Je, ni halali mke arithi mali mumewe akitangulia?

Je, ni halali mke arithi mali mumewe akitangulia?

Yaani unaoa kwa kufuata maelekezo ya wazazi? Kwani lazima wampende? Au wanakusaidia kutomba.a?
Oa kwa ajili yako na sio kwa ajili ya wazazi au mtu mwingine.

Mimi nilioa nikiyetaka mimi.

Wazazi wako walifanya jukumu la kukulea
Inaonekana wazaziwako hawakukulea vema, asante kwamtazamo wako. Ni kawaida kwa kizazi kipya kutoelewa mada
 
Mwandishi umeandika, lakini ulichoandika huna taarifa sahihi.
Umeandika mambo msingi katika maisha ya binadamu. Hapa umeandika Ndoa, Mume na Mke, Mali na urithi.
Ingefaa ukaelewa kama kila mume na mke wanaoishi pamoja ni ndoa?
Aidha, ungejiuliza: mume na mke wana sifa sawa? Ukweli ni kuwa, mume na mke wameumbwa tofauti hivi kwamba, mke ni msaidizi wa mume.
Kwa maneno mengine, na hapa nisieleweke kama nadharau wanawake la hasha! Kwa sababu hivi ndivyo walivyoumbwa. Mwanamke hana uwezo wa kumiliki mali, bila mwanaume!
Kuhusu mali hili ni suala ambalo lina misingi yake. Mali ili uipate na ili wengine waweze kuindeleza inahitaji sifa au sheria. Bila ya hizo sifa au sheria hakuna mali pia hakuna kurithi au kuendeleza mali.
Wajima bwana
Eti mwanamke hawezi miliki mali bila mwanaume
Unamjua Oprah Winfrey?.
 
Tatizo laanza kwa familia kumuona mke kama adui yao. Tukiondoa huo uchawi ndoa zetu zitakuwa imara sana na kuanzia hapo ndio mali na biashara zetu zitaendelea vizazi na vizazi.
Tukiwachukulia wanawake kama wachumaji tu. Au pale tunapokufa basi familia iwaone hawafai na familia ndiyo yenye haki ya kutawala mali ambazo wamechuma wao kutokea chini, hii ndo sababu kubwa ya hawa wanawake kujihami mapema
Inasikitisha wkt mke ndo huwa victim akinyang'anywa mali na ndugu wa mume

Km kweli wanamthamini km muendeleza ukoo wanachukua mali za nini?..

Wanawake ht km umejitoa vipi kujenga mji wako watu wanakuona mbaya wanataka wakuweke pembeni ss hio inakuaga ngumu
 
Kwa mujibu wa mila na desturi zetu za kisukuma ambazo zinapuuzwa kwa kiwango kikubwa sana nyakati hizi ni kwamba ikitokea mume amekufa na kuacha mjane basi huyo mjane ataolewa ndani ya huohuo ukoo.

Ikitokea mwanamke amekataa na anataka mali kwa mgongo wa watoto huyo huwa analazwa mahala pema peponi mapema sana.
kwa kifupi wanaume wenzangu ambao hamjaoa hadi sasa hakikisheni mnachuma kwanza mali kiwango cha kutosha ili kuepusha changamoto zijazo kama kuachana alafu mwanamke atake mgawo wa 50/50 n.k
Kuna shida gani mali kuandikishwa jina la watoto wa marehemu?.
 
Mkuu umesema kweli, ila tatizo linaanza na muoaji kutozingatia maagizo ya wazazi. Tunaoa vituko halafu tunawataka wazazi wawapokee, badala yake kwa sababu za kitabia wanapishana. Huo ndio mwanazo wa ugomvi. Tukianza kwa kuwasikiliza wazazi mengine yatakaa sawa.

Wazazi ni overrated, kusema uwasikilize kwa kila jambo hadi kuchagua mke ni kama walipoteza hela zao kusomesha. Dunia imebadilika, wazazi hawawezi kukaa na kuchagulia mtu mzima mke, mke unachagua mwenyewe unayempenda, msiwasikilize sana wazee wazamani watawalisha vitu wanavyoamini wao, mila na desturi za kizamani ambazo hazikuwafikisha popote.

