Watu dizaini hii ndio wakifa wanaacha watoto wao wanakuwa machokoraa au changudoa.
Hutaki mkeo arithi mali zako, unataka nani arithi? Hivi kwani mali za mwanamke huwa za nani baadaye?
Uzoefu wangu katika maisha ni kuwa kipaumbele cha mwanamke yeyote ni watoto wake. Ndicho hata tunacholalamikia wanaume kuwa wake zetu wanajali watoto kuliko kutujali sisi (of course hatupendi hali hii), lakini ni uhakikisho kuwa hata nikifa mke wangu ataendelea kuwajali wanae ambao ni watoto wangu. Kwahiyo njia bora kuliko zote ya kuhakikisha urithi unawafikia watoto ni kumwachia mama yao (unless umeoa single mother akaja na watoto wengine ambao sio wako, hapo sasa ni wewe tu na uchoyo wako kama hutaki mtoto wa mwanaume mwenzio arithi mali zako, lakini kwa hakika mama atapigania wanaye).
Mtoto wa kike unamnyima urithi, na umemwacha ana miaka 15, si changudoa huyo unatengeneza? Umekataa kurithisha mkeo ukarithisha ndugu zako eti wakuchungie mali waje wamkabidhi mwanao wa kiume, uzoefu unaonyesha mali hizo huliwa, by the time mwanao anapata akili anakuta hakuna kitu kilichobaki vimekombwa vyote! Au ndugu zako wanamwekea zengwe mkeo wanamfukuza na wanao, wanaenda kuzurura wanageuka machokoraa huko.
Nyenyere acha ujima, mambo hayo yamepitwa SANA na wakati. Ndoa ni ushirika wa kudumu, na akifa mmoja anabaki mwingine kutunza watoto kama wapo. Kama hamna watoto bado mkeo ana haki ya kurithi vyote mlivyokuwa navyo pamoja, ndiyo kumbukumbu yako aliyobaki nayo.