7/7: Mfumo unaogopa nini? Je ni Hitilafu ya mfumo?

7/7: Mfumo unaogopa nini? Je ni Hitilafu ya mfumo?

Joined
Jun 19, 2026
Posts
11
Reaction score
19
Salute

Kila mfumo wenye kujiamini huona sauti za wananchi kama sehemu ya afya ya taifa. Lakini mfumo wenye hitilafu huona kila swali kama tishio, maandamano kama uadui, na kila ukosoaji kama uhaini.

Uhuru wa kuandamana si zawadi ya serikali; ni sehemu ya haki ya wananchi kusikika. Tatizo huanza pale mamlaka yanapoanza kuogopa watu wanaotaka kueleza hisia zao.

7/7 haitakiwi kuwa vita ya wananchi na viongozi, bali iwe kipimo cha kama mfumo wetu una uwezo wa kusikiliza au bado unaishi kwa hofu. Hitilafu Ya Mfumo
 
Mfumo uliwauwa ndugu zetu hapo October 29 wakiwa majumbani mwao.
Mfumo ulipika.data za matokeo ya uchaguzi. Hapakuwa na uchaguzi kwa sababu ya mfumo
Mfumo unaruhusu watu kutekwa, kuwawa na kulawitiwa ( polepole, kibao na wengine)
Mfumo mbovu
 
Mfumo uliwauwa ndugu zetu hapo October 29 wakiwa majumbani mwao.
Mfumo ulipika.data za matokeo ya uchaguzi. Hapakuwa na uchaguzi kwa sababu ya mfumo
Mfumo unaruhusu watu kutekwa, kuwawa na kulawitiwa ( polepole, kibao na wengine)
Mfumo mbovu

Mfumo umepata hitilafu. Mfumo unapiga shot na kudhuru watu na wengine kuuawa. Mfumo ubadilishwe
 
Natamani sana serikali iwaache hiyo siku mkafanye uharibifu na uporaji kama mlivyopanga alafu tuone nani atakuwa kaumia ni mfumo au nyie walalahoi.

Mtapigana sana wenyewe kwa wenyewe huko mtaani. Mtaanza kama maandamano, mtaanza kuibiana mali then mtaangukia kwenye kupigana wenyewe.
 
Naona defender zinazunguka tu huku mtaani, kila nikitoka lazima nikutane nazo.

Polisi wanaogopa hawataki tutimize haki yetu kikatiba, wanatumia silaha walizonunua kwa kodi zetu ili watuumize.
 
Natamani sana serikali iwaache hiyo siku mkafanye uharibifu na uporaji kama mlivyopanga alafu tuone nani atakuwa kaumia ni mfumo au nyie walalahoi.

Mtapigana sana wenyewe kwa wenyewe huko mtaani. Mtaanza kama maandamano, mtaanza kuibiana mali then mtaangukia kwenye kupigana wenyewe.
Hii ramli umejifunzia wapi?
 
Mfumo umepata hitilafu. Mfumo unapiga shot na kudhuru watu na wengine kuuawa. Mfumo ubadilishwe
Mfumo umejaza mapolisi wenye mitutu ya bunduki kwenye mabarabara
Lengo la mfumo ni kuwatisha waja wa mungu?
Juzi tu walikuwa wakipiga magoto kuomba kura Leo wananchi wamegeuzwa MAADUI
Salaaale
Mfumo huu
 
Back
Top Bottom