Kama mtu umesoma basi tumia akili yako mwenyewe, ukishakua in y
 
Tumeachiwa urithi mbovu sana wa tabia, sijui na wakoloni au vizazi vilivyotangulia?! Mtazamo wangu ni kuwa mke ndiyo mrithi halali wa mali za mume, na wala si watoto wala ndugu wengine. Kila mtu atafute mali zake FULL STOP! Inatia kinyaa jitu kubwaa eti limekaa, vivu, zembe kusubiri mwingine mchapakazi, mtafutaji afe ligawiwe mali asiyoichuma!!!!
 
Mkuu Nyenyere,

Mtazamo wako upo sahihi kabisa.

Shida siku zinakimbia sana, mambo mengi yanabadilika: elimu, utamaduni, siasa, Imani, n.k. vyote vinabadilika kwa kasi sana kutokana na kuongezeka kwa muingiliano kati ya watu.

Ndio maana ndoa badala ya kuwa taasisi ya upendo inakuwa hisa ya 50% kwa 50%.
Huo ndio ukweli mkuu, ndoa si mwili mmoja tena, ni watu wawili ndani ya nyumba moja. Mpaka sasa tumebaki na kale kawoga ka kuwasaidia wazazi kwa mbali, lakini siku zinakuja ambapo itakuwa wazazi wakizaa wamemaliza, kila mtu kivyake tusijuane. Tutakuwa kama wanavyoishi ulaya na marekani sababu kila mmoja anaanzisha kiukoo chake na hakutakuwa na muunganiko wa ukoo tena.

Kizazi hiki kimeaminishwa kuwa kuendekeza udugu ni kukaribisha umaskini. Hivyo hata wazazi wamegeuka mzigo mkubwa kwani kila mtu anaishi kwa tamaa na ubinafsi!
 
Nadhani hujaelewa hata nilichoandika. Hakuna sehemu hata moja nimeandika mke ni adui kama chui, soma kwa uwazi. Nimelinganisha mifumo ya maisha kwa wana ndoa tu. Hiki ulichoandika ndio huo mfumo wa kizazi kipya chenye ubinafsi

Mali zangu nikifa kama nina mke wakati huo zote anabeba mke, sio ndugu wala nani mwingine, hadi tumependana na kuoana means I trust her 100% na ni my other half, nikiondoka kila kitu anabaki nacho.

Huo ni mtazamo wako ambao ni ule wa haki sawa. Why? Unaposema mkeo ni other half maana yake yeye si msaidizi tena, ni mwana hisa ambaye amewekeza asilimia 50 kama wewe nsdani ya ndoa. Hiyo haimaanishi hata kidogo kwamba ndio unamwamini zaidi kuliko wale wanaomchukulia mke kama sehemu ya ukoo wao. Tofauti kati ya huo mfumo wako na ule wa awali ni kuwa unajijengea ukoo wako mbali ni kuendeleza ukoo toka kwa wazazi, unakuwa umejitenga na jamii pana. Ni modern view ambapo mwanamke na mwanamume wako sawa kwa kila kitu ingawa hii ina defy natural law.

Kama nina watoto wakati huo najua sitooa jinga la kuwatupa, atawajali vizuri tu, na hakuna kulea watoto waje kua lazy, watoto walee wajue kujitafutia wenyewe, wakifika in their 20s hawahitaji hata hela za wazazi, wanakua na uwezo wa kujianzishia biashara wenyewe.

Hakuna atakaye kuoa mke mjinga, lakini wengi wa mtazamo wako wamekuja kulia majuto makuu. Process ya kupata mke mwema ni zaidi ya kupambana peke yako, inahitaji guidance, tena mke mwema anategemea malezi uliyolelewa ili kuweza kumtambua.

Watoto kufanya biashara wakifika kwenye 20s ni haja ya kila mzazi, ama wapate ajira. Kikubwa ni kuwa wajitegemee, na huo ndio mfumo wa awali ambao kwa kiasi kikubwa ulifanya hayo kwa ufanisi. Leo hii zimebaki wishful thinking tu kwa sababu mfumo wa sasa hausapoti kwa kiasi kikubwa mtazamo huo. Watoto wanafika umri huo wakiwa hawajitambui, hawana mtazamo wa future, wanatamani mwaishi kama kina Ja Rule huku hawana mbele wala nyuma. Wanashindana kukariri mashairi ya hiphop tu.

