Je, ni halali mke arithi mali mumewe akitangulia?

Je, ni halali mke arithi mali mumewe akitangulia?

Bias.

Hujawa objective. Hujaeleza hasara za mfumo wa kwanza. Hujaeleza faida za mfumo wa pili.

Hujaeleza hiyo shida ilianza kutokea lini na kwanini. Hujaeleza mfumo upi unaendana na mazingira ya sasa ya kuchanganyikana na utandawazi.

Imebidi niishie katikati kwasababu there is no way unaweza kuwa na objective conclusion kama analysis yakl.iko biased hivyo.
 
Haya ya urithi niyaweke kwanza kando, ndoa ni muunganiko wa wewe na mkeo na sio ukoo wenu. Huo ukoo ndio uliojaa nyumbani kwa yule mwimbaji hadi dada wa watu akakumbuka mirungi akaenda kwao
 
Mkuu kwenye kuthamini watoto wa jinsia zote bila kubagua tupo pamoja.

Endapo hii sehem ya mwisho niliyoinukuu ni ya kweli na unaiamini, naona watoto wanachohitaji sana kutoka kwetu ni malezi bora na elimu basi. Mali na mengine watajitafutia zakwao.
Kwa kuongezea tu, kama uwezo upo, wote tu watoto, wadogo na wakubwa zako, wazazi na hata ndugu wa karibu ni vizuri kuwasaidia hasa elimu, ndiyo urithi namba moja. Mali na mengine kabisa kabisa wajitafutie za kwao.
 
TAASISI YA NDOA, haina fomula hata kidogo.....mshirikishe Mungu unayemuamini.......kweli wazazi wana nafasi nzuri ktk kushauri mke mwema, but suala la kunichagulia bado ni tatizo.....mr Nyenyere najua una hoja ya msingi...na hata wachangiaji wana hoja zao.....ila hakika kila mmoja atapata la kujifunza kutoka pande zote,,,, mleta hoja, wachambua hoja na wapinga hoja.....
 
Yaani unaoa kwa kufuata maelekezo ya wazazi? Kwani lazima wampende? Au wanakusaidia kutomba.a?
Oa kwa ajili yako na sio kwa ajili ya wazazi au mtu mwingine.

Mimi nilioa nikiyetaka mimi.

Wazazi wako walifanya jukumu la kukulea
Na kwanini mambo ya ndoa yanapokusumbua unawahusisha? kuto...a sio kazi pekee ya ndoa! Na dhana kama hizi ndio zile zipatikanazo kwa wale ambao nyumba zao zimewashinda!! Ya kuambiwa changanyanya na yako!!
 
Mtoa mada umenigusa kwa kweli 80% ya uloyaandika ndio mim nayopitia naishi na mwanamke lakan upande Wa Mke na upande wangu hakuna mawasiliano
 
Na hapa ndipo penye tatizo, kusoma kusiondoe maarifa. Wazazi wanafanya mambo kwa experience, wameishi miaka mingi, wamepitia mengi. Wakati wewe ndio kwanza unajiandaa kuingia kwenye ndoa na elimu yakko na akili zako za darasani, wao wako karibu kabisa kuiaga dunia baada ya kuishi miaka mingi kwenye ndoa. Wao wana elimu kubwa ya maisha lich ya degree zako.

Huwezi kuwazidi wazazi experience, ongelea mambo ya kazi na elimu ya darasani. Usiqadharau wazazi mkuu, wana mchango katika maisha. Pia kumbuka mtoto hakui kwa wazazi.

Sijasema udharau wazazi, nimesema usiwasikilize kwa kila kitu maana dunia ya leo sio sawa na ya zamani, wazazi kuwazidi experience kwenye lipi hasa? kuna mambo nawazidi experience na mambo mengine wananizidi, ni kitu obvious, ila kusema wao wana siri sijui za ndoa ni maneno tu mnajidanganya, ndoa nyingi watu wa zamani wanavumiliana tu, siku hizi unaona nyingi zinavunjika sababu wanawake wamepata voice, hawakai wakaonewa wakaendelea kukaa tu, zamani walikua wakionewa wanakua wapole tu hawafanyi lolote, wanaendelea kuishi kibishi. Hayo sio maisha ya kuishi. Unakufa 80-90years old, umeishi na mume miaka 50, kati ya hiyo 50 furaha ulikua nayo only 10% of the time, wakati mwingine ilikua shida tu, we only live once, mambo ya mwanamke kukaa ana-waste maisha yake kumvumilia mwanaume ni total bullshit bora angeondoka tu, what a waste of life seriously. I've seen first hand wazazi wanagombana mzee anapiga mwanamke na mwanamke anarudi tu coz hana choice, anadepend on the guy, mwanaume anaenda ku-cheat anarudi hata na magonjwa ya zinaa ndani, mwanamke anaendelea tu kuvumilia, is this the bullshit unachotaka tukae nacho tukivumilie? coz I promise you fuatilia utagundua ndoa nyingi za zamani wanaume ndo walivyo, tena karibia zote.

Wapo waliofanikiwa kuishi vizuri ndiyo kwa amani miaka yote, ni mfano mzuri ila ni wachache sana. Kukaa ukachukulia wazazi kama vile mwisho wa mambo utaishia kua mama boy miaka nenda rudi. Nashukuru wazazi walinikuza, wakanifundisha mema na mabaya, wakanipa elimu, ila ni wakati sasa wa kutumia akili zangu mwenyewe na sio kusikiliza kila wanachosema, wao nao wana tamaa pia, ni binadamu kama wengine. We leo upeleke mchumba wako wakwambia hawamtaki na wewe utasema tu "ndiyo mzee"? bila kujua hata sababu?
 
Nadhani hujaelewa hata nilichoandika. Hakuna sehemu hata moja nimeandika mke ni adui kama chui, soma kwa uwazi. Nimelinganisha mifumo ya maisha kwa wana ndoa tu. Hiki ulichoandika ndio huo mfumo wa kizazi kipya chenye ubinafsi



Huo ni mtazamo wako ambao ni ule wa haki sawa. Why? Unaposema mkeo ni other half maana yake yeye si msaidizi tena, ni mwana hisa ambaye amewekeza asilimia 50 kama wewe nsdani ya ndoa. Hiyo haimaanishi hata kidogo kwamba ndio unamwamini zaidi kuliko wale wanaomchukulia mke kama sehemu ya ukoo wao. Tofauti kati ya huo mfumo wako na ule wa awali ni kuwa unajijengea ukoo wako mbali ni kuendeleza ukoo toka kwa wazazi, unakuwa umejitenga na jamii pana. Ni modern view ambapo mwanamke na mwanamume wako sawa kwa kila kitu ingawa hii ina defy natural law.



Hakuna atakaye kuoa mke mjinga, lakini wengi wa mtazamo wako wamekuja kulia majuto makuu. Process ya kupata mke mwema ni zaidi ya kupambana peke yako, inahitaji guidance, tena mke mwema anategemea malezi uliyolelewa ili kuweza kumtambua.

Watoto kufanya biashara wakifika kwenye 20s ni haja ya kila mzazi, ama wapate ajira. Kikubwa ni kuwa wajitegemee, na huo ndio mfumo wa awali ambao kwa kiasi kikubwa ulifanya hayo kwa ufanisi. Leo hii zimebaki wishful thinking tu kwa sababu mfumo wa sasa hausapoti kwa kiasi kikubwa mtazamo huo. Watoto wanafika umri huo wakiwa hawajitambui, hawana mtazamo wa future, wanatamani mwaishi kama kina Ja Rule huku hawana mbele wala nyuma. Wanashindana kukariri mashairi ya hiphop tu.

Unaposema hawahitaji hela za wazazi unakuwa umetoka nje ya mada. Kwani mzazi akifariki akaacha mali zake hupelekwa wapi? Kwenye NGO au kwenye taasisi za watoto yatima? Mtazamo huo ni wa kizazi kipya, disjointed usio na mtazamo mpana wa ukoo. Ni kama mtu anayeishi kisiwa cha peke yake akianzisha uzao wake. Ukweli ni kwamba kuna wakati mali za wazazi itabidi ziendelezwe hasa pale wanapokuwa wameacha mfumo mzuri wa kibiashara.



