa mkoloni nikiwa Primary School, nikafundishwa namna ya kujitegemea nikiwa Secondari, nikafundishwa kufanya kazi nikiwa JKT, nikaenda Ulaya na kujionea faida za kutopitia utumwa katika maisha yangu kama weusi wa US, kama wa-Surinam wa Holland, kama weusi wa Arabuni. Mwalimu akanipa elimu kuhusu utaifa wangu, akanipa nationality, akanipa ID, baada ya miaka 14 majuu siku moja nikarudi bongo nikiwa nimeelewa uzuri na utamu wa maisha yangu ya kibongo na mapungufu yake, na uzuri na mapungufu ya maisha ya majuu, bado bongo ni tambarare, lakini kwenda majuu na kurudi nyumbani na this kind of education, ya kumuweka uchi kiongozi wa taifa kama alivyofanyiwa leo ni aibu yetu wananchi wote wa Tanzania, licha ya wale tu tunaoingia kwenye mitandao.

- Kwa wale mnaoshangilia ni haki yenu, isiyokuwa haki yenu ni ku-question haki za wengine kutoshangilia, mnachotakwia kutufundisha hapa kwenye uwanja huu wa Great Thinkers ni vipi this thing inaweza kutusaidia taifa na maendeleo yake, na hasa vipi hii new ideology yenu inakwenda samba samba na masilahi yetu kitaifa.

- Kumbuka kwa shujaa huenda kilio, lakini kwa muoga siku zote huwa ni kicheko!

FMES!

Well said FM ES. Keep it up. Hatuwezi kumdhalilisha kiongozi wa nchi. Hapa tuweke tofauti ya itikadi pembeni tuongee habari za maadili na malezi. Achana na mapungufu ya kiongozi wetu mkuu huyu, of all anahitaji heshima yake.
 
Computer scientists ,Hivi kuna njia yoyote ile ambayo inaweza kumgindua mwenye Blog kama hajajitambulisha? Kwa sababu ya uelewa wangu mdogo wa mambo ya networking naona kama vile mtu anaweza kuwa South Africa alfu aka-register kwenye blog na kusema yuko South America.

Kitendo kilichofanywa na Ze utamu sio kizuri kabisa na hakikustaili kufanywa na mtu mwenye akili timamu. Sijui jeshi la polisi litatumia njia gani kuwapata hao wamiliki.
 
Napenda kuungana na wana JF wenzangu kullani kitendo cha ZE UTAMU kubandika barua ya kumdharilisha mheshimiwa raisi wetu. Siwezi epuka kumlaumu MODERATOR /Administrator wa hi blog (kama yupo) kwa kutoibandua mapema hiyo picha kama ilibandikwa yeye akiwa hana habari. Napenda kuelimishwa, huuyu Mkuchika ana madaraka vilevile ya kufungia blogs?? Tumemsikia mara anakimbilia kufungia magazeti yakianika kashifa za VIGOGO lakini yakiaandika kashifa za walala hoi wana hana habari. Magazeti ya udaku utakuta yamepiga picha za maiti wa ajali za gari / mitumbwi lakini Mkuchika kimya!! Nina hasira naweza sema vibaya!!!

Mama mdogo punguza hasira. Tatizo ni kwamba kufungia blog ni ngumu kidogo kuliko kufungia magazeti. kama unakumbuka mwanzoni Ze utamu ilikuewa inaitwa The Utamu. kwa hiyo hata akifungia ze utamu inaweza kuja kwa jina jingine. kinachotakiwa administrator wa hii blog waweke some kind of restrictions kwa watu wanao post hizi picha.
 
Jeshi la polisi kutumia resources za walipa kodi kuwasaka wamiliki wa ze Utamu na hatimaye kuwatima mabaroni au LAA itakuwa ni kutumika vibaya kwa rasilimali hizo. Nashangaa kuona kuwa tumelia sana na majambazi, tumelia sana na ndugu zetu Albino kuchunwa hatukuwahi kusikia kuwa Jeshi la polisi linashirikiana na akina so and so kuwabaini wauwaju wa Albino, mpaka Mh. alipoamuru washukiwa washukiwe na mawe mpaka kufa na alipoambiwa atoe kauli aliamua kmwaga chozi ndio serikali ikaja na utaratibu wa kuwafanya wachache watengeneze pesa kwa kuratatibu zoezi la upigaji kura za siri kuwabaini watuhumiwa. Ningekuwa Mh. Rais ningemwambia mwandishi wangu kuwa awatangazie waTz kuwa mheshimiwa Rais ansema hiyo picha ni ya kutengenezwa na hahusiki na lolote lile wala hawaombi wahusika kuomba msamaha, wala hataamuru chochombo chochote kinachotumia kodi ya wanachi kumtafuta mhusika, naawaombeni wananchi mrudi kwenye kazi zenu hasa kipindi hiki cha mwanguko wa uchumi kidunia, Asanteni sana.

Kesho hiyo story isingekuwa story tena ingekuwa imekosa maana kabisa.
 
Jeshi la polisi kutumia resources za walipa kodi kuwasaka wamiliki wa ze Utamu na hatimaye kuwatima mabaroni au LAA itakuwa ni kutumika vibaya kwa rasilimali hizo. Nashangaa kuona kuwa tumelia sana na majambazi, tumelia sana na ndugu zetu Albino kuchunwa hatukuwahi kusikia kuwa Jeshi la polisi linashirikiana na akina so and so kuwabaini wauwaju wa Albino, mpaka Mh. alipoamuru washukiwa washukiwe na mawe mpaka kufa na alipoambiwa atoe kauli aliamua kmwaga chozi ndio serikali ikaja na utaratibu wa kuwafanya wachache watengeneze pesa kwa kuratatibu zoezi la upigaji kura za siri kuwabaini watuhumiwa. Ningekuwa Mh. Rais ningemwambia mwandishi wangu kuwa awatangazie waTz kuwa mheshimiwa Rais ansema hiyo picha ni ya kutengenezwa na hahusiki na lolote lile wala hawaombi wahusika kuomba msamaha, wala hataamuru chochombo chochote kinachotumia kodi ya wanachi kumtafuta mhusika, naawaombeni wananchi mrudi kwenye kazi zenu hasa kipindi hiki cha mwanguko wa uchumi kidunia, Asanteni sana.

Kesho hiyo story isingekuwa story tena ingekuwa imekosa maana kabisa.

Labda hana uhakika je? Aseme tu, zikiwekwa na nyingine je?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom