Je, ni kweli kuwa Utajiri unapatikana Shambani?

Nyabukika

JF-Expert Member
Jun 15, 2022
1,402
942
FpPdXdWWYAIhbg3

Hayawi hayawi sasa yamekuwa, mpango wa kuwawezesha vijana kwa kuwapa ujuzi na mahitaji ya kuwawezesha kuanza shughuli za kilimo unakwenda kubadili hostoria ya Afrika.

Kupitia mpango huu wa BBT, kila kijana anapata fursa ya kuijenga kesho yake iliyo bora. Wakati suala la ajira likiwa changamoto katika nchi zote za Afrika, Rais Samia ameweka rekodi ya kuwa kiongozi wa kwanza kuja na muarobaini wa suala la ajira kwa kuwawezesha vijana kujikwamua kiuchumi kupitia kilimo.

Mpaka sasa zimetengwa takribani Hekari 162,492. Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi thabiti wa Rais Samia imejikita katika kuwawezesha wananchi zaidi.

Katika hatua ya kwanza mashamba yametengwa katika Mikoa ifuatayo; Mbeya (Hekari 52,165), Dodoma
(Hekari 20600), Kagera (Hekari 3227) na Kigoma (Hekari 86500). Mpango wa BBT ni endelevu na utafika kila kona.

Sanjari na uwezeshaji huu, serikali inaendelea kutoa pembejeo kwa wakulima wote, msamaha wa kodi kwa malighafi za kilimo, kuiwezesha Bodi ya Nafaka kwa fedha za kutosh, kutafuta masoko ya kimataifa, kuwawezesha Maafisa Ugani nchi nzima, kuboresha miundombinu ya usafirishaji wa mazao na kudhamini tafiti muhimu kwa sekta ya kilimo.

Tanzania ina ardhi nzuri inayofaa kwa kilimo takribani Hekta Milioni 13 na nusu, hivyo uwekezaji mkubwa unaofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan utakuwa wa kihistoria na wenye kumgusa kila mtanzania moja kwa moja au vinginevyo, hususani vijana.
 
Serikali imefanya jambo jema kuwawezesha vijana kufanya shughuli za kilimo, itasaidia kupunguza vijana wasio na kazi vijiweni
 
Mjinga wa akili ndio atakaye amini hizo janja janja,serikali za kipigaji zilijifanya zinapenda kilimo kumbe wizi mtupu,kumbukeni ile ya kilimo kwanza.
 
Ni kweli kabisa ila kwetu bado sababu ubepari wa ardhi kwenye ukulima ujifika.
Kwetu nchini mkulima ni maskini mwenye shamba la hekari ila ulaya ni mtu tajiri na anasikirizwa sana na serikali.
 
Back
Top Bottom