Je ngono ndio inayotambulika rasmi kiimani?

Je ngono ndio inayotambulika rasmi kiimani?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,666
Reaction score
860,961
1471628755570.jpg
ni mjadala mkongwe zaidi duniani, mjadala wa vizazi na vizazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu kwa muktadha wa kiimani
Ni mjadala tata kuhusiana na kile kilichotokea pale Eden na ukweli kuhusu dhambi ya asili....kimsingi ni mjadala usioisha nguvu wala kuchuja! Ulikuwepo upo na utakuwepo! Mjadala wa ngono uzinzi uasherati na majina yake mengi...!
1471629027384.jpg
...shetani naye ana dini yake na mojawapo ya ibada zake muhimu ni hili tendo la kufanya ngono hadharani, hili linahusishwa na kile kitendo cha pale Eden, kwamba ile dhambi ya asili ni ngono! Kwenye satanism ngono ina nafasi kubwa sana..naweza kukiri ni zaidi ya asilimia 90! Ibada ya kishetani bila tendo la ngono haijakamilika
1471629251243.jpg
mfanano wa kushangaza no kwamba kwenye imani nyingi kama si zote zinazoamini katika Mungu mmoja kitendo cha kuzaa nje ya ndoa ndio dhambi kubwa inayokutenga na imani yako na ili uweze kurudishwa kundini tena kuna ibada maalum na rasmi kwa ajili ya tendo hilo (ibada ya kurudi kundini )
Tafsiri ya dhambi
Ni jambo lolote lile lenye madhara ama kwa mtenda au kwa mtendewa lakini kiimani ni jambo lolote lile linalokwenda kinyume na mapenzi ya Mungu
1471629609915.jpg
...kwenye kanuni za kikristo kumeainishwa dhambi nyingi tu lakini hizi zote hazipewi uzito mkubwa kama ngono! Kwenye imani za wenzetu wengine kitendo cha mwanamke kukutwa amezini bila ndoa adhabu yake ni kupigwa mawe hadi kufa! Mwanaume akiachwa anapeta mitaani na hahesabiwi hatia hata kama alimlazimisha mwanamke husika kufanya naye ngono
1471629863498.jpg
hii hali imekuwa ni kama desturi na mapokeo vizazi na vizazi, hata leo hii ni rahisi sana mwanaume kukubalika kwenye mahusiano hata kama ana mtoto tayari kwa mwanamke mwingine kuliko mwanamke ambaye ana mtoto kwa mwanaume mwingine
Baadhi ya imani zinaruhusu ndoa za mitala , lakini kamwe huwezi kukuta mwanamke anachangia wanaume zaidi ya mmoja kihalali
Vyovyote vile iwavyo bado ngono inaonekana ndio dhambi halisi na mwathirika mkubwa akiwa ni mwanamke
1471630267767.jpg
 
Kupost tu hizi picha umeshatenda zambi ya kuwatamanisha watu
Kwakuwa tayari mind yako imekuwa possessed na huyo shetani.....
1471630724357.jpg
1471630727900.jpg
1471630740607.jpg
ni mara chache mno kukuta mwanaume akikumbana na adhabu hii hasa kwa suala linalohusu ngono na nje ya imani
Wakati kwa shetani ngono ikiwa ni ibada kwa Mungu ni dhambi ambayo msamaha wake ni ibada maalum. ..
 
utakuwa una matatizo ya kihisia kama umetamanishwa hapo.
Na hapa ndio wengi waliposhindiwa...ukisikia mshika dini ama mlokole kaanguka dhambini asilimia 90 huwa ni mambo yanayohusiasa na ngono
somo zuri ila fupi....ila ata mimi nipo pamoja na wewe maana dhambi ya zinaa bwana duh....wengi wataacha vyote ila kuacha kuzini ni shida
 
Hivi Mshana ni lini utaachana na hizi myth za Eden???...zime kuadict vibaya sana...Ngono ni tendo la asili kabisa...linatokea kwa jamii zote za viumbe hai...hadi mimea inangonoka pia, kusema ni dhambi ni mawazo ya watu tu...Kwahiyo jogoo naye anatenda dhambi pindi anapongonoka???...Mafundisho ya dini karibia yote yapo against nature ndo maana hayaeleweki wala kufanikiwa, si umewahi kuona viongozi wa dini wanachepuka???...waache kuwatisha watu kwa kutumia vitisho hewa.
 
Hivi Mshana ni lini utaachana na hizi myth za Eden???...zime kuadict vibaya sana...Ngono ni tendo la asili kabisa...linatokea kwa jamii zote za viumbe hai...hadi mimea inangonoka pia, kusema ni dhambi ni mawazo ya watu tu...Kwahiyo jogoo naye anatenda dhambi pindi anapongonoka???...Mafundisho ya dini karibia yote yapo against nature ndo maana hayaeleweki wala kufanikiwa, si umewahi kuona viongozi wa dini wanachepuka???...waache kuwatisha watu kwa kutumia vitisho hewa.
Sijakuelewa kabisa hebu rudia kusoma tena nilichoandika halafu uniambie nimetisha wapi? je nilichoandika hakifanyiki kwenye dini zetu? Je si kweli kwamba mijadala ya ngono haiishi kila mahali? Je ni uongo kwamba kwenye satanism ngono ndio hukamilisha ibada?umesoma kwa kukurupuka rudia kusoma kwa kutulia tafadhali
 
Ujue Mshana sijawahi kuelewa mada zako?
Zimekaa kichawichawi sana.
[emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji87] [emoji87] [emoji87] [emoji87] [emoji87] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125]
 
Moderator nimeomba msaada wa kurekebisha heading tangu jana naona kimya mpaka sasa tatizo ninini???
 
Back
Top Bottom