Je, Panya Road wamewashinda? Wamerudi kwa kasi ya kutisha sana

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Oct 31, 2014
5,360
11,514
Jamaa yangu anaishi Makubuli anasema hawa watu wamerudi kwa kasi kubwa,ari na guvu kubwa sana. Wanaweza pora nyumba mpaka 20 kwa usiku mmoja. Ni vijana wa umri wa miaka 12-30 wanakuwa wengi wakiwa na mapanga ,visu ,magongo na bisibisi. Kiukweli wameuteka mji wa Dar es Salaam. Nadhani kwa hiki kipindi ambacho polisi wapo mapumziko tutapata shida sana. Mpaka wakimaliza likizo Polisi hali itakuwa tete. Tuuombe Mungu sana.

Serikali yetu sikivu yenye kutujali na kutupenda je bado hamjapewa hizi habari? yaani kuna watu washavamiw ana kudhuriwa zaidi ya mara tatu na wakiepeleka taarifa polisi wanawaambia "wewe siyo mtu wa kwanza kushambuliwa na hao vibaka andika maelezo tutafuatilia" inaishia hapo. imekuwa ni jambo la kawaida na polisi haw aamabo tunawalipa mshahara wanaonekana kutoshtushwa kabisa na jambo hili. tunaomba serikali kwa kweli iingilie kati suala hili kwa ajili ya usalama wa wapiga kura wake na wachangia kodi.

Jamani sisi wananchi wote tukiuliwa nchini wakabaki panya road penye yao ninyi viongozi nani atawachangia kodi ambayo ndiyo inawasaidia kuzunguka nchini kwenye helkopta kuhamasisha anuani za makazi? au kwenda kuzinduliwa huko Ulaya na Marekani? Tumsaidie Rais wetu jamani mbona kama kila kitu mmemuachia yeye tu. yeye uzinduzi , yeye kusafiri kujielezea, yeye kila kitu ninyi mnafanya nini?
 
Mtaa unapaswa uwe na Ulinzi shirikishi,
Kama hauna,
Wanaume wa mtaa huo hasa wababa wa familia waitishe kikao cha dharura kuwakabili hao wahuni.

Itafaa akipatikana mmoja Kati ya kumi WA mfano ambaye mtamuadhibu Kwa kiwango cha juu kabisa ambacho itakuwa funzo Kwa wengine.
Kiwango cha juu ndio kiwango gani mkuu, ama wawanyang'anye mapangayao harakaharaka.😆😆
 
Undeni vikundi vyenu vya ulinzi shirikishi mjilinde wenyewe acheni uoga.

Halafu hao ni vijana wenu mnaishi nao huko kwenu huenda hayo ni matokeo ya malezi mliyowapa, jiulizeni mlikosea wapi.
Maranyingi hivi vikundi havitoki mtaa husika! Huwa wanaama wanaenda kufanya matukio na eneo ambalo haishi wala kupiga stori! Labda utapata mmoja tu wakutoa raman katika ao 20

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Miaka ya nyuma kwetu mburahati kuna mtindo ulitumika wa kuwa na list ya watoto wote walioshindikana basi walikuwa wanapita kila nyumba na kuwachinja mikono hata kumaliza kabisa ila kipindi hiko mrema alikuwa wazili wa ulinzi.watu mpaka wakakimbia
 
Kunakipindi walichomwa pia lakini bado wanarudia labda kuwachoma sio sawa wakamatwe wapelekwe kwenye vyombo vya sheria ili sheria ichukue mkondowake.😎
Najua kuwachoma moto is extreme and too much lakini lazima itafutwe namna ili wakitaka kufanya tena wajiulize mara mbili, lakini wale mbwa nasikia hawaibi tuu na kupora wanaua watu pia, fire for fire
 
Serikali itoe silaha kwenye uongozi wa serikali za mitaa kwa ajili ya kutengeneza operation ya kuwadhibiti hawa.


Nasema hivyo kwasababu sungusungu wenye marungu na panga ni ngumu kudhibiti kundi la panya road maana kwa hesabu ya haraka wanakuwa hadi 40 afu mmoja kati yao anakuwa na gun

Zipo habari kwamba hawa watoto wanapewa silaha za moto na baadhi ya matajiri kwa hiyo kama unafikiria ku solve hii ishu kwa silaha ya panga utakuwa unajidanganya.

Serikali ikitoa hizo silaha naamini haitakuwa tena jambo la kuwasubiri wapite ndio muwashambulie, hiyo itakuwa ni special operation ya kuwafata kokote walipo na pindi unapomkamata mmoja bana pumbu na prise mpaka ataje kikosi kizima.
 
Nyie ni waoga.

Waambie hao wahuni waje huku Chuga.
Unapaswa kujua kuwa Dar es salaam ni sehemu ambapo Ina kila aina ya watu wanaotoka mikoani

Wababe wapo dar,
Wachezaji wa mpira wazuri wapo dar
Riadha,boxing,wanamuziki wazuri wapo Dar

Wavivu wengi,wapo Dar,watu laini laini wapo hapa

Hivyo niseme tu hakuna mjanja wa mkoa anaweza kushindana na watu wa Dar
 
Back
Top Bottom