Hebu mtazame Bhahresa na mali zake, unadhani anaishi kwa mtazamo wako wewe kuwa watoto watafute mali zake na wamwache yeye wasihubutu kumwingilia? Je, ukoo wa Bharesa hawahusiki kwenye utajjri wake? Hayo ni mawazo ya maskini kuwa nikipata mali mtu asiniingilie. Hakuna anayekuingilia kwenye mali isipokuwa una mtazamo hasi.

Unapokosea ni pale unapotazama habari ya kugawana urithi, mimi naongelea kuendeleza mali za ukoo. Siku hizi kwa sababu ya ubinafsi kila mtu anajitazama yeye, hata hao watoto wako wanaweza kugombania hizo mali na mama yao kiasi pasibaki hata kijiko. Mzazi mwema ataacha mfumo mzuri wa kibiashara ama mfumo endelevu, ili watoto wafit naturally katika huo. Hakuna habari ya ndugu kurithi mali, bali ni mali iendelezwe. Ndivyo ilivyokuwa, sio kuuza ili wagawane, watoto walisimamia moja kwa moja.

Mambo ya kumwamini mke, yalikuwa na nguvu sana kwa mfumo wa zamani, sasa hivi ni hadithi tu mkuu, wake wa leo hawatoki makwao. Ukifikia kuoa utalijua hili, lakini kubwa zaidi unatafuta mali ili ukiondoka uwaache wanao sehemu nzuri, uache legacy ndani ya ukoo. Kama unaunda ukoo wako kupitia mwanamke basi sawa, lakini kama unaendeleza ukoo, mkeo atakuwa sehemu muhimu ya ukoo wenu, tena hutathubutu kuwaambia ndugu mniache na mke wangu.

Anyway, ni mtazamo wako mkuu ambao ndio modern view.

Kuna sehemu tunapoint sawa ila kuna sehemu hatuwezi elewana kabisa. Sisemi ukoo ni kitu cha kutupilia mbali, ila ukikaa ukaishi kua kila kitu kifanywe kiukoo utaishia kufa maskini coz mtaishia kurudishana nyuma tu, kama ukoo una watu smart na wao wote wana goal la kuendeleza company ikakua then haina shida kabisa kufanya kazi pamoja, ila kukaa unafanya kazi na ndugu just because ni ndugu hata kama hawastahili then ni ujinga, same goes for watoto, sawa unaweza waachia mali na mfumo mzuri kuhakikisha kampuni inaendelea, ila sio kulazimisha kuwapa kila kitu kwa kua tu ni damu.

Ulivyoandika unamchukulia mke kama vile mtu katoka tu huko kaja kukuingilia, hadi unafika kuoa doesn't that mean umeshamchunguza na kukaa naye vya kutosha kujua kama ni sahihi au la? Mke unaoa wewe alafu unataka ndugu ndiyo wakae wanam-monitor wakupe report kama anafaa au hafai?

Mwanamke na mwanaume wako sawa ndiyo ila sio unavyofikiria wewe, kila mtu anajua biologically tupo tofauti, mwanaume hatoweza kuzaa hata siku moja, na mwanamke hatoweza kua as strong kuliko mwanaume, ndiyo natural law hiyo, ila apart from that tukija kwenye vitu kama nani anastahili nini, hakuna kumtenga mwanamke sababu tu yeye ni mwanamke, hakuna cha natural law hapo, ni construct tumeweka wenyewe tu kua mwanamke atafanya kazi hizi na mwanaume hizi, hata kama ni kitu any sex anaweza fanya.

Naungana na modern view kwenye mambo mengi (sio yote) kwa kua imeprove kufanya vizuri, anayesema zamani was better anatudanganya tu, kwenye human history hakuna wakati mzuri kama leo, miaka ya zamani kulikua na shida tupu, wanawake kuonewa, watu kuuana ovyo, world war, ubaguzi wa rangi ulikua wazi wazi, mwanamke alikua anakua treated kama slave majumbani, alafu unasema kau things worked well before? what before are you talking about? Generation hii mtu yeyote anauwezo wa kua na kufanya chochote anachotaka, sawa kuna mapungufu ila sio makubwa kama zamani. Wazee hua nashangaa sana wanvyokaa kulaumu this generation kisa tu wamesikia habari mbili tatu mbaya, wanasahau generation yao ilikua ni habari mbaya kila siku.
 