Unaposema hawahitaji hela za wazazi unakuwa umetoka nje ya mada. Kwani mzazi akifariki akaacha mali zake hupelekwa wapi? Kwenye NGO au kwenye taasisi za watoto yatima? Mtazamo huo ni wa kizazi kipya, disjointed usio na mtazamo mpana wa ukoo. Ni kama mtu anayeishi kisiwa cha peke yake akianzisha uzao wake. Ukweli ni kwamba kuna wakati mali za wazazi itabidi ziendelezwe hasa pale wanapokuwa wameacha mfumo mzuri wa kibiashara.

Swala ni kua na mke mwema tu, ukiwa na kilaza na mwenye tabia za kijinga sijui umeoa kwa sababu ipi. Ndugu watajijua aisee, wao kama walishindwa kunitumia vizuri wakafungua biashara zao wakati mi mzima, wasisumbue familia yangu kabisa nikiwa nimekufa, ni sawa na kusema mzee afe alafu uone ndugu wa baba waje kumsumbua mama, haimake sense kabisa.

Watu mnamuona mke ka chui, kama mwanamke huwezi kumuamini 100% basi usioe. I date a woman I can trust period. Love does exist

Hebu mtazame Bhahresa na mali zake, unadhani anaishi kwa mtazamo wako wewe kuwa watoto watafute mali zake na wamwache yeye wasihubutu kumwingilia? Je, ukoo wa Bharesa hawahusiki kwenye utajjri wake? Hayo ni mawazo ya maskini kuwa nikipata mali mtu asiniingilie. Hakuna anayekuingilia kwenye mali isipokuwa una mtazamo hasi.

Unapokosea ni pale unapotazama habari ya kugawana urithi, mimi naongelea kuendeleza mali za ukoo. Siku hizi kwa sababu ya ubinafsi kila mtu anajitazama yeye, hata hao watoto wako wanaweza kugombania hizo mali na mama yao kiasi pasibaki hata kijiko. Mzazi mwema ataacha mfumo mzuri wa kibiashara ama mfumo endelevu, ili watoto wafit naturally katika huo. Hakuna habari ya ndugu kurithi mali, bali ni mali iendelezwe. Ndivyo ilivyokuwa, sio kuuza ili wagawane, watoto walisimamia moja kwa moja.

Mambo ya kumwamini mke, yalikuwa na nguvu sana kwa mfumo wa zamani, sasa hivi ni hadithi tu mkuu, wake wa leo hawatoki makwao. Ukifikia kuoa utalijua hili, lakini kubwa zaidi unatafuta mali ili ukiondoka uwaache wanao sehemu nzuri, uache legacy ndani ya ukoo. Kama unaunda ukoo wako kupitia mwanamke basi sawa, lakini kama unaendeleza ukoo, mkeo atakuwa sehemu muhimu ya ukoo wenu, tena hutathubutu kuwaambia ndugu mniache na mke wangu.

Anyway, ni mtazamo wako mkuu ambao ndio modern view.
 
Inasikitisha wkt mke ndo huwa victim akinyang'anywa mali na ndugu wa mume

Km kweli wanamthamini km muendeleza ukoo wanachukua mali za nini?..

Wanawake ht km umejitoa vipi kujenga mji wako watu wanakuona mbaya wanataka wakuweke pembeni ss hio inakuaga ngumu
Kuna shida gani mali kuandikishwa jina la watoto wa marehemu?.
Mkuu, hapa tuko pamoja, why? Leo hii familia nyingi ziko disjointed, ndio maana mwanamke akiolewa anaanza kujiandaa kutoka. Yaani hakuna uhakika wa kuishi japo mwaka mmoja, kila siku ni mashaka tu. Suala la ndugu kugombea mali ni kwa sababu ya mfumo kuvurugika. Vijana wanaoa wake zao bila kuwashirikisha wazazi na pia wakishaoa wanasema huyu ni wangu mimi hivyo mniache msiniingilie.

