Yani ni kukosa eshima kumfananisha Iran na Mrusi. Yani ukitaka kujua warusi wanaleta balance of power hapa Duniani basi angalia kule Syria ndege za Israel zilivyokuwa zinashambulia kutokea mbali wala uwezi kuta zinaingia ndani ya Syria, ni kwa sababu ya mifumo ya kirusi japo walikuwa na mifumo ya muda ila imefanyiwa update.
Iran walitaka kuziwa mfumo S-300 na s-400 ila wakajifanya wajanja wakanunua baadhi wakaenda kufanyia utafiti kisha wakatengeneza za kwao zinazofanana na zile za Warusi.
Warusi wakasema aina shida sisi sio milima ipo siku maji na mafuta vitajitenga.na kweli mifumo yao imeonekana kuwa walipoteza pesa na muda. Sasa ivi wanataka kurudi tena kwa Mrusi na kwenda kwa mchina kununua ndege.
Kupambana na Israel ni lazima uwe na Anti air missile za kutosha pia fighter aircraft za maana ili ndege zikutane angani ila kama zikitokea zimepenya basi zinakutana na SAM. Hapa lazima uwe na Mig 31, mig 35, SU-35, Su-57.
Mfano mzuri kule F-16 inavyoshindwa kufua dafu Ukraine
Hapo umetoa maelezo kimihemko na kishabiki tena sana.
-Sawa hatuwezi kumfananisha Iran na Urusi,ila HUWEZI ukamdogosha Iran kwa namna hiyo.
Tukianzia na mifumo ya ulinzi wa anga ya Iran Khordak na Bavar-373 imeonesha ufanisi kuliko hata mifumo ya ulinzi mathalan Iron dome.Tukio la shambulizi la Israel dhidi ya Iran 2024 Oktoba lilionesha uwezo wa ulinzi wa anga wa Iran.
Pia ukija kwa tukio hili la sasa tambua kuwa Israel imetumia mashushushu kuharibu miundombinu ya ADS ya Iran iliyopelekea miundombinu mingi kufeli na kushindwa kulinda anga.
Tambua Iran ni taifa lenye vikwazo since 1979 ila kwa alipofikia amejitahidi sana.
Hiyo Russia yenyewe iliwahi kutoa sapoti kwa IRAQ dhidi ya IRAN vita ya Iraq-Iran war ya 1980-1988 lakini Iran ikasimama imara.
Hiyo Urusi vikwazo ilivyowekewa na EU dhidi ya vita na Ukraine Urusi ilishaanza kutepeta kiuchumi,kama sio CHINA kuisaidia Urusi kwa financial aid basi Urusi isingesimama.
Hata hizo S-400 zilizopo Urusi zilishindwa kuzuia drones za Ukraine ziliposhambulia ndani ya Urusi.
Sawa sio sahihi kumfananisha Urusi na Iran,ila SIO SAWA KUMDOGOSHA IRAN kama ulivyodai mkuu.
Maelezo yako yapo too biased.