Hebu nieleweshe mkuu. Maana urithi wa asili ni wa sura, tabia na mambo utakayomrithi wa/mzazi wako tu vinginevyo chagua wewe neno linalokupendezea. Ndiyo, mke wangu atanirithi na si wa/mwanangu. Tafuta chako.
Kurithi ni pale unapokufa. Nadhani utazikwa na mali zako, pole sana. Umepotea ama huelewi maana
 
Bias.

Hujawa objective. Hujaeleza hasara za mfumo wa kwanza. Hujaeleza faida za mfumo wa pili.

Hujaeleza hiyo shida ilianza kutokea lini na kwanini. Hujaeleza mfumo upi unaendana na mazingira ya sasa ya kuchanganyikana na utandawazi.

Imebidi niishie katikati kwasababu there is no way unaweza kuwa na objective conclusion kama analysis yakl.iko biased hivyo.
Ungesaidia kueleza hayo, ndio maana ya mjadala. Lakini kwa sababu umesoma ukiwa na pocha fulani ndio maana umehukumu hivyo. Good for you.
 
Haya ya urithi niyaweke kwanza kando, ndoa ni muunganiko wa wewe na mkeo na sio ukoo wenu. Huo ukoo ndio uliojaa nyumbani kwa yule mwimbaji hadi dada wa watu akakumbuka mirungi akaenda kwao
Si kwa maana hiyo mkuu, hujaelewa. Kuunganisha ukoo kunaletwa na ndoa ya watoto. Maana yake mnachangia damu, ila watoto wanakwenda kuendeleza ukoo. Sio kujaza ndugu nyumbani, haimaanishi hilo.
 
Kwa kuongezea tu, kama uwezo upo, wote tu watoto, wadogo na wakubwa zako, wazazi na hata ndugu wa karibu ni vizuri kuwasaidia hasa elimu, ndiyo urithi namba moja. Mali na mengine kabisa kabisa wajitafutie za kwao.
Nadhani hatujaelewana dhana ya urithi. Labda niulize, watoto wako wakitafuta mali zao lakini mwosho wa siku ukifariki hizo mali zako utazikwa nazo? Hatuongelei kugawa mali kwa watoto, tunaongelea pale unapoacha mali zifanyiwe nini.

Kuna tatizo kwenye jamii ambapo watu wanatazama urithi kama kugawana mali, si kweli. Tutazame ule mwisho, sio tamaa za hivu karibuni kutaka kila mtu apate japo kijiko. Mfano una kiwanda kidogo, halafu umekufa na wosia wako kwamba watoto watafute malo zao binafsi, jna maana kiwanda kiende serikalini? Hapo ndipo ilipo hoja yangu
 
TAASISI YA NDOA, haina fomula hata kidogo.....mshirikishe Mungu unayemuamini.......kweli wazazi wana nafasi nzuri ktk kushauri mke mwema, but suala la kunichagulia bado ni tatizo.....mr Nyenyere najua una hoja ya msingi...na hata wachangiaji wana hoja zao.....ila hakika kila mmoja atapata la kujifunza kutoka pande zote,,,, mleta hoja, wachambua hoja na wapinga hoja.....
Kwa watu wa kada ya chini (kwa kipato) ni kweli unayosema. Sasa hivi vijana wanakwenda na trend, hivyo akili zimekuwa programmed kuona mambo kama media zinavyotaka. Hata definition ya urembo inabadilika na wakati, ni mambo ya kupita. Siku za nyuma mwanamke mrembo alikuwa english figure, leo hii matako makubwa ndii kila kiu, it's the matter of season.

Familia zenye mali nyingi wako makini na hili, wanawakikisha wanabalance mambo ili watoto wao wasijetumbukia kwenye lindi la umaskini. Ni majira yetu yako hivyo mkuu
 
Back
Top Bottom