Haya yanasababisha mke asitambulike ama kukubalika ndani ya ukoo. Sisi wanaume ndio chanzo cha yote hayo, tumeiga western culture ambayo imeharibika. Lakini cha ajabu wenye mali nyingi hawako hivyo, wanaishi mfumo wa kale. Angalia wahindi na waarabu mfano, angalia matajiri wakubwa huko ulaya, wanaishi kwa kushirikisha koo zao kiasi kwamba utajiri wao unazunguka ndani ya ukoo, ndio concept. Sisi masikini tunapenda tuwe tofauti na wote kwenye koo zetu tuweze kutukuzwa.

Mfumo wa sasa ni wa "abiria chunga mzigo wako"
 
Wazazi ni overrated, kusema uwasikilize kwa kila jambo hadi kuchagua mke ni kama walipoteza hela zao kusomesha. Dunia imebadilika, wazazi hawawezi kukaa na kuchagulia mtu mzima mke, mke unachagua mwenyewe unayempenda, msiwasikilize sana wazee wazamani watawalisha vitu wanavyoamini wao, mila na desturi za kizamani ambazo hazikuwafikisha popote.

Kama mtu umesoma basi tumia akili yako mwenyewe, ukishakua in y
Na hapa ndipo penye tatizo, kusoma kusiondoe maarifa. Wazazi wanafanya mambo kwa experience, wameishi miaka mingi, wamepitia mengi. Wakati wewe ndio kwanza unajiandaa kuingia kwenye ndoa na elimu yakko na akili zako za darasani, wao wako karibu kabisa kuiaga dunia baada ya kuishi miaka mingi kwenye ndoa. Wao wana elimu kubwa ya maisha lich ya degree zako.

Huwezi kuwazidi wazazi experience, ongelea mambo ya kazi na elimu ya darasani. Usiqadharau wazazi mkuu, wana mchango katika maisha. Pia kumbuka mtoto hakui kwa wazazi.
 
Tumeachiwa urithi mbovu sana wa tabia, sijui na wakoloni au vizazi vilivyotangulia?! Mtazamo wangu ni kuwa mke ndiyo mrithi halali wa mali za mume, na wala si watoto wala ndugu wengine. Kila mtu atafute mali zake FULL STOP! Inatia kinyaa jitu kubwaa eti limekaa, vivu, zembe kusubiri mwingine mchapakazi, mtafutaji afe ligawiwe mali asiyoichuma!!!!
Wrong on all accounts!! Umepotoshwa na huelewi urithi unakuwaje, nadhani umefundishwa kugawana mali, umepotezwa vibaya. Anyway ni sahihi kwa mtazamo wako, mkeo ndio mrihi wako.
 
Uko sahihi na ninakubaliana na hoja zako ila zama zina badilika mimi kusema kweli siwezi kuchaguliwa mke kamwe lazima nimpende mwenyewe huo ndyo uhalisia wa maisha ya sasa hivyo toa mbinu n nini kifanyike ili maisha yasonge ila syo kwa kuchaguliwa waume au wake
 
Mengine nimeacha ku-comment. Lakini nikuulize, kwanini usubirie ndugu yako afe ukarithi mali yake? Kwanini usitafute ya kwako?

Mkuu kwenye kuthamini watoto wa jinsia zote bila kubagua tupo pamoja.

Endapo hii sehem ya mwisho niliyoinukuu ni ya kweli na unaiamini, naona watoto wanachohitaji sana kutoka kwetu ni malezi bora na elimu basi. Mali na mengine watajitafutia zakwao.
 
Siku hizi mali tunasaidiana kutafuta, kama ni biashara mke nae anakuwa anafanya kazi kwenye hizo biashara kwa hiyo mume akifa automatically mali zinaangukia mikononi mwa mwanamke
 
Wrong on all accounts!! Umepotoshwa na huelewi urithi unakuwaje, nadhani umefundishwa kugawana mali, umepotezwa vibaya. Anyway ni sahihi kwa mtazamo wako, mkeo ndio mrihi wako.
Hebu nieleweshe mkuu. Maana urithi wa asili ni wa sura, tabia na mambo utakayomrithi wa/mzazi wako tu vinginevyo chagua wewe neno linalokupendezea. Ndiyo, mke wangu atanirithi na si wa/mwanangu. Tafuta chako.
 
Back
Top